Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United Vs Celta Vigo

Katika moja ya game za kuziangalia hii nayo si ya kukosa,Man U ya Mourihno imeshapoteza matumaini ya kuwa mmoja wa timu zitakazokuwa Top 4,Mourihno Vita ameihamishia kwenye Europa,ukiangalia Man U ilivyocheza katika ligi na Asernal utaona kabisa haikuwa na cha kupoteza,Kiakili Mourihno hakuutilia manani mchezo ule,alirelax alikubaliana na matokeo ya aina yeyote, hakuamini katika Ushindi ndio mana hakuwasumbua wachezaji wake,tulivyofungwa goli mbili alichofanya ni kuja kuzuia tusifungwe mengi Zaidi ndio mana alilazimika kufanya mabadiliko yale.

Game ya leo itakuwa ni game ya Vita,ni kama ile na Chelsea,Game plan,akili ya Mourihno MovemeMourohno,wachezaji na Matumaini ya Mashabiki ni kushinda game ya leo.

Sioni dalili na uwezekano wa kupoteza mchezo wa leo,Mou ameshawasoma Celta vigo vizuri na amefanya kazi yake vizuri kwa kujuwa all possibilities za kupoteza mchezo wa leo,hatoruhusu hilo litokee.

Leo kila mchezaji ana majukumu yake uwanjani na atacheza vile anavyotaka Mourihno,tunakumbuka kazi ya Herera kwa Hazard,alihakikisha Hazard hachezi na kupandisha timu yake,na kweli alifanikiwa ndio kitachofanyika Leo.

Tutegemee mabadiliko makubwa ya Man United kimchezo Leo,utapigwa mpira Mwingi sana leo,wachezaji wamepumzika vya kutosha kimwili na kiakili.

Celta de Vigo hawana cha kupoteza;wao ni kutafuta Ushindi tu,ndio utamu wa natch ya leo.

Leo Mourihno hakai chini muda wote wa Mpira.

Ila Mpira unadunda,uamuzi dakika tisini,ila Mou hajawahi kuniangusha katika Michezo ya namna hii,hajawahi kuniangusha anapokuwa na uhakika anapotoa kauli ya Ushindi.

Defencive ya Man U katika michuano hii ni ya uhakika,imeyumba kidogo baada ya Muhuni wa Ki Argentina Marcus Rojo kuumia,Lakini Ukuta wa Chuma chini ya Jemedari wa Kisenergal Eric Baily na uwepo wa David De Gea langoni unatuhakikishia ulinzi wa uhakika.

Tegemeo la Ushindi leo ni Marcus Rashford.

Man United 2 - Celta de Vigo 1.

Karibu Old T,Njoo
 
Nimekusoma mkuu, uchambuzi mzuri
 
Kwanini siku za hivi karibuni Mourihno ameamua kuanza na S. Romeo kama golikipa namba moja badala ya De Gea.

Huku tunafahamu Ubora na umuhimu wa De Gea,na tunafahamu mara nyingi makipa huwa hawa busy kuchoka kama wachezaji wa ndani?

De Gea ana majeruhi?au ndio maandalizi ya kwenda Madrid?
 
Aisee fellain na lingard wanakua kwenye first IX kwenye mechi yenye umuhimu kama hii, alafu unajiuliza inakuaje tupo wa sita?
Chief Wana umuhimu mkubwa sana kaka,kwa mfumo unaotumika wanapata nafasi ya moja kwa moja,hawa Celta de Vigo ni wa kukabia kuanzia kwao ili kupunguza mashambulizi kwetu,so leo Mpira utapigwa sana katikati au upande mmoja wa goli.

Tukumbuke,Martial, Mata sio wakabaji, na ili kubalance lazima tuwe na wachezaji sita Wenye kariba ya uzuiaji.
 
kuna mechi yoyote ya europa umemuona de gea ana daka?
kwa lugha rahisi ni kwamba tunaenda kujilinda?
 
kuna mechi yoyote ya europa umemuona de gea ana daka?

kwa lugha rahisi ni kwamba tunaenda kujilinda?
Yeah sure tunajilinda na hapo hapo tunashambulia kwa kasi,na hiyo kazi,Herera,Lingard na Fellain wanaiweza.

Ondoa shaka,tutapiga mpira Mwingi sana leo.
 
Sio siku za karibuni mkuu, kwenye michuano ya europa Romero amecheza almost mechi zote, huku de gea akicheza nyingi sana za premier
 
Manutd hawajawahi kupoteza mechi ya pili katia historia yao baada ya kushinda ya kwanza kwenye mashindano ya Europa
 
Sio siku za karibuni mkuu, kwenye michuano ya europa Romero amecheza almost mechi zote, huku de gea akicheza nyingi sana za premier
Shukrani Mkuu,sikuwa makini kuliona hili,ila nadhani Fainal de Gea atasimama
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…