Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Wanazi wa Man jana tulipigwa kipigo sawa na cha mtoto mtukutu aliyemwaga supu ya Mzazi.Ukweli niliumia sana kiasi nikaamua kunywa mvinyo wangu kuugulia maumivu.

Katika mpira kuna matokeo aina tatu,kufungwa,kufunga na kutoka sare matokeo ya aina yoyote utegemea mipango ya Mwalimu na mwitikio wa wachezaji.

Mourinho alisajili wachezaji wawili ambao nilifikiri aina ya uchezaji katika msimu huu ingekuwa kushambulia zaidi kuliko kupaki bus.Paul Pogba na Mkhitaryan ukiongeza na wachezaji aliowakuta kama Anthony Martial,Rashford na Mata nilitegemea Mourinho angetenegeza mfumo wa kushambulia zaidi ambao ndio utamaduni wa Manchester United.

Mchezo wa jana mipango yote ilitbuliwa na bao la mapema,kama uliangalia mchezo vizuri bila kengeza la ushabiki Lingard na Rashford walikuwa wakicheza kama mabeki zaidi kuliko kushambulia.Kwa maneno mengine kama si bao la mapema tungeiona Manchester ikipaki bus kama walivyocheza na Liverpool.

Tangu Mwanzo nilikuwa nabishana na wanazi wenzangu wa Manchester United juu ya ujio wa Mourinho kwasababu moja kubwa sana tena sana MFUMO WAKE tangu akiwa Porto na baadae Chalsea ni kuzuia zaidi kuliko kushambulia.Si kwamba nakataa Mourinho si kocha mzuri la hasha nakubali kabisa ni mwalimu mwenye mafanikio makubwa sana ukilinganisha na umri wake lakini mfumo wake si rafiki na mfumo tuliozoea kuuona Manchester United ikiutumia mara kwa mara.

Bado ligi ipo katika hatua za mwanzo sana,ni vizuri tumeona udhaifu wetu timu inapocheza na timu imara,timu kubwa lazima tubadilike tuache mtindo wa kupaki bus tushambulie.Chelsea iliyotufunga jana iligaragazwa na Liverpool na Arsenal kwakuwa walishambuliwa tungejipanga kushambulia.

Manutd for life.
 
Spend the money wisely,simply glory time is over mmebaki jina ukiangalia hakuna jipya nilisema na narudia tena Mourinho atatupa furaha sana msimu kama alivyo tufurahisha msimu uliopita.

Nawakumbusheni tu jana mmegongeka 4-0 pale darajani na mlizibwa matundu yote ya kutolea hewa next tym kuweni na nidhamu alafu kelele za kua eti ni mechi ya 9 hatutaki maana mliongea sana game 3 za mwanzo......Man 4ngo.
 
Hahahhahha jirani midomo imepewa kuongea,kuhusu kubaki jina basi nyie mwaongoza, jirani kwa upande wa kuongea aisee hatuwashindi nyie mwaongoza ndo maana yakiwazidi kitanzi kinakuwa solution kwenu....
 
Hahahhahha jirani midomo imepewa kuongea,kuhusu kubaki jina basi nyie mwaongoza, jirani kwa upande wa kuongea aisee hatuwashindi nyie mwaongoza ndo maana yakiwazidi kitanzi kinakuwa solution kwenu....

Tatizo lako jirani ni kua hautaki kukubali kua Fergie kaondoka na identity yenu bado unaamini wewe ni giant sana bado unajifariji kua kukosa kwako UCL ni bahati mbaya tu kumbe ni uhalisia kua haustahili kuwepo na njia unayoitumia kujipanga ndio mbovu zaidi after babu mmeajiri waalimu watatu ambao hakuna jipya so far ni wale wale na tumeanza kufanana nna uhakika j5 utapata matokeo chanya utakuja hapa kwa vurugu sana kua mmerudi mnasahau kua mna kansa.
 
Shindwa na ulegeeee hatuna kansa siye...!!!!...... jirani unajua kujenga ni kazi kuliko kubomoa ,tupo tunajitahidi kujenga tutoke tulipo sasa jirani yangu ulitaka tuendelee kugalagala tu kwenye matope tu na kulia ilihali hatuna juhudi zozote za kujitoa ?. .....mtafutaji hachoki ,Wacha tu tubadilishe... tunatafuta tunachokipata tutafanikiwa tu.
 
Nilijitoa Man Utd toka mourinho atangazwe kocha pale, nitarudi akishaondoka sijawahi kushawishika na mourinho toka nimjue, nilisema mwanzo bora abaki LVG au mrudisheni Moyes Lakini mourinho ni mbovu kuzidi wote
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…