Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Thiago motta vs simone inzaghi
Inzaghi na Xabi wanazungumzwa sana na ni kwa Kustahili. Mwisho wa siku Pia wako Smart sana kwenye Sajili zao angalia Free Transfers zingine Dau dogo

Kuzungumzwa kwa Inzaghi na Xabi, Kunambeba Motta na Hoeness wa Stuttgart, Motta kila kitu kinajieleza, Ila Hoeness anaweza kuja kuwa Tatizo mbeleni. Stuttgart mwanzoni mwa Msimu wengi tuliona ni Fluke na yule Guirassy anaweka tu Rekodi.

Wale VFB Ni tatizo Jipya na Huyu Hoeness kafanya Maamuzi mazuri sana kubaki Pale. Mpira wake ni Mchanganyiko wa Possession + Transition, Nibakize Maneno ila ana uwezekano wa kuwa jina kubwa mno, Germany wana Walimu asee ila Tuchel HAPANA.. Stuttgart vs Bayer 04 nadhani ni Mechi bora za msimu Bundesliga, Alonso alikuwa haelewi {Ligi na ile ya DFB Pokal}. Mwisho wote wana timu Nzur za Uongozi.
 
Ukiangalia hii mechi ya wenzetu City na Liverpool unashindwa kuelewa United inacheza mpira ili kutimiza lengo gani haswa!
Hupati ushindi, huchezi mpira wa kuvutia na wala hauoni dalili ya kuondoka na kikombe wala kimoja.
Ushindi Man United wanapata ila hawana consistent.

Solkajer alikosa ubingwa wa EPL 2020/2021 kwa kupata sare nyingi sana mwezi January na February.

Msimu huu Ten Hag amepoteza mwelekeo kwa kufungwa mechi nyingi zaidi.

Mechi sita tu kati ya kumi na moja alizopoteza angekuwa anaongoza ligi.

Injury nyingi na squad depth ndogo sana kimetuangusha sana yapo mapungufu ya mwalimu ila kikosi chetu ni kidogo sana ukilinganisha na timu zote za top ten.
 
Pamoja na hilo kocha a achangiwe kwa nn hawaamini watoto.wa academy eti anawatafuta saa hizi
Huwezi tu ukawaamini wachezaji wa academy lazima wawe na quality hata sasa ameshatumia wachezaji wa academy watano msimu huu peke yake.
 
Ligi ya Italy wachezaji wanatumia performance enhancers ndiyo maana hata wazee wanaweza kukimbia dakika 90 zote bila kuchoka.

Kuna msitari mwembamba sana kati ya uhuni na Serie A.

Simon Inzaghi ni kocha mzuri lakini kwenye timu yenye structure nzuri huu ni msimu wake wa tatu Inter Milan kabla ya kufika fainali ya UEFA hakuna aliyekuwa akimuona Inzaghi kama kocha wa maana.
 
Manchester United toka aondoke Mzee Feg haijapata tena Mwl mzuri wa mpira..

Au ni uongozi hautaki mabadiliko..

Mechi ya jana kayi ya Liverpool na City imenifanya nione ukubwa wa tatizo la timu yetu..

Mpira unepigwa na viungo wawili wadogo tu hadi maestro KDB akafokeana na Mwl wake..

Utd walimlindia heshima bwana Erik kwa mtazamo wake wa kuichukulia poa EPL..

Na mwisho wa siku haiwezi tena..

Ni kweli majeruhi yamemkwamisha zaidi msimu huu..top 4 angeingia bila shida yeyote..

Ila ukweli uliowazi ile ligi kwake ni kubwa..
 
Pamoja na ubovu wa wachezaji wetu bado pia atahitajika Mwl mpya mwenye uwezo kumzidi Erik..

Erik ni mzuri ila sio wa kupambana na kina Pep..

Mechi zote ashinde, atoke sare na hata afungwe timu inateseka sana bila kujali nani mpinzani wake..

