MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
1. Hawajisifu balip humsifia sana Kristo na Baba Muumba ( Mungu )
2. Wanahubiri Kiustaarabu na hawapigi Kelele kama Walevi wa Gongo wa Kunduchi Mtongani au wa Kawe kwa Mapupu
3. Wanaenda mno na muda na Wanathamini sana Ratiba za Watu nje ya Ibada
4. Hawatuhimizi kila mara kutoa Sadaka bali kwa Mahubiri yao mazuri Wewe Mwenyewe tu utashawishika kutoa Sadaka
5. Hawatulazimishi tununue Maji au tubebe Mikojo na Vinyesi vyetu vikaombewe ili vitolewe Mapepo
6. Shuhuda za Kipuuzi Kipuuzi na za Kitoto kama za kukutana na Mende au Panya Jikoni Kwako hawazitaki
7. Japo Wanahubiri ila pia Wanaheshimu sana Tafiti za Kisayansi kuhusu Afya ya Mwanadamu tofauti na Wetu wanaodharau Tiba za Kisayansi ( Hospitalini ) wakisema Kristo na Damu yake inatosha Kukutibia hata kama Unaugua hoi na Safari ya kwenda Kulala rasmi Frijini Mochwari unaiona
Ni Matumaini yangu makubwa yale Madhehebu mengine hapa nchini Tanzania ( ukiyaondoa tu ya Catholic, Lutheran, Anglican na SDA ambayo ndiyo yana Ustaarabu,Umakini na Waumini wenye Akili Kubwa na Timamu pia ) nayo yatakuwa yamejifunza Kitu kutoka kwa hawa Wahubiri wa IMANI, UPENDO na MIUJIZA hivyo kuanzia Jumapili hii ( ya Keshokutwa ) katika Ibada zao tutaona Mabadiliko.
2. Wanahubiri Kiustaarabu na hawapigi Kelele kama Walevi wa Gongo wa Kunduchi Mtongani au wa Kawe kwa Mapupu
3. Wanaenda mno na muda na Wanathamini sana Ratiba za Watu nje ya Ibada
4. Hawatuhimizi kila mara kutoa Sadaka bali kwa Mahubiri yao mazuri Wewe Mwenyewe tu utashawishika kutoa Sadaka
5. Hawatulazimishi tununue Maji au tubebe Mikojo na Vinyesi vyetu vikaombewe ili vitolewe Mapepo
6. Shuhuda za Kipuuzi Kipuuzi na za Kitoto kama za kukutana na Mende au Panya Jikoni Kwako hawazitaki
7. Japo Wanahubiri ila pia Wanaheshimu sana Tafiti za Kisayansi kuhusu Afya ya Mwanadamu tofauti na Wetu wanaodharau Tiba za Kisayansi ( Hospitalini ) wakisema Kristo na Damu yake inatosha Kukutibia hata kama Unaugua hoi na Safari ya kwenda Kulala rasmi Frijini Mochwari unaiona
Ni Matumaini yangu makubwa yale Madhehebu mengine hapa nchini Tanzania ( ukiyaondoa tu ya Catholic, Lutheran, Anglican na SDA ambayo ndiyo yana Ustaarabu,Umakini na Waumini wenye Akili Kubwa na Timamu pia ) nayo yatakuwa yamejifunza Kitu kutoka kwa hawa Wahubiri wa IMANI, UPENDO na MIUJIZA hivyo kuanzia Jumapili hii ( ya Keshokutwa ) katika Ibada zao tutaona Mabadiliko.