Mama yangu adui yangu

Mama yangu adui yangu

Nikuonee aibu wewe kama nani kwangu mimi?Wewe kinakuuma kitu gani mimi ni Ki kopi na ku paste? umetumwa na hawa watu wako? nina kuheshimu na wewe niheshimu tafadhali kwenda zako shika mpango wako tafadhali usiniharibie usiku wangu MR. CONFIDENT


Mkuu MziziMkavu,achana nae huyo endelea kutuletea hilo story wengine hatuna muda wa kuyapata hayo magazeti,kwanza kama anavyosema kwamba alianza kuboreka baada ya mtunzi wa mwanzo kuanza kuzingua, basi wewe boresha tupe mautamu
 
Last edited by a moderator:
Last edited by a moderator:
MAMA YANGU ADUI YANGU -37-

ILIPOISHIA:
Ilikuwa baada ya kupoteza fahamu kwa siku mbili, kilichositisha kuzikwa kwangu ni joto la mwili ambalo wazee walisema wanaweza kunizika nikiwa bado hai.

Baada ya hapo sikuelewa kilichokuwa kikiendelea mpaka niliposhtuka pale nilipopiga chafya mfululizo.

Nilipofumbua macho nilijikuta sehemu ambayo haikuwa ngeni lakini bado sikuwa na uhakika nayo.

Nilipojaribu kunyanyuka nilishindwa, nilipojipapasa bado nilikuwa mifupa mitupu. Kutokana na harufu niliyokuwa nikiisikia nilijua pale ni kwa mganga.


Nilijiuliza kwa nini wamenipeleka tena kwa mganga ikiwa tulikubaliana nisubiri mauti yangu. Nikiwa bado katikati ya mawazo kwa nje ya chumba nilichokuwa nimelala, nilisikia sauti ya watu wakizungumza nje ya chumba.


SASA ENDELEA...


Nilisikia sauti ya mama akizungumza na sauti nyingine ambayo ilinishtua. Ilikuwa ya mtu ninayemfahamu lakini nilijua labda zinafanana na nyingine ilinishtua zaidi ilikuwa kama ya mama Amina mganga aliyenitibu mwanzo.
Nilimsikia akizungumza:

“Mmesikia chafya atakuwa amerudiwa na fahamu.”
“Hata mimi nimesikia.”
“Mmh! Akipona nitashukuru,” nilimsikia mama akisema.
“Tumuombe Mungu, lakini mwanao yote kayataka mwenyewe, nilimueleza arudi akadharau. Wagonjwa wengi wakipata nafuu huwa hawajali kumalizia tiba na kujiona wapo sawa matokeo yake ugonjwa unamrudia tena kwa kazi kubwa kwa vile vita inakuwa mara mbili.”

“Hakuniambia, kama angenieleza haya mapema ningemleta pengine hata ujauzito wake usingetoka.”
“Nilimwambia arudi niufunge lakini akadharau matokeo yake ni haya. Lakini nakuhakikishia Mwaija atatembea na kurudia katika hali yake ya kawaida.”

“Kweli?” mama aliuliza.

“Tatizo alilonalo likitoka mbona mwanao mzima, hilo nina uhakika wa kulitoa.”
Nilishangaa kusikia mganga akijiamini kupita kiasi, kwani hata mganga wa Yombo alisema hivyo lakini mwisho wa siku alichemka.
“Ngoja nikamuangalie.”

Baada ya kimya cha dakika chache nilisikia sauti za nyayo za miguu zikija ndani.
Nilitulia nikitizama juu kwa vile sikuwa na nguvu ya kujigeuza, nilivyolazwa ndivyo nilivyolala.

Baada ya muda nilisikia nikiitwa.
“Mwaija.”
“Abee,” niliitikia.

Baada ya kuitikia aliyeniita alisogea karibu yangu ndipo nilipomtambua vizuri kuwa ni mama Amina.

