wakati man utd inamsajili michael carrick kama sikosei nilikua darasa la 6 kiukweli sikuamini kabisa kama ataziba nafasi ya mwendawazimu roy keane kwa sababu yupo taratibu sana.ni miaka 10 sasa mwenzenu nimegundua kuwa michael si mwanaadamu wa kawaida,pia nimepata kugundua kuwa yule zeruzeru (scholes) ambaye tokea niifahamu man utd mwaka 2001 nikiwa na miaka 8 mpaka anastaafu soka sijawahi kufahamu mshara wake na wala sijawahi kumfahamu wakala wake ndiye aliyenifanya nimuone michael carrick ni mchezaji wa kawaida.kwa kupitia thread hii ya wapenzi wa man utd natangaza rasmi kuwa ni
team michael 16 kuanzia leo na pia hii itakuwa ni miongoni mwa thread nitakayoitembelea kila siku hapa jamiiforums na kutoa mawazo yangu kuhusu red devils.kumuangalia
michael 16 akicheza mpira ni burudani zaidi kuliko kuangalia live show za wasanii wa kibongo.