'Mambo ya Kinana' yaipaisha Tanzania!

'Mambo ya Kinana' yaipaisha Tanzania!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Tanzania imetajwa kama moja ya nchi zinazoongoza kwa ujangili na hasa biashara ya pembe za ndovu duniani. Sasa inatajwa kama nchi mojawapo hatari kabisa kwa wanyama wa porini duniani.Nchi nyingine ni Kenya na Uganda.Ikumbukwe kuwa Katibu Mkuu wa CCM,Abdurahman Kinana alishutumiwa waziwazi na Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii,Mchungaji Peter Msigwa, kuwa ni kinara wa biashara ya pembe za ndovu. Nchi zilizotajwa kuongoza katika ununuzi wa pembe za ndovu ni China,Thailand,Vietnam,Malaysia na Ufilipino. Nini kifanyike waungwana ili kuwalinda wanyama wetu hasa tembo? Habari kamili ni kwenye Mwananchi la leo uk wa 1 na 4. Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam.
 
Last edited by a moderator:
Tanzania imetajwa kama moja ya nchi zinazoongoza kwa ujangili na hasa biashara ya pembe za ndovu duniani. Sasa inatajwa kama nchi mojawapo hatari kabisa kwa wanyama wa porini duniani.Nchi nyingine ni Kenya na Uganda.Ikumbukwe kuwa Katibu Mkuu wa CCM,Abdurahman Kinana alishutumiwa waziwazi na Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii,Mchungaji Peter Msigwa, kuwa ni kinara wa biashara ya pembe za ndovu. Nchi zilizotajwa kuongoza katika ununuzi wa pembe za ndovu ni China,Thailand,Vietnam,Malaysia na Ufilipino. Nini kifanyike waungwana ili kuwalinda wanyama wetu hasa tembo? Habari kamili ni kwenye Mwananchi la leo uk wa 1 na 4. Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam.

huna unachokijua wala huelewi kitu tukupe pole kwa vile hujui kinachoendelea hapa tanzania.
 
Nchi hizo ambazo zinatambuliwa kama kundi la wanane ‘gang of eight’ ni pamoja na Tanzania, Kenya na Uganda, ambazo zimewekwa katika kundi la nchi zinazozalisha pembe hizo. Nchi zilizowekwa katika kundi la wanunuzi ni China na Thailand, Malaysia, Vietnam na Ufilipino. ( Na Kinana alikuwa China juzi juzi, tujiulize? )

Nimesoma gazeti la Mwananchi ya leo tarehe19/05/13 na kujua kuwa kumbe Tanganyika ni ya nane duniani katika ujangili wa Meno ya Tembo sasa najiuliza huyu weka mbali na tembo anasema yeye hausiki, sawa lakini mbona meli yake iliyokamatwa na meno ya tembo haijataifishwa. Yaani katika Tanganyika matatizo madogo yanatumiwa nguvu kubwa kuliko yale makubwa. Kwa mfano kuua au kutumia mabomu na maji ya kuwasha kwa kutawanya watu kwenye maandamano/machinga pasipo kutumia lugha nzuri inaliingiza nchi hii katika matatizo mengi na gharama kubwa.

Kwani mabomu ya machozi, maji ya kuwasha hazigaiwi bure zinanunuliwa leo hii tukipiga mahesabu tangu uchaguzi wa 2010 uishe ili tujue tumetumia kiasi gani kwa manunuzi ya mabomu na maji ya kuwasha, ni pesa nyingi sana. Halafu wale mapapa ambao wangekamatwa na kuchukuliwa mali zao walizoiibia serikali wanaachiwa na kesi zao kupigwa kalenda ili wananchi wasahau. Tukirudi nyuma hivi kweli katika kashfa zote ambazo serikali hii imepata kutokana na Chenge (Vijisenti). Ingekuwa nchi nyingine Chenge angekuwa bungeni na kupewa tena kamati ili aongoze. Hii inawezekana Tanganyika tu
 
Tanzania imetajwa kama moja ya nchi zinazoongoza kwa ujangili na hasa biashara ya pembe za ndovu duniani. Sasa inatajwa kama nchi mojawapo hatari kabisa kwa wanyama wa porini duniani.Nchi nyingine ni Kenya na Uganda.Ikumbukwe kuwa Katibu Mkuu wa CCM,Abdurahman Kinana alishutumiwa waziwazi na Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii,Mchungaji Peter Msigwa, kuwa ni kinara wa biashara ya pembe za ndovu. Nchi zilizotajwa kuongoza katika ununuzi wa pembe za ndovu ni China,Thailand,Vietnam,Malaysia na Ufilipino. Nini kifanyike waungwana ili kuwalinda wanyama wetu hasa tembo? Habari kamili ni kwenye Mwananchi la leo uk wa 1 na 4. Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam.
Mkuu hongera sana, umeingiza posho yako vizuri kabisa, leo unapata mara saba zaidi ya siku zote
 
Kinana si mtu wa kupuuzwa, ni strategist na mchapakazi wa kweli, lazima mhangaike kumchafua kwa salama yenu.
 
Nakumbuka makala za kibanda kabla hajafukuzwa tanzania daima ndipo aje ateswe, alishasema mengi kuhusu utendaji wa kinana...kwamba kuteuliwa kwake ukatibu mkuu ccm ni msiba kwa upinzani....mada kma hii ni mbinu za kumdhoofisha na kumchafua mbele za jamii
 
huna unachokijua wala huelewi kitu tukupe pole kwa vile hujui kinachoendelea hapa tanzania.

Kwamba hajui Ndovu wetu wanakwisha kwa sababu ya Kinana kutajwa kwamba ndiyo Master Planer wa dili za Pembe za ndovu? kwamba Meli zake ni moja ya vyombo vinavyo safirisha Pembe za Ndovu wetu?

Kwamba Pembe za Ndovu wetu walio uawa zimekamatwa Hong Kong na kwingineko kutoka kwenye meli za Kinana?

ACHANA NA AKILI ZAKUSHIKIWA.
 
Ndio maana ccm na China ni ndoa ya maisha. Mikataba 19 kimya kimya unafanya mchezo.
 
jangili kinana atatumaliza jamani uwiii tembo wetu hawa wanaisha ivi ivi wajameni
 
only in tanzania...Mtu anafanya ujangili badala ya kuomba watanzania maskini msamaa anataka aombe yeye radhi...
 
nchi hizo ambazo zinatambuliwa kama kundi la wanane ‘gang of eight’ ni pamoja na tanzania, kenya na uganda, ambazo zimewekwa katika kundi la nchi zinazozalisha pembe hizo. Nchi zilizowekwa katika kundi la wanunuzi ni china na thailand, malaysia, vietnam na ufilipino. ( na kinana alikuwa china juzi juzi, tujiulize? )

nimesoma gazeti la mwananchi ya leo tarehe19/05/13 na kujua kuwa kumbe tanganyika ni ya nane duniani katika ujangili wa meno ya tembo sasa najiuliza huyu weka mbali na tembo anasema yeye hausiki, sawa lakini mbona meli yake iliyokamatwa na meno ya tembo haijataifishwa. Yaani katika tanganyika matatizo madogo yanatumiwa nguvu kubwa kuliko yale makubwa. Kwa mfano kuua au kutumia mabomu na maji ya kuwasha kwa kutawanya watu kwenye maandamano/machinga pasipo kutumia lugha nzuri inaliingiza nchi hii katika matatizo mengi na gharama kubwa.

Kwani mabomu ya machozi, maji ya kuwasha hazigaiwi bure zinanunuliwa leo hii tukipiga mahesabu tangu uchaguzi wa 2010 uishe ili tujue tumetumia kiasi gani kwa manunuzi ya mabomu na maji ya kuwasha, ni pesa nyingi sana. Halafu wale mapapa ambao wangekamatwa na kuchukuliwa mali zao walizoiibia serikali wanaachiwa na kesi zao kupigwa kalenda ili wananchi wasahau. Tukirudi nyuma hivi kweli katika kashfa zote ambazo serikali hii imepata kutokana na chenge (vijisenti). ingekuwa nchi nyingine chenge angekuwa bungeni na kupewa tena kamati ili aongoze. Hii inawezekana tanganyika tu

kinana ni fisadi papa,ata kama report iliyotoka imemsafisha hiyo haiondoi maana kuwa amekuwa akishiriki vitendo vya kulihujuma taifa hili kwa muda mrefu sasa,amekua akitumia muavuli wa chama kama sehemu yake ya kujifichia,hii inajidhihirisha wazi kwa kuwa ccm imekuwa ni pango la walanguzi na genge lisilovumilika la wahalifu
 
Mkuu hongera sana, umeingiza posho yako vizuri kabisa, leo unapata mara saba zaidi ya siku zote

Mijitu mingine bwana hata iwekewe nini yenyewe ishazoea kudanganywa tu.Sasa unaambiwa tumeshika nafasi ya kwanza kwa ujangili huelewi nini hapo,shenzi type.Hivi unafikiri kwa kuwa una hicho kinafasi ulichopewa ndo ndugu zako hata bibi zako wa kijijini wananeemeka ama ni wewe peke yako.Acha akili za matope na kama huna cha kuandika tulia zako.

Sisi tumekuwa kwenye mapori anzia mapori ya Biharamulo, Burigi, Ugala, Katavi,Myovosi,Selous,Fort Ikoma na kila pori unalolijua wewe tumefika na tunajua kinachoendelea.Wewe kaa hapo na siasa utakula siasa zako na hizo hela za kuhongwa.Huenda unaongea hata hujawahi hata kuona tembo kwa macho yako kwa kuwa akili zako ni za kushikiwa na kuongozwa mapaka ujifie
 
Nakumbuka makala za kibanda kabla hajafukuzwa tanzania daima ndipo aje ateswe, alishasema mengi kuhusu utendaji wa kinana...kwamba kuteuliwa kwake ukatibu mkuu ccm ni msiba kwa upinzani....mada kma hii ni mbinu za kumdhoofisha na kumchafua mbele za jamii
Hivi akiwa msiba kwa upinzani hawezi pia kuwa msiba kwa vitu vingine?
 
ILi mradi Kinana bado ni Katibu Mkuu wa CCM basi tuhesabie maumivu sasa nadhani Tembo ndio watazidi kuuliwa manake tangu apewe hivho cheo kasi imeongezeka kama mbio za marathon naona ashitakiwe kwenye mahakama za kimataifa manake hapa majaji wenyewe wanahukumu kesi kwa kubalance sio kwa haki
 
Back
Top Bottom