Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

n00b

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2008
Posts
1,013
Reaction score
2,684
Wakuu,

Nipo maeneo ambayo huenda nikawapasha kidogo juu ya nini kinaendelea hapa, naweza kuwa natoweka online lakini nitawapa dondoo za kinachoendelea.

Wakuu hapa wanajadili nini kifanyike dhidi ya wanaokipaka matope chama, hapa namaanisha watuhumiwa wa ufisadi pamoja na mzee Makamba.

15sa80h.jpg


==============

UPDATES:

Wajumbe wapya wa NEC wa kuteuliwa na Mwenyekiti ni Nchimbi, Januari Makamba, Anna Abdallah, Ali Juma Shamhuna, Peter Kisumo, Wilson Mukama na Lameck Mwigulu.

Katibu Mkuu mpya wa CCM atakuwa ni Wilson Mukama, Naibu wake atakuwa ni John Chiligati, Fedha atakuwa ni Mwigulu, Nape atakuwa Uenezi, Mambo ya nje ni Januari Makamba.

Hussein Mwinyi, Mbarawa, Omar Yusuf, Seif Khatib, Samia, Maua Daftari, Meghji, Kinana, Lukuvi na Mwenyekiti wa Kagera wa CCM (Mama Buhie), Kigoda, Wassira na Pindi Chana - CC

ZAIDI:
- Wakulu tupo pamoja sana, hali sio shwari Dodoma the dataz ni makundi ndani ya CCM yakirushiana mawe, lakini kundi lenye nguvu ya kushika Urais 2015 ndilo linaloelekea kushinda.

- Mafisadi time is up, wameshikwa pabaya sasa maana hawana pa kupitia tena Six holds the big key to the changes which are coming ndani ya CCM kutoka hiki kikao!

......Stay Tuned.....!


FMes! - Wazee Wa Sauti Ya Umeme!

Wajumbe Wa Halmashauri Kuu Ya CCM Taifa wakipiga Kura Kuchagua Wajumbe Wa Kamati Kuu Ya CCM Mjini Dodoma


GO9G5601.JPG

Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipiga kura wakati wa kuchagua wajumbe wapya wa Kamati kuu ya CCM mjini Dodoma leo jioni.Kushoto ni makamu wa CCM bara Pius Msekwa na watatu kulia ni aliyekuwa katibu mkuu wa CCM Yusuf Makamba.
2.JPG

Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete,aliyekuwa katibu mkuu wa CCM Yusuf Rajab Makamba na Rais wa Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein wakipiga kura kuchagua wajumbe wapya wa Kamati kuu ya CCM wakati wa mkutano wa Halmashauri kuu ya CCM uliofanyika mjini Dodoma leo jioni.
5.JPG

Mzee Kingunge akipiga kura yake katika uchaguzi huo
1.JPG

Baadhi ya wajumbe wa Halmshauri kuu ya CCM wakipiga kura kuchagua wajumbe wa Kamati kuu ya CCM mjini Dodoma leo jioni
4.JPG

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM, Martine Shigella akipiga kura yake.Picha na Freddy Maro-IKULU​
 
mkuua asante kwa taarifa na ufatilia. endelea kutujuza yanayoendelea
 
Consultant aliyepewa kazi ya kufuatilia sababu ya JK kupata ushindi mwembamba kawasilisha ripoti nayo imetoa pendekezo la watuhumiwa wa ufisadi kutoswa kwani ndo njia pekee ya kurejesha imani kwa wananchi
 
JK anaonekana kuwa na hasira tokana na kinachoendelea ndani ya chama, Rostam kaomba radhi kuwa endapo kuna sehemu kakosea basi wamsamehe
 
Consultant aliyepewa kazi ya kufuatilia sababu ya JK kupata ushindi mwembamba kawasilisha ripoti nayo imetoa pendekezo la watuhumiwa wa ufisadi kutoswa kwani ndo njia pekee ya kurejesha imani kwa wananchi
Itakuwa too little, too late, hata hivyo.
 
Consultant aliyepewa kazi ya kufuatilia sababu ya JK kupata ushindi mwembamba kawasilisha ripoti nayo imetoa pendekezo la watuhumiwa wa ufisadi kutoswa kwani ndo njia pekee ya kurejesha imani kwa wananchi

Kwa nyekundu ,ni nani huyo.
Kama upo ndani,kwamba LOWASA.ROSTAM.KARAMAGI,MSABAHA,CHENGE watoswe CCM? Dhubutu!!.Hiyo ni sawa na ngamia kupita kwenye tundu la Sindano.
 
Kwa utetezi wa Rostam na wenzake ni kuwa mbona majimboni mwao walishinda kwa ushindi wa Tsunami na JK alipata ushindi mzito sana? Anadai si sahihi wao kudaiwa kuwa chanzo cha kupungua kura za JK uchaguzi uliopita
 
Consultant aliyepewa kazi ya kufuatilia sababu ya JK kupata ushindi mwembamba kawasilisha ripoti nayo imetoa pendekezo la watuhumiwa wa ufisadi kutoswa kwani ndo njia pekee ya kurejesha imani kwa wananchi

Hili hawaja Copy and Paste kweli kutoka CDM kutumia ma-consultants kwenye mambo ya kitaalam kuliko kutumia mawazo ya miaka ya 47????????
 
Ni CC ambayo ilianza jana ikaendelea leo na mchana wamepumzika sasa, hadi saa moja usiku watakapoendelea.

Kifupi hayo ndo niloona niwafahamishe. Usiku nitajitahidi kuwafahamisha kitakachoendelea
 
JK anaonekana kuwa na hasira tokana na kinachoendelea ndani ya chama, Rostam kaomba radhi kuwa endapo kuna sehemu kakosea basi wamsamehe
Heee asamehewe? kweli RA pamoja na utajiri wake wote lakini hana akili kabisa....yaani baada ya kusema jamani imetosha na sasa najitoa rasmi kwenye siasa,na badala yake anaomba misamaha ili aendelee kuliibia Taifa? yaani mikashifa yote hiyo anayoipata kutoka kwa wananchi bado hatosheki tu? sheenz type ccm
 
NEC nayo leo imeahirishwa hadi kesho na JK anayo ajenda nzito mwenyewe japo Msekwa ndiye anao utangulizi.

Maelezo ya kwanza yalihusiana na CC naomba nisiwachanganye kwa title ya thread
 
Wakuu,

Nipo maeneo ambayo huenda nikawapasha kidogo juu ya nini kinaendelea hapa, naweza kuwa natoweka online lakini nitawapa dondoo za kinachoendelea.

Wakuu hapa wanajadili nini kifanyike dhidi ya wanaokipaka matope chama, hapa namaanisha watuhumiwa wa ufisadi pamoja na mzee Makamba

Baba endelea wengi tunahitaji kujua yaliyomo huko. Well done!
 
Hawana ubavu wa kumtosa R.A. Kwa sababu ndio mfadhili wao, their days are numbered.
 
Back
Top Bottom