Manara asema ataishitaki Simba

Ataishitaki kwa minajili ipi? Yeye alikuwa Kibarua tu. Alipolialia akapewa option asainishwe 4m kwa mwezi ila asifanye mikataba kokote kule akaona ngoma ngumu akaendelea kupokea posho!

Sasa leo hii anapata wapi nguvu za kuishtaki Simba?
Naona anataka kuteka mitandaoni ili wamzingatie tu.
 
Simba timu tajiri isiyolipa wafanyakazi wake stahiki zao. Kama mtu anayejulikana na wengi, Manara hakuwahi kulipwa, vipi hao watendaji wa chini mfano wafanya usafi
Siku zote alivyokuwa anafanya kazi simba kwanini hakulalamika hana mkataba,kwanini asingeacha kazi sababu ya kukosa mkataba,na kama kuna watumishi wengine ambao wako simba ambao hawana mikataba kwanini mpaka leo hawasemi popote?
 
Anafmdanganya kuwa kaenda sijui kusalimu Kumbe amekimbiw

Ataishitaki kwa minajili ipi? Yeye alikuwa Kibarua tu. Alipolialia akapewa option asainishwe 4m kwa mwezi ila asifanye mikataba kokote kule akaona ngoma ngumu akaendelea kupokea posho!

Sasa leo hii anapata wapi nguvu za kuishtaki Simba?
Tatizo ni kwamba,Manara alidekezwa sana na timu ya Simba.Sasa anataka kuendelea kudeka hata wakati huu hayupo Simba S.C.Amevimbiwa deko huyo!
 
Mwanaume kusema "Nitatoa siri ya taasisi fulani au ya mtu fulani" ni aibu na pia ni fedheha kubwa kubwa sana,

Huyu jamaa yupo njiani kupotea na mdomo ndio utakaomponza,
Time will tell.
Kweli jamaa anashangaza sana yaani anapenda sifa mpaka anaboa
 
Mhindi akulipe uneemeke, wafanyakaz wake tu wa viwanda vyake choka mbaya, Maisha duni, wanamzalishia mivitenge, Kama wamevurugwa, tunao mitaani na tunaishi nao, sembuse mpiga Domo wa timu.
Wakina Dk Mengi, Tigo, Voda ni wahindi? Mbona wafanyakazi wao Bado wana maisha magumu mishahara kidogo? Rejea tena kwenye maandiko usome kuhusu ubepari siku zote bepari anaangalia masilahi yake binafsi anachotaka nikuona faida na yeye azidi kustawi ila siyo kumstawisha mfanyakazi, Tanzania nzima uwe unafanya kazi Kwa muhindi Kwa mchina Kwa nani maisha ni yaleyale, sizani kama dereva wa Kampuni ya GSM analipwa mshahara mkubwa na masilahi mengine zaidi ya Dereva wa Mo enterprises
 
Manara ana Tatizo kubwa la Kisaikolojia,ila naona anajificha kwenye kivuli cha usemaji wa yanga naamini kabisa kama asingekuwepo yanga mpaka sasa angekuwa kwenye msongo wa mawazo unao onekana kabisa.
Huyu hata yanga inapaswa wawe nae makini sana
 
Huyu hata yanga inapaswa wawe nae makini sana
Nadhani Yanga pia kuna Viongozi wenye akili ambao wanajua Manara ni mtu wa aina gani,naamini kabisa Manara kuendelea kuwepo yanga sio kwamba viongozi wa yanga na mashabiki wanampenda ni kwaajili tu ya usimba na Uyanga wa nchi hii na sio weledi wake ,na naamini kuna vitu wanavitaka kutoka kwake (kumtumia), Manara kuendelea kubaki Yanga itategemea yanga inafanya vizuri kiasi gani kwenye msimu wa mwaka huu,kama ikifanya vibaya siku sio nyingi watamtema.
Time will tell.
 
Kwahiyo ipo siku haya maneno atawaambia Yanga siku akiondoka?
Eti Kaifanya Simba ipate mashabiki hahahaha....
Amekosa kiki sasa a atafuta pakuongelea. Simba hawana muda na maneno yake. Huyu mtu ni mpuuzi. Kwahiyo anaitishia Simba?
 
Kwahiyo ipo siku haya maneno atawaambia Yanga siku akiondoka?
Eti Kaifanya Simba ipate mashabiki hahahaha....
Amekosa kiki sasa a atafuta pakuongelea. Simba hawana muda na maneno yake. Huyu mtu ni mpuuzi. Kwahiyo anaitishia Simba?
Yaani yeye kila sehemu anaisema simba vibaya.
Yaani kipindi hicho kilikuwa cha mapenzi badala azungumzie kwa nini mke kamukimbia yeye anazungumzia mambo ya simba
 
Ila tuacheni utani na tuseme ukweli bila unafiki wowote tukitoa ule Usimba na Uyanga je kuna shabiki au Mwanachama yeyote wa Yanga anamuamini Manara?
Labda lakini huku niliko hata mashabiki wa Yanga hawaamini katika Manara
 
Yaani yeye kila sehemu anaisema simba vibaya.
Yaani kipindi hicho kilikuwa cha mapenzi badala azungumzie kwa nini mke kamukimbia yeye anazungumzia mambo ya simba
Ohoooooo kumbe mke wake amemkimbia?
Dah mbona mpya hii. Vijana mna siri sana aisee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom