Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Binafsi sijawahi kuwa muumini wa wachezaji wavivu! Rashford yupo hili kundi, Ila penye sifa zinazostahili inabidi tuzitoe! anajitahidi msimu huu na mpira wa kisasa ukiwa unajituma mara nyingi nafasi zinajitokezaga ukiwa maeneo sahihi,

Bruno ni muhanga mwingine wa kupoteza form yake, INEOS kama wangemuuza binafsi ningewaelewa ila kabaki nawaelewa pia, Bruno ni MD ambae hawezi ku-contorl game timu ikiwa inamiliki mpira zaidi, timu zikiiachia UTD icheze Bruno ufanisi wote unapotea,

ETH ni sababu presha ipo juu ila angejilipua kujaribu 4~4~2 ya Hojlund na Zirkzee kwa pamoja baadhi ya michezo na kwa 4~2~3~1 yake ajaribu Garnacho LW, Amad AM, Rashy RW, baadhi ya michezo ili Bruno apunguziwe ile presha ya kupoteza fomu yake

Bagabeach niliku~quote post #203,068 Hii ilikuwa maoni ya muendelezo kwenye post yako
 
Xavi Hernandez na baadae Hans Flick wameirejesha kwa namna fulani heshima ya LA MASIA.

natamani siku moja kuiona United ikitamba ndani ya uwanja kupitia vijana wake.

Tupunguze woga, khofu na presha ya kutaka kurudi juu kwa haraka.

Hatimaye klabu inaishia kufanya sajili za kitapeli.

Kuna vijana mfano wa mantato benedito, bianchineri (sijui nimeandika sahihi), ibragimovic, lacey, amass na wengineo ambao wamekuwa wakiondolewa Kila mwaka kwa kukosa kuaminiwa.
 
Naiogopa zaidi Manchester united ya nje ya uwanja kuliko ya ndani ya uwanja.
Nimeshazoweshwa na vipigo vilivyodumu kwa miaka 10 ila nafsi yangu bado haijakubali kuzowea sajili za ovyo.
 
Timu yetu kwa kweli haivutii kutizama wachezaji wetu ni kama wamechoka sana, hawachezi kitimu yaani kila mtu kivyake vyake. Timu ndio maana kuna wachezaji kama Zirkzee akacheza timu ya Taifa anaperform akija utd anaonekana hachezi vizur hii ni kwa sababu timu haina muunganiko ukiangalia touch za Zirkzee ni nzuri mno hasa kwenye kucheza one two na kuweka mpira kwenye njia ila muda mwingi unakuta mtu hayupo. Kwa style yake ya uchezaji angekuwa yupo Arsenal au City nadhani angekuwa anazingumzwa sana kwa sasa. Tatizo hadi sasa mimi naona ni style ya uchezaji wa kocha yaani muda mwingi mpira unapigwa back pass hakuna mipira mirefe inayopigwa kwa winga kwa ajili ya kuanzisha mashambulizi au kwa ceter forward wao wanataka wapige pass kuanzia nyuma hadi wafike mbele, huu ni mpira wa kizamani sana ndio maans majeruhi kwentu hayaishi sababu wachezAji wetu wapigiana vipasi vifupi vifupi hivyo inakuwa rahisi kufikwa.
 
Out of the 36 teams in the Europa League, 12 remain unbeaten after three matchdays, with Manchester United being one of them.
 
Kama unapitia magumu yoyote na unahitaji kupata mganga, ongea na EtH πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…