'Mambo ya Kinana' yaipaisha Tanzania!

'Mambo ya Kinana' yaipaisha Tanzania!

du yaani hii ndo sifa tumepata ha ha ha ha ha ha ha
 
Tukiacha utani wa kisiasa, hakiki tembo wanapotea kwa kasi sana, je tuamini wahusiku wakuu hawako kwenye mfumo wa tabaka tawala?
 
945288_201878133294636_36115892_n.jpg

hayo ndo mambo ya hawa watu hatari kwa tembo

Tanzania imetajwa kama moja ya nchi zinazoongoza kwa ujangili na hasa biashara ya pembe za ndovu duniani. Sasa inatajwa kama nchi mojawapo hatari kabisa kwa wanyama wa porini duniani.Nchi nyingine ni Kenya na Uganda.Ikumbukwe kuwa Katibu Mkuu wa CCM,Abdurahman Kinana alishutumiwa waziwazi na Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii,Mchungaji Peter Msigwa, kuwa ni kinara wa biashara ya pembe za ndovu. Nchi zilizotajwa kuongoza katika ununuzi wa pembe za ndovu ni China,Thailand,Vietnam,Malaysia na Ufilipino. Nini kifanyike waungwana ili kuwalinda wanyama wetu hasa tembo? Habari kamili ni kwenye Mwananchi la leo uk wa 1 na 4. Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam.
 
Wajukuu zetu watawaona tembo kwenye picha tu. Kwa wale wenye uwezo watawaona kwenye Zoo za nchi za nje.
 
Kama mlikuwa hamjui kuhusu uteuzi wake wa ukatibu mkuu wa chama ulitokana na sifa ya kuitangaza Tanzania ughaibuni. Mwisho utasikia kikao cha CC kimempandisha cheo kuwa mgombea urais 2015 kwa kuwa anao mtaji wa kutosha.
 
Kinana si mtu wa kupuuzwa, ni strategist na mchapakazi wa kweli, lazima mhangaike kumchafua kwa salama yenu.
Tuulize watu wa Arusha kwa nini hatathubutu kugombea hata ubalozi wa nyumba kumi kumi kwa chama chake CCM.
 
aisee zile tani zetu 101 za meno ya tembo kwenye ghala la taifa hatujapata tu kibali cha kuziuza Asia? je kinana anaweza kutusaidia kuzitafutia soko ili hela zitakazopatikana tununulie madawa na madawati kwa ajiri ya watoto wetu? maana tumekaa na mamilion ya mi-dolla
 
huyu msomali sasahivi anatapatapa maana mwanzo alisema hatishwi na shutuma hizi na hatakatishwa tamaa katika halakati zake za kisiasa sasa kama ndivyo vipi leo atishie kwenda mahakamani nawakati anajua hatakwenda? ushali wangu kwake nibola achane na siasa aendelee na biashala yake maana hawezi kuacha hiyo biashala na hasa ukizingatia kuwa ndiyo iliyomtoa toka enzi za mzee wa ruksa.
 
Ningependa ndugu Kinana ajibu yafuatayo!

  • Bill of Lading (BL), pamoja na mambo mengine pia ni risiti ya mzigo uliokubaliwa kusafirishwa na kupelekwa mahali unapo takikana!
  • pia ni document inayoeleza aina ya mzigo, jinsi ulivyopakiwa, idadi yake, thamani yake na gharama za kuusafirisha!


Mwenye meli au wakala wake kabla ya kutoa bill of lading kwa exporter/importer lazima waukague na wauone mzigo ili mwishowe watoe gharama za kuusafirisha!

  • Kinana, kampuni na meli yake, waliwezaje ku'issue bill of lading kwa kontena lenye pembe za ndovu bila ya kuuona mzigo?
  • Kwakuwa bei ya kusafirisha 40'ft container kutoka point A hadi B hazilingani, hali kadhalika kwa container ya 20'ft...kutoka point A to B kutokana na utofauti wa mizigo na thamani zake.....SWALI, Kinana, kampuni na meli yake, walipata wapi bei ya kusafirisha hilo container bila ya kujua thamani ya wanacho kisafirisha?
  • Endapo container lililo safirisha pembe za ndovu kupitia meli ya kinana, badala ya kukutwa pembe wangekutwa wasomali....nani angewajibishwa...mwenye meli, wakala au clearing and forwarding agents?
 
Faru wa Mheshimiwa Rais wapo mkuu.

Washaua tayari faru wa JK.
WEWE WA WAPI.
haikuchukua hata roundi wakaua faru wa kwanza kama sikosei anaitwa GEORGE.
WEK MBALI NA FARU ashafanya mambo yake kitambo.
 
1.Kinana weka mbali na tembo
2.kinana weka mbali na faru
3.kinana weka mbali na twiga
4.kinana weka mbali na sokwe
5.kinana weka mbali na swala
 
Kwamba hajui Ndovu wetu wanakwisha kwa sababu ya Kinana kutajwa kwamba ndiyo Master Planer wa dili za Pembe za ndovu? kwamba Meli zake ni moja ya vyombo vinavyo safirisha Pembe za Ndovu wetu?

Kwamba Pembe za Ndovu wetu walio uawa zimekamatwa Hong Kong na kwingineko kutoka kwenye meli za Kinana?

ACHANA NA AKILI ZAKUSHIKIWA.
Huhitaji kuwa "rocket scientist" kujua kwamba CCM wana lengo la kuifilisi nchi hii.Tembo 57 hufa kila siku Tanganyika ili kukipatia fedha za kutosha chama cha mapinduzi kuhakikisha wanahonga watu na kuiba kura ili kibaki madarakani.Wameuza kwa bei ya kutupa migodi yote ya almasi na dhahabu,Juzi wamesaini kwa siri mikataba 19 na china ili wajibebee mafuta,gesi na uranium ya mtwara na lindi.Ni lazima uwe mwendawazimu tuu kukiunga mkono chama cha mapinduzi
 
huna unachokijua wala huelewi kitu tukupe pole kwa vile hujui kinachoendelea hapa tanzania.

Mkuu, tuambie maana hatujui kinachoendelea. Sote ni watanzania. Ukituacha tutaendelea kuamini kilichoandikwa
 
By Izz<br />
Faru wa Mheshimiwa Rais wapo mkuu.
<br />
<br />
Washaua tayari faru wa JK.<br />
WEWE WA WAPI.<br />
haikuchukua hata roundi wakaua faru wa kwanza kama sikosei anaitwa GEORGE.<br />
WEK MBALI NA FARU ashafanya mambo yake kitambo.
Huyo George alikua anaishi Creator na aliwahi kutoroka na wakamkamatia Serengeti.....wengine wapo mkuu, labda huyo ndio atakua kapoteza maisha.....ngoja nikachimbue chimbue tena then nitakuja na jibu mujarabu!
 
Back
Top Bottom