Quenda kwenda CFC habari nzuri sana, UTD kwa namna ilitaka mtumia ingekuwa ni kuchelewesha maendeleo yake. Kingine dili lake linampa nguvu kubwa sana "AGENT" juu ya timu. (CFC Hawajui nini wanataka pale maana wana Palmer, Paez, Estevao, Neto, Madueke, Tyrique, Wote wanaweza kuwa RW/LW)
Kuna mbadala wa Quenda, Roger Fernandes, Kwa ile role ya RWB kama timu inataka kwenda na (Unorthodox WB's) yeye ni bora zaidi kwenye kuzuia,
Mpira unabadilika na tunaokelekea hii 3 CB's itakuwa ni mfumo wa kuendea, Bundesliga wahafidhina wa 4~3~3 wengi wanaswitch kwenye 3~4~3 na Variations zake (3~4~1~2, 3~4~2~1)
Serie A karibu nusu ya timu ligi nzima zinaenda na mfumo huu, Ligue 1 nao mpaka De Zerbi ndo umekuwa mfumo wake rasmi.
Huu mfumo unahitaji "Zonal Experts" na ukitoa CB's eneo lingine muhimu zaidi kwenye mfumo huu ni WB's (Wingbacks) Ila bado naamini kwa Traditional WB's kwa kuanzia UTD ingepambana kumpata Vanderson ama Raoul Bellanova. Yule Frimpong ile Physicality yake kwa EPL changamoto (aina za Lamptey + Barco) UTD inatakiwa fanya Bullying hayo maeneo kama Dorgu namna anafanya (unavamia). EPL Combo bora kufanya vizuri ni (Physicality + Technicality) Hii ukiongeza na Mentality ambayo Mwalimu ana sehemu yake kubwa pamoja na idara ya Usajili mafanikio ni nje nje.