El Tiger
Senior Member
- Aug 15, 2018
- 142
- 785
Umemaliza Mkuu! Nadhani Mashabiki wengi wa UTD walikuwa wanataka ETH aendelee kuwemo na Sababu Mingi Umeziweka wazi, NIDHAMU, ACADEMY, MORALI, Ila kikubwa ambacho nadhani hajapata Sapoti ya Kutosha kukirudisha ni ile wanasema UTD DNA ila anaweza irudisha taratibu kwa Mazingira ya Uongozi Mpya,Hii habari imenifurahisha sana. Kamwe sikuwahi kuwa na mashaka na Ten Hag. Kwangu mimi ndio kocha bora utd kumpata baaada ya Sir Ferg. Nasema hivyo kwa sababu anatabia na falsafa fulan kama za Sir Ferg ambazo ndio ziliifikisha utd pale ilipo.
Kwanza hacheki na kima na haangali jina la mchezaji, awe mkubwa awe mdogo akizingua anamzingua na anamuondoa kwenye timu au kupiga mnada Ole guna alikuwa kocha mzuri hili lilimshinda na alikuwa na kijitabia cha ubaguzi kwa baadhi ya wachezaji kwa kuwanyima nafasi, huwezi kuwa na Cavan benchi halafu Martial anacheza dakika 90 na hakupi matokeo vivyo hivyo kwa Igalo dhidi ya Martial. Erick kawanyoo
sha mfano Ronaldo, Pogba kuuzwa Sancho kutolewa kwa mkopo na Maguire kuvuliwa ucaptain.
Pili anaibua vijana kutoka academy hii inaonesha anajua kufundisha mpira na hichi kitu ndio mafanikio ya utd. Vijana wa academy siku zote ni wafia timu. Tatu ni kocha wa vikombe, pamoja na wakati mgumu aliyepitia katika misimu yake miwili kachukua vikombe viwili hii inaonesha ana uwezo wa kuchukua kombe katika mazingira yeyote.
Kilicho mgharimu Ten hag ni majeruhi ya muda mrefu ya wachezaji wake muhimu hasa aliyewasajili wamekuwa wakipishana kwenye majeruhi na hii ilimuharibia mipango yake toka msimu wa kwanza na kubadilisha hata style ya uchezaji. Kuna kipindi Casemiro akiwa kiungo tegemeo wa timu alipata majeruhi ya muda mrefu mara makadi mekundu timu ikaanza kudrop point ikiwa kwenye kinyang'anyiro cha ubingwa.
Kuna wakati Luca Show,Varane, Malacia ,Bisaka wote kwa pamoja walikuwa majeruhi lakini bado timu ilipambana. Unakuta timu inastraika kama Martial tena majeruhi, winga mvivu kama Sancho na Rashford lakini bado jamaa alipambana. Mimi naami jamaa kafanikiwa sana hasa kwenye nidhamu ya timu na kuwapa hamasa vijana hii imewapa alert wakubwa hasa wavivu kama Rashford. Naamini kuanzia msimu ujao utd itaanza kuwa ya moto maana kutakuwa na ushindani mkubwa wa number na hata vijana wa academy wengi watapanda hivyo wazee wakae chonjo. Naona kabisa utawala wa City ya Pep na Liver ya Klopp unakaribia kuisha unarudi utawala wa utd na arsenal ila kwa sasa ni Ten hag na Ateta.
Changamoto amepitia Kubwa naweza sema ni Uongozi wa Kimichezo Juu yake. Kuna Suala la Miundombinu ishu za Majeraha, Usajili, Nguvu kubwa ya Wachezaji toka kwenye Mikataba, Pamoja na Media
Poch, RDZ, Potter, ni walimu wa Timu za Kati, Huwezi enda tafuta Ubingwa nao labda ukubali wewe unatengeneza Project yako. TT Sijawahi Jua ni Mwalimu mzuri kwenye kitu gani! Leicester yenyewe ilifanya Maajabu na Mwalimu Mzoefu Ranieri.