Bahati mbaya Manchester United huwa haitoi muda
 
Mourinho ameshinda ligi makombe mengi akiwa Madrid, Chelsea, Intermilan na Porto huyu siyo mwalimu mbaya.

Luis Van Gaal ameshinda makombe akiwa Ajax, Barcelona, Bayern Munichen, Az Alkmar huyu siyo mwalimu mbaya.

David Moyes na Ole hawakuwa level ya United ila Ole alikuwa anagrow vizuri na United walimharibia Project kina Woodawrd wenyewe msimu wake wa mwisho kwa kumsajilia wachezaji wazee.

Ralf hakuwa mwalimu mbaya na talent ID ilikuwa kubwa tu.

Ten Hag ameshashinda makombe na Ajax na ameshaperform vizuri kwenye UEFA siyo mwalimu mbaya tatizo lile lile lilimtesa Van gaal , Mourinho na OGS ni hilo hilo linalomtesa Ten Hag.
 
Erik akiaminiwa atatuvusha?

Ni kweli kabisa Shaw na Licha ndio sababu ya kufanya hata Fulham wakamate dimba na Pereira??

To me Sidhani..
Anthony
Mount
Amrabat hawa Erik hakwepi lawama kwa vyovyote vile..
Hii imempunguzia Credit kubwa sana..

Nakubali Manchester United kuna matatizo makubwa sana huko juu..
Rashford nae Superstar...

Pale Madrid hata Kylian hatakuwa Superstar..japo ndie atakuwa ncha kwenye Mkuki..

Pound 400+ alizotumia walau tungekuwa na wachezaji wanne au watano wa maana wa kuanzia..

Ofcourse kafanya jambo Ajax na niwe mkweli sikuwatazama sana nje ya mechi zao chache..miaka yake miwili basi angeonesha njia tujue tunapoenda..

Tulipo kwa sasa hakupishani na alipotukuta..
 
Erik Tan Hag hakuwa mwalimu mzuri sana kiulinzi tangu akiwa Ajax.

Lakini Squad yake ni mbovu sana kwa aina ya intensity ya ligi ilivyo kwa sasa.

Man United wamekuwa na fitness ndogo sana tangu msimu wa mwisho wa Ole na kwa sasa ni mwendelezo tu.
 
Hebu fafanua tena maelezo yako kwa ushahidi kaka, hii ni February gap la points ni 14 na unasema man u ilikua kwenye race
Msimamo wa ligi uliisha hivi, hii ilikua ni one horse race kaka si vyema kutumia kwenye reference zako
 
I second you bro
Sanasana ameamin kuwa hii sio ligi lele mama makocha miamba kama pep na huy wa Liverpool sio mchezo..tatizo ni yeye mwenyewe....

Waxhezani ka.ma amana unaitumiaje. Alitakiwa mlezi pia. Kukosana na Ronald. Pogba. Sancho..kumuuza Fred nakadhalika ni kukosa uwezo wa kupambana na malezi.

Baada ya kukosana na pogba na Ronaldo alipaswa kulea watoto wa academy..

Kama alivyompata mainoo na ganacho alipaswa kumpata left back. Centa back right back hawa stricker watoto alipaswa sometimes kuwachanganya. Sasa utakaaje unamtegemea Evans. Mbona kambambwa anapambana poa tu
 
Ni suala la muda,
ROMA haikujengwa kwa siku moja
1. Hojlund
2. Garnacho
3. Martinez
4. Maino
5. Dalot
6. Onana
7. Bruno
8. Shaw
9. Rashford
Hawa wakiwa fit, united tunamiliki ball na %kushinda inakuwa juu na hiyo list 80% yeye ndio kasajili.
Style of playing ni transition football, hii style kwa sasa inataka rashford, garnacho, bruno, maino na hojlund wawe fit ndio utaona impact
Kwa kweli ETH bado yuko asubuhi kweny hii project plus kaikopy baada ya kutua united.
Kuhusu usajili jamaa support haikuwa super sababu club ilikuw sokoni, tulikuw tuna ungaunga plus management mbovu.

MIMI NIKO NA ETH, msimu tunatoboa top 4.
Msimu ujao ndio wa kumuuliza maswala magumu, na yeye alipofika aliahidi msimu wa tatu ndio aulizwe.
Puuzia nyama ya jirani zetu, sasa sisi tule tembele, tukisubri hii process ya ETH km itakubali au vinginevyo.
sio mbali ni next season tu ndio utaamua hatma yake na ni mwisho wa mkataba pia.
 
Erik Tan Hag hakuwa mwalimu mzuri sana kiulinzi tangu akiwa Ajax.

Lakini Squad yake ni mbovu sana kwa aina ya intensity ya ligi ilivyo kwa sasa.

Man United wamekuwa na fitness ndogo sana tangu msimu wa mwisho wa Ole na kwa sasa ni mwendelezo tu.
Na hili ni pungufu lake katika falsafa yake ya kufundisha mpira..ameshindwa kuiheshimu EPL..

Pep ametamba kwa gharama kubwa sana na bado amepata free run mara 2 tu kati ya ndoo zake 5..mbili kazibeba mechi ya mwisho..

Moja pia ni kukosa ukomavu kwa Arsenal..

Zile mbili tulizomfatia alikuwa ligi ya peke yake..

Erik ameshindwa kuiheshimu EPL na mwisho ataondoka..

Manchester United sio kama hao
 
Baada ya kukosana na pogba na Ronaldo alipaswa kulea watoto wa academy.

Pogba ETH hakufanya naye kazi, ila Ishu ya CR7 unaona hata Ole Ilimuharibia kwa sababu kimaelezo anasema timu ilibidi icheze kumzunguka mana msimu mmoja kabla ya CR7 UTD ndo ilikuwa moja ya timu zilokuwa juu kwenye Pressing kuja kwa CR7 kila kitu kikabadilika.

Tizama kiwango cha makadirio ya Mishahara hapo halafu angalia Uwiano wa Umri Hamna Ujengwaji wa timu na Uongozi ni mbovu.
Sancho, Pogba, CR7, kwa asilimia kubwa zilikuwa zimekaa kibiashara zaidi, CITY katoka huko angalia sajili nyingi zinaenda fanya kazi na zinaendana na uchezaji wao. ALVAREZ ni aina za Sajili za Ferguson watu kama CHICHARITO na Kina RAFAEL.

HAMNA TIMU INAPIGA HATUA IKIWA NA UONGOZI USOELEWEKA , UTD Ni Mfano Mkuu.
 
Hivi nyumbu mna shida gani? Hamjui hata hesabu? Ten hug apo kwenye iyo list ya wachezaji 9 amesajili watatu tu, sasa iyo asilimia 80 umeitoa wapi?
Ten hug ni failure tu hapo unyumbuni hamna mahali atawafikisha, kocha ego kubwa uwezo mdogo
 
Tatizo ni mfumo Mkuu..hili kashindwa..au ni uongozi wa mpira haupo Manchester United..

Liverpool jana hawakuwa na
Allison
Trent
Robbo(alitokea benchi)
Salah (alitokea benchi)
Konate
Jota

Ila watoto waliupiga sana sana..
Ikifika sehemu KDB anagomba, Bernado anapaniki, Foden anangoja Rebound basi mambo yalikua moto..

Kwetu mfumo haupo..
Still tuna viungo wa ulinzi wengi ambao wangeficha kabisa ubovu wa safu ya ulinzi..

Matokeo yake Lindelof akimbizane mwanzo mwisho..
Mwl pamoja na ubovu wa uendeshwaji ila na yeye hatoshi tu..

Van gal bana pasi hata kama ni za kurudi nyuma zilipigwa na kina fellaini..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…