“Pole.”
Badala ya kuitikia nilianza kulia, mama Amina alinibembeleza:
“Mwaija utapona japo umechelewa sana.”

Lakini kumbe sikuwa nalia kwa maumivu bali aibu ya kumkimbia baada ya kupata ujauzito na kuondoka bila kurudi, pia kuwa muongo kwa niliyomuahidi.

“Silii hilo dada.”

“Unalia nini?”
“Nimekuwa muongo na hii ndiyo adhabu yangu.”
“Hebu achana na hayo, naomba nikupe uji wa dawa kwa vile sasa hivi huwezi kula chakula kigumu ili niendelee na tiba yako.”
“Sawa.”

Mama Amina alitoka na kuniacha nikiwa na maswali mengi, huku nikijiuliza ni nani aliyenipeleka kwake.

Baada ya muda alirudi na bakuli la uji akiwa ameongozana na mama pamoja na da’ Suzy hapo ndipo nilipojua aliyenileta kwa mama Amina ni da’ Suzy.

Nilijikuta nikisahau ugonjwa wangu na kutabasamu baada ya kumuona da’ Suzy japokuwa niliamini sura yangu ilikuwa kama ya mzee kutokana na kukonda kwa ugonjwa.

“Mwaija,” da Suzy aliniita
“Abee.”
“Pole mdogo wangu.”
“Sijapoa.”
“Utapona tu dada.”

“Mmh! Nitashukuru japokuwa imani yangu imekuwa ndogo sana.”
“Mwaija kwa uwezo wa Mungu utapona tu mdogo wangu,” mama Amina alinipa moyo.

Walisaidiana kunikalisha kisha nilipewa uji uliochanganywa na dawa. Japokuwa nilikuwa mgonjwa niliweza kuunywa wote uliokuwa kwenye bakuli.

Baada ya kunywa waliniacha nipumzike kwa muda. Baada ya muda nilifuatwa na kutolewa nje, ilionesha ni majira ya jioni inayokimbilia usiku kutokana na kigiza kuanza kuimeza nuru ya mchana.

Kama kawaida nilitolewa kwa kubebwa, ilikuwa yataka moyo kwani kila aliyenishika alishika mifupa. Nilitolewa uani na kulazwa kwenye mkeka.

Nilielezwa natolewa mdudu (jini) niliyetupiwa, kazi ya kumtoa ilianza mara moja.

Nilipewa dawa ya maji ambayo nilielezwa ni miti zaidi ya nane iliyokuwa imechangwanywa pamoja.

Baada ya kunywa nilianza kujisikia vibaya tumbo likaanza kunichanganya na kusikia kichefuchefu. Nilianza kutapika lakini hakuna kilichotoka nilipoanza kujigogoa, mama Amina alikuja na kuingiza vidole mdomoni kwangu kama anatafuta kitu na kukitoa kwa kukwangua.

Aliingiza vidole mpaka kwenye koromeo na kukwangua na kutoa vitu kama malenda na kusema anatoka. Sikuelewa anatoka nani, aliendelea kufanya vile na kutupa nje yale malenda.

Alifanya vile zaidi ya mara tano kisha alisema:
“Lilikuwa limeanza kukomaa lakini bahati nzuri limetoka lote.”

Bado sikuelewa lilikuwa limekomaa nini. Baada ya muda nilipewa uji wa dawa ambao ulinifanya niharishe mpaka nguvu ziliniishia. Mauti niliyaona mbele yangu, baada ya zoezi lile nilirudishwa ndani.

Kutokana na mshikemshike nilioupitia usingizi mzito ulinichukua.

Niliamshwa usiku sana na kupewa ndizi zilizopondwa na kulazimishwa kula japo mwili haukuwa na nguvu hata kidogo.

Baada ya kula nilirudi kitandani kulala. Siku ya pili niliamshwa na kupewa uji wa dawa na kupumzika. Majira ya saa nne nilipata kifungua kinywa cha nguvu. Nilishangaa siku ile nilikula vizuri.

Mama Amina aliniambia mdudu aliyekuwa akinisumbua ametoka. Japokuwa nilikuwa naumwa lakini nilikuwa na uwezo wa kuzungumza.

“Mdudu ndiyo nini?”

“Jini ulilotupiwa.”

“Unamaanisha limetoka?” sikuamini.

“Ndiyo.”

“Mbona yule mganga wa mwanzo alisema limetoka na kupata nafuu lakini matatizo yalizidi?”

“Hakumtoa.”

“Alifanya nini?”

“Alimpoza, waganga wengi huwapoza tu lakini hawawatoi.”

“Kwa hiyo wewe umemtoa?”

“Ndiyo.”

“Hatarudi tena?”

“Ndiyo.”

“Kwa hiyo nimepona.”

“Kwa vile kilichokuwa kikikumaliza tumekitoa nina imani sasa hivi afya yako itaimarika.”

Kauli ya mama Amina niliiamini kwa asilimia ndogo sana, niliamini alikuwa akinitia moyo tu. Ajabu mwili wangu ulikuwa

mwepesi tofauti na siku za nyuma ambapo nilikuwa nikiusikia kuwa mzito kama nimebebeshwa mzigo, hata kuhema

kwangu kulikuwa kwa shida lakini baada ya zoezi lile nilihema vizuri.

Nilikaa kwa mama Amina kwa siku kadhaa huku nikiendelea kutumia dawa zake. Alinieleza jini nililotupiwa lilitaka kufanya

viungo vyangu kupooza, kama ningechelewa mwili mzima ungekufa ganzi na kupooza kabisa.


Je nini kitaendelea? Fuatilia Jumapili ijayo
 
Mkuu tunaisubiria sana hii hadithi kwanini usiwe unaweka hata mbilimbili tu?
Ni ushauri na ombi...
 
Yule mzee katoweka kabisa .. binadamu siye hakika wa kumwamini ni Mola tu .. ufahari wote ule kwenye ugonjwa haonekani ... Mwenyezi Mungu tuepushe na maradhi ya sihr
 
MAMA YANGU ADUI YANGU -37-

ILIPOISHIA:
Ilikuwa baada ya kupoteza fahamu kwa siku mbili, kilichositisha kuzikwa kwangu ni joto la mwili ambalo wazee walisema wanaweza kunizika nikiwa bado hai.

Baada ya hapo sikuelewa kilichokuwa kikiendelea mpaka niliposhtuka pale nilipopiga chafya mfululizo.

Nilipofumbua macho nilijikuta sehemu ambayo haikuwa ngeni lakini bado sikuwa na uhakika nayo.

Nilipojaribu kunyanyuka nilishindwa, nilipojipapasa bado nilikuwa mifupa mitupu. Kutokana na harufu niliyokuwa nikiisikia nilijua pale ni kwa mganga.


Nilijiuliza kwa nini wamenipeleka tena kwa mganga ikiwa tulikubaliana nisubiri mauti yangu. Nikiwa bado katikati ya mawazo kwa nje ya chumba nilichokuwa nimelala, nilisikia sauti ya watu wakizungumza nje ya chumba.


SASA ENDELEA...


Nilisikia sauti ya mama akizungumza na sauti nyingine ambayo ilinishtua. Ilikuwa ya mtu ninayemfahamu lakini nilijua labda zinafanana na nyingine ilinishtua zaidi ilikuwa kama ya mama Amina mganga aliyenitibu mwanzo.
Nilimsikia akizungumza:

"Mmesikia chafya atakuwa amerudiwa na fahamu."
"Hata mimi nimesikia."
"Mmh! Akipona nitashukuru," nilimsikia mama akisema.
"Tumuombe Mungu, lakini mwanao yote kayataka mwenyewe, nilimueleza arudi akadharau. Wagonjwa wengi wakipata nafuu huwa hawajali kumalizia tiba na kujiona wapo sawa matokeo yake ugonjwa unamrudia tena kwa kazi kubwa kwa vile vita inakuwa mara mbili."

"Hakuniambia, kama angenieleza haya mapema ningemleta pengine hata ujauzito wake usingetoka."
"Nilimwambia arudi niufunge lakini akadharau matokeo yake ni haya. Lakini nakuhakikishia Mwaija atatembea na kurudia katika hali yake ya kawaida."

"Kweli?" mama aliuliza.

"Tatizo alilonalo likitoka mbona mwanao mzima, hilo nina uhakika wa kulitoa."
Nilishangaa kusikia mganga akijiamini kupita kiasi, kwani hata mganga wa Yombo alisema hivyo lakini mwisho wa siku alichemka.
"Ngoja nikamuangalie."

Baada ya kimya cha dakika chache nilisikia sauti za nyayo za miguu zikija ndani.
Nilitulia nikitizama juu kwa vile sikuwa na nguvu ya kujigeuza, nilivyolazwa ndivyo nilivyolala.

Baada ya muda nilisikia nikiitwa.
"Mwaija."
"Abee," niliitikia.

Baada ya kuitikia aliyeniita alisogea karibu yangu ndipo nilipomtambua vizuri kuwa ni mama Amina.

"Pole."
Badala ya kuitikia nilianza kulia, mama Amina alinibembeleza:
"Mwaija utapona japo umechelewa sana."

Lakini kumbe sikuwa nalia kwa maumivu bali aibu ya kumkimbia baada ya kupata ujauzito na kuondoka bila kurudi, pia kuwa muongo kwa niliyomuahidi.

"Silii hilo dada."

"Unalia nini?"
"Nimekuwa muongo na hii ndiyo adhabu yangu."
"Hebu achana na hayo, naomba nikupe uji wa dawa kwa vile sasa hivi huwezi kula chakula kigumu ili niendelee na tiba yako."
"Sawa."

Mama Amina alitoka na kuniacha nikiwa na maswali mengi, huku nikijiuliza ni nani aliyenipeleka kwake.

Baada ya muda alirudi na bakuli la uji akiwa ameongozana na mama pamoja na da' Suzy hapo ndipo nilipojua aliyenileta kwa mama Amina ni da' Suzy.

Nilijikuta nikisahau ugonjwa wangu na kutabasamu baada ya kumuona da' Suzy japokuwa niliamini sura yangu ilikuwa kama ya mzee kutokana na kukonda kwa ugonjwa.

"Mwaija," da Suzy aliniita
"Abee."
"Pole mdogo wangu."
"Sijapoa."
"Utapona tu dada."

"Mmh! Nitashukuru japokuwa imani yangu imekuwa ndogo sana."
"Mwaija kwa uwezo wa Mungu utapona tu mdogo wangu," mama Amina alinipa moyo.

Walisaidiana kunikalisha kisha nilipewa uji uliochanganywa na dawa. Japokuwa nilikuwa mgonjwa niliweza kuunywa wote uliokuwa kwenye bakuli.

Baada ya kunywa waliniacha nipumzike kwa muda. Baada ya muda nilifuatwa na kutolewa nje, ilionesha ni majira ya jioni inayokimbilia usiku kutokana na kigiza kuanza kuimeza nuru ya mchana.

Kama kawaida nilitolewa kwa kubebwa, ilikuwa yataka moyo kwani kila aliyenishika alishika mifupa. Nilitolewa uani na kulazwa kwenye mkeka.

Nilielezwa natolewa mdudu (jini) niliyetupiwa, kazi ya kumtoa ilianza mara moja.

Nilipewa dawa ya maji ambayo nilielezwa ni miti zaidi ya nane iliyokuwa imechangwanywa pamoja.

Baada ya kunywa nilianza kujisikia vibaya tumbo likaanza kunichanganya na kusikia kichefuchefu. Nilianza kutapika lakini hakuna kilichotoka nilipoanza kujigogoa, mama Amina alikuja na kuingiza vidole mdomoni kwangu kama anatafuta kitu na kukitoa kwa kukwangua.

Aliingiza vidole mpaka kwenye koromeo na kukwangua na kutoa vitu kama malenda na kusema anatoka. Sikuelewa anatoka nani, aliendelea kufanya vile na kutupa nje yale malenda.

Alifanya vile zaidi ya mara tano kisha alisema:
"Lilikuwa limeanza kukomaa lakini bahati nzuri limetoka lote."

Bado sikuelewa lilikuwa limekomaa nini. Baada ya muda nilipewa uji wa dawa ambao ulinifanya niharishe mpaka nguvu ziliniishia. Mauti niliyaona mbele yangu, baada ya zoezi lile nilirudishwa ndani.

Kutokana na mshikemshike nilioupitia usingizi mzito ulinichukua.

Niliamshwa usiku sana na kupewa ndizi zilizopondwa na kulazimishwa kula japo mwili haukuwa na nguvu hata kidogo.

Baada ya kula nilirudi kitandani kulala. Siku ya pili niliamshwa na kupewa uji wa dawa na kupumzika. Majira ya saa nne nilipata kifungua kinywa cha nguvu. Nilishangaa siku ile nilikula vizuri.

Mama Amina aliniambia mdudu aliyekuwa akinisumbua ametoka. Japokuwa nilikuwa naumwa lakini nilikuwa na uwezo wa kuzungumza.

"Mdudu ndiyo nini?"

"Jini ulilotupiwa."

"Unamaanisha limetoka?" sikuamini.

"Ndiyo."

"Mbona yule mganga wa mwanzo alisema limetoka na kupata nafuu lakini matatizo yalizidi?"

"Hakumtoa."

"Alifanya nini?"

"Alimpoza, waganga wengi huwapoza tu lakini hawawatoi."

"Kwa hiyo wewe umemtoa?"

"Ndiyo."

"Hatarudi tena?"

"Ndiyo."

"Kwa hiyo nimepona."

"Kwa vile kilichokuwa kikikumaliza tumekitoa nina imani sasa hivi afya yako itaimarika."

Kauli ya mama Amina niliiamini kwa asilimia ndogo sana, niliamini alikuwa akinitia moyo tu. Ajabu mwili wangu ulikuwa

mwepesi tofauti na siku za nyuma ambapo nilikuwa nikiusikia kuwa mzito kama nimebebeshwa mzigo, hata kuhema

kwangu kulikuwa kwa shida lakini baada ya zoezi lile nilihema vizuri.

Nilikaa kwa mama Amina kwa siku kadhaa huku nikiendelea kutumia dawa zake. Alinieleza jini nililotupiwa lilitaka kufanya

viungo vyangu kupooza, kama ningechelewa mwili mzima ungekufa ganzi na kupooza kabisa.


Je nini kitaendelea? Fuatilia Jumapili ijayo

yaani hapa Mzizi ndio wazidi kunifanya niwe addict na hizi mambo japo unaweka kwa matone tu ila kwa kweli kwa sie wazee wa suspense hapa tunakuwa hoi kabisa. Nimeenda internet cafe kisa hii hadithi maana huku kwetu naona Tanesco wanaajenda ya siri.
halafu nakuwa nawashangaa hawa wanaosema "oohh copy&paste" kwani wameona wote tunapenda hayo magazeti ya Udaku??? Ubarikiwe sana mkuu kwa kujitoa kwako!!:laugh::laugh::laugh::smiling::smiling:
 
MAMA YANGU ADUI YANGU -38-

ILIPOISHIA:
Kauli ya mama Amina niliiamini kwa asilimia ndogo sana kwa kuamini aliyosema ilikuwa kunipa moyo. Ajabu mwili wangu ulikuwa mwepesi tofauti na siku za nyuma ambao niliusikia mzito kama nimebebeshwa mzigo kizito hata kuhema kwangu kulikuwa kwa shida lakini baada ya zoezi lile nilihema vizuri.
Nilikaa kwa mama Amina kwa siku kadhaa huku nikiendelea kutimia dawa zake.Alinieleza jini nililotupiwa lilitaka kufanya viungo vyangu kupooza kama ningechelewa mwili mzima ungekufa ganzi na kupooza kabisa.
SASA ENDELEA...


Nilijiuliza hata kama ndiyo mke wa mzee Sambi kanifanya hivi kosa langu nini ikiwa alikubaliana na mumewe. Kama alikuwa akimtaka mumewe angenieleza kama ningekataa ndiyo angenitenda.

Moyoni niliwaza mengi baada ya kupina nami lazima nilipe kisasi kama alivyonifanyia. Baada ya tiba ile niliweza kukaa peke yangu baada ya wiki, nilishangaa mama kumsifia mama Amina, kwangu sikuona kigeni sana japokuwa nililetwa nusu mfu lakini haikuwa na tofauti na kwa mganga wa kwanza.

Niliendelea kukaa kwa mama Amina kwa kutumia dawa za kunywa na kufusha. Kila siku nilichuliwa sehemu zote zilizo kufa ganzi kama miguu ambayo ilikuwa haina nguvu.

Baada ya wiki moja nyingine niliweza kunyanyuka na kutembea kwa kushikwa. Niliendelea kutumia dawa ya kuchua na kunywa na kuweza kutembea mwenyewe japo kwa shida.

Pamoja na kutolewa kwenye umauti bado sikuwa na imani ya kurudia hali yangu ya zamani. Baada ya afya yangu kuimalika niliruhusiwa kuondoka lakini baada ya kupata kinga.
Niliweza kutembea lakini miguu bado ilikuwa haijakaa vizuri. Nilijiuliza yatakirudia ya mwanzo japo kulikuwa na tofauti na mganga wa mwanzo kwa kiasi kikubwa.

Niliendelea kutumia dawa ya kuchua kwa ajili yakuondoa ganzi miguuni ambayo iliondoka taratibu. Lakini ajabu muda wote sikumuona mzee Sambi.

Nilimuuza mama ambaye alinieleza niachane naye kama kila kitu kimekwenda vizuri.
“Lakini mama mtu niliyekuwa naishi naye kama mume na alikuwa mstari wa mbele katika matatizo yangu apotee ghafla lazima kutakuwa na kitu.”

“Sasa sisi tutajuaje, tulitakiwa kukuuliza wewe kwa vile baada ya siku ile ambayo ulisema ulimbana kuhusu yule mwanamke aliyekuja kwako kuwa ni mkewe alipoondoka hatujamuona tena.
“Ilitakiwa utumbie baada ya mazungumzo yale kuna kitu gani kingine kilitokea.”
“Mbona yalikuwa mazunguzo ya kawaida wala hakukuwa na kitu chochote kibaya.”

“Ndiyo maana nasema uachane naye, kama hamjakosana ameondoka akijua wewe ni mgonjwa. Hivi leo upo hivi nimuone nitamfukuza kama mbwa.”
“Lakini mama lazima nijue sababu.”
“Kama hakukwambia, mimi nitajuaje?”

“Mamaa ina maana naye anaweza kuondoka kana Beka?” kauli ya mama ilinishtua sana.
“Kwani Beka ulimfukuza?”
“Sijamfukuza, lakini aliniachia fumbo zito.”
“Fumbo gani?”

“Kwamba wewe unajua, lakini wewe umekataa. Kabla sijapata jibu inawezekana mzee Sambi