crankshaft
JF-Expert Member
- Jun 12, 2019
- 1,410
- 3,376
Dar es Salaam. Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imesema haiutambui usajili wa Chuo cha Tanzania Aviation College kilicho na matawi katika mikoa ya Mwanza, Dares Salaam na Arusha.
Chuo hicho ambacho kimekuwa kikitumia usajili namba wa CAA/AT0/050 imebainishwa kuwa usajili wake ulifikia ukomo mwaka 2018.
Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Hamza Johari inaeleza kuwa kukoma kwa usajili huo kunafanya mafunzo ya usafiri wa anga yanayoendeshwa na chuo hicho kwa kutumia mgongo wa kutambulika na TCAA kuwa ni kinyume na sheria.
“Pia hii inafanya wahitimu wa chuo hiki kukosa sifa za kupata leseni kutoka TCAA hivyo kushindwa kupata ajira,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Kufuatia hilo, imeelezwa kuwa kinachofanyika sasa ni kinyume na taratibu za usajili kama ilivyoainishwa katika Sheria ya Usafiri wa Anga, Sura ya 80 na Kanuni zake, The Civil Aviation (Approved Training Organisation) Regulations, 2017.
“TCAA inatoa wito kwa wazazi na wanafunzi wanaotaka kusoma kozi za Usafiri wa Anga kujiridhisha kwa Mamlaka ya Usafiri wa Anga ili kupata uhakika kuhusu uhalali wa vyuo vinavyotambulika, pia orodha yake inapatikana katika tovuti ya Mamlaka,” imeelezwa.
Mwananchi
Chuo hicho ambacho kimekuwa kikitumia usajili namba wa CAA/AT0/050 imebainishwa kuwa usajili wake ulifikia ukomo mwaka 2018.
Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Hamza Johari inaeleza kuwa kukoma kwa usajili huo kunafanya mafunzo ya usafiri wa anga yanayoendeshwa na chuo hicho kwa kutumia mgongo wa kutambulika na TCAA kuwa ni kinyume na sheria.
“Pia hii inafanya wahitimu wa chuo hiki kukosa sifa za kupata leseni kutoka TCAA hivyo kushindwa kupata ajira,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Kufuatia hilo, imeelezwa kuwa kinachofanyika sasa ni kinyume na taratibu za usajili kama ilivyoainishwa katika Sheria ya Usafiri wa Anga, Sura ya 80 na Kanuni zake, The Civil Aviation (Approved Training Organisation) Regulations, 2017.
“TCAA inatoa wito kwa wazazi na wanafunzi wanaotaka kusoma kozi za Usafiri wa Anga kujiridhisha kwa Mamlaka ya Usafiri wa Anga ili kupata uhakika kuhusu uhalali wa vyuo vinavyotambulika, pia orodha yake inapatikana katika tovuti ya Mamlaka,” imeelezwa.
Mwananchi