Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ila huko baadae tutaweka kipengele katk mkataba kwamba ukizingua kama alivyofanya glazers tunakuondoa kwa sheria
Changamoto kubwa UTD tayari ipo katika Soko la Hisa la NYSE. Kuweka sheria labda timu ingechukuliwa na Mtu mmoja kama Kina King faisal na Flano wanavyopendekeza. Timu angemiliki Mtu mmoja ingekuwa rahisi.

Kwa sasa twende nao tu hivyo hivyo Muhimu wafanye Machaguzi Bora yatayoleta Performance nzuri Uwanjani. Mara nyingi Mashabiki Mapato yanatugusa ila sio sana kama Matokeo Mabovu.

Glazzer kuanzia Anainunua UTD Fergie alishamkataa na alishatakaga achia timu Mara kadhaa sababu yake ila Yule Mama Cathy kuna attempts kadhaa alimzuia. Timu imedondokea kwa watoto ndo imekuwa changamoto haswa.
 
Hawa watoto wa glazzers wakiongozwa na Avram ndio wanaiteketeza kabisa mkuu
 
Naomba kujua ni mchezaji gani amemuudhi tajiri Ratcliffe hadi kutamka hataki kumuona tena kwenye Timu ?
 
Wiki hii italeta presha mpya kwa meneja wa hii club Erik ten Hag, huku jukumu lake kama meneja wa klabu halijahakikishiwa kuendelea hadi msimu ujao. Tangu INEOS ilipopata umiliki wao wa hisa chache wa klabu imekuwa wazi kuwa Ten Hag alikuwa akichunguzwa kwa matokeo, uchezaji na ujumuisho wa timu.

Kumekuwa na matukio makubwa - kwa kawaida malengo makubwa ya timu ingawa, badala ya utawala kamili wa mchezo. Kwa hivyo uongozi wa United unafikiria kama yeye ndiye mtu wa kuwaongoza mbele. Iwapo United watapata draw leo na Tenhug akaomba kazi hiyo, je ataipata? Hicho ndicho United wanajaribu kuamua. Bado inaweza kuwa kwamba anabaki kuwa mgombea bora wa kazi hiyo. Hakuna wasimamizi wengi wenye uzoefu wa soka la kisasa wanaopatikana sokoni.
 
Bahati nzuri leo mko na Sheffield, mjipigie kadri mtakavyo.
 
Ya kweli haya?

NEW: Jason Wilcox has told Erik ten Hag he must play the “new” #mufc way, starting against Sheffield United.

If Ten Hag does not deliver a possession-based style of play in the remaining weeks of the season, his future looks limited.

[
@reluctantnicko
]
 
Bahati nzuri leo mko na Sheffield, mjipigie kadri mtakavyo.
Wewe ndio unamzarau Sheffield, ila kwa hii Man Utd yetu hio mechi na Sheffield inaweza kua kama fainali na wanaweza wakatugonga vilevile kama sio kutoa draw.
Hii timu yetu dakika 90 zote inazocheza mashabiki hua roho mkononi, mpaka tusikie kipenga cha mwisho kinapulizwa ndio tunashusha pumzi kama tumeambulia points3

 
Usiwe na shaka hapo bro.

Wewe jione kama Tobiti na Sheffield ni malaika aliyekuja kukukiga tafu katikati ya safari ngumu 😄😄
 
Kusema kweli mimi nilikuwa muumini mzuri wa Teg Hag akiwa na Ajax yake. Nilitegemea ule mpira aliokuwa anaubonda Ajax auhamishie United pindi akianza kazi. Lakini ameniangusha sana hadi amewapa akina Masingeli cha kuongea.

Tuseme hakupata first target zake kwa kila mchezaji aliyeletwa kwenye utawala wake, lakini wachezaji hao wa second and third choices wamekuwa na ubora kwa 70% kwa matakwa yake. Ukiwalinganisha hao wachezaji na wachezaji wa timu kama everton, brentford, palace, fulham, luton n.k wa kwake wana ubora mkubwa. Lakini mbona bado timu ina struggle sana kiuchezaji kila mechi tunayocheza na hao vibonde kama shida ni ubora wa wachezaji? Ubora wa wachezaji ulitakiwa umuathiri kwenye mechi kubwa za top 4 au top 6 na sio kwenye kila mechi.

Teg Hag afundishe mpira asijifiche kwenye kivuli cha target na majeruhi. Atleast atupatie kimoja wapo kama ya hivi: mpira mzuri ila matokeo ya kubahatisha au matokeo mazuri yenye mpia mbovu sababu amekosa target zake. Lakini kwa sasa vyote hivyo ni anasa kwa timu yetu.

Binafsi simuungi mkono kuendelea na united kuanzia msimu ujao.
 
3-0 juzi nilishangaa sana

Tena wakatupenyezea la nne thanks to var
 
Nilikuwa sina mpango wa kwenda kuchek gemu ila kikosi cha Leo nimeona kipo vizuri...

Casemiro kaludi kula mkoba Antony na Ercksen wameanza...

Mpemba leo hayupo 🤝

Nadhani kuna burudani leo naweza pata

GGMU
 
Japokuwa list ya majeruhi ni ndefu lakini kwa namna yoyote McTOMINAY ambaye ni mfungaji wetu bora anatakiwa aanze. Sijui ni kitu gani kinamuweka benchi AMAD, mara zote anazoingia unaona kabisa uwezo wake. Muambieni huyo mjinga ETH na leo amtoe tena MAINOO auone mziki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…