Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,340
- 51,901
Kwema Wakuu!
Nashukuru Kwa sababu mpaka sasa Nina mialiko mitatu ya Idi, nawashukuru wote mlionialika. Nirejee kwenye mada.
Kama kichwa kinavyojieleza hapo juu, Hii ni orodha ya mambo tuliokatazwa na kusisitizwa na Wazee wetu linapokuja suala la mahusiano ya ndoa, sasa Vijana wanapiga mayowe.
1. OA BIKRA
Hii ilikuwa moja ya hoja kuu Kwa kijana anayeenda kuoa. Mimi kama Taikon ninawaelewa wazee na nina sababu ya kufanya hivyo. Ingawaje inaweza kuwa ni Mtazamo wa kizamani lakini Kwa wanaouzingatia wengi wao wanapata matokeo chanya.
2. OA Kabila lako au mnaolingana Mila na desturi. Achana na hawa Watoto wasiojua maana ya kabila, sijui Mila na desturi, hawa waliozaliwa mjini. Hao hawawezi kuwa kitu kinachoitwa ukabila.
Mahusiano hayajawahi kuwasumbua Watu wanaofuata mambo ya Mila na desturi za makabila Yao. Mapenzi yanayosumbua Wenye kuiga Mila za kigeni, wasomi na wadandia Mambo kama dini za kigeni.
3. Mwanaume ni kichwa cha Nyumba.
Kichwa kina ubongo, macho, masikio, mdomo. Mwanaume lazima uwe mwanaume, ukisema umesema, ukisimamia Jambo umesimamia, mchakarikaji, unayejituma kwaajili ya familia na jamii yako.
Hakuna usawa baina ya Mwanamke na Mwanaume. Mwanaume hapswi kufuata matakwa ya MKE au Mwanamke. Wote wanaofuata Kanuni hiyo mahusiano hayawezi kuwasumbua. Hata hivyo mwanaume kama kichwa cha Nyumba hapaswi kuwa muonevu na kutowatendea Haki Watu wa nyumba yake.
4. Mwanaume Halii
Mwanaume kujilizaliza, kutia Tia huruma, sijui. Kupiga magoti au kuwa chawa na mpambe mpambe kijingajinga Huko ni kujiingiza kwenye ushoga. Hakuna Mwanamke anayempenda mwanaume lainilaini, mliaji liaji, dekaji dekaji, hakuna.
Mahusiano lazima yakusumbue tuu!
Umetongoza Mwanamke kakukatalia Achana naye, usibembeleze na kujiliza Liza kama lipuuzi, usije ukadhani kujiliza ndio kutaugeuza moyo WA Mwanamke, zaidi Sana atakudharau.
Umepata matatizo kidogo unalia, sasa unalia nini kama mtoto, sasa Baba mzima unalia Mkeo na watoto wafanye nini. Mwanaume lazima uwe ngangari.
Hawa Wanawake wapo hivi walivyo Kwa sababu siku hizi wanaume wengi wamekuwa kama Wanawake.
Wanawake wanapenda Wanaume washoka, wahuni, wenye Roho ngumu, wasioogopa, wenye Akili, wenye maamuzi.
Nipumzike Sasa.
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam
Nashukuru Kwa sababu mpaka sasa Nina mialiko mitatu ya Idi, nawashukuru wote mlionialika. Nirejee kwenye mada.
Kama kichwa kinavyojieleza hapo juu, Hii ni orodha ya mambo tuliokatazwa na kusisitizwa na Wazee wetu linapokuja suala la mahusiano ya ndoa, sasa Vijana wanapiga mayowe.
1. OA BIKRA
Hii ilikuwa moja ya hoja kuu Kwa kijana anayeenda kuoa. Mimi kama Taikon ninawaelewa wazee na nina sababu ya kufanya hivyo. Ingawaje inaweza kuwa ni Mtazamo wa kizamani lakini Kwa wanaouzingatia wengi wao wanapata matokeo chanya.
2. OA Kabila lako au mnaolingana Mila na desturi. Achana na hawa Watoto wasiojua maana ya kabila, sijui Mila na desturi, hawa waliozaliwa mjini. Hao hawawezi kuwa kitu kinachoitwa ukabila.
Mahusiano hayajawahi kuwasumbua Watu wanaofuata mambo ya Mila na desturi za makabila Yao. Mapenzi yanayosumbua Wenye kuiga Mila za kigeni, wasomi na wadandia Mambo kama dini za kigeni.
3. Mwanaume ni kichwa cha Nyumba.
Kichwa kina ubongo, macho, masikio, mdomo. Mwanaume lazima uwe mwanaume, ukisema umesema, ukisimamia Jambo umesimamia, mchakarikaji, unayejituma kwaajili ya familia na jamii yako.
Hakuna usawa baina ya Mwanamke na Mwanaume. Mwanaume hapswi kufuata matakwa ya MKE au Mwanamke. Wote wanaofuata Kanuni hiyo mahusiano hayawezi kuwasumbua. Hata hivyo mwanaume kama kichwa cha Nyumba hapaswi kuwa muonevu na kutowatendea Haki Watu wa nyumba yake.
4. Mwanaume Halii
Mwanaume kujilizaliza, kutia Tia huruma, sijui. Kupiga magoti au kuwa chawa na mpambe mpambe kijingajinga Huko ni kujiingiza kwenye ushoga. Hakuna Mwanamke anayempenda mwanaume lainilaini, mliaji liaji, dekaji dekaji, hakuna.
Mahusiano lazima yakusumbue tuu!
Umetongoza Mwanamke kakukatalia Achana naye, usibembeleze na kujiliza Liza kama lipuuzi, usije ukadhani kujiliza ndio kutaugeuza moyo WA Mwanamke, zaidi Sana atakudharau.
Umepata matatizo kidogo unalia, sasa unalia nini kama mtoto, sasa Baba mzima unalia Mkeo na watoto wafanye nini. Mwanaume lazima uwe ngangari.
Hawa Wanawake wapo hivi walivyo Kwa sababu siku hizi wanaume wengi wamekuwa kama Wanawake.
Wanawake wanapenda Wanaume washoka, wahuni, wenye Roho ngumu, wasioogopa, wenye Akili, wenye maamuzi.
Nipumzike Sasa.
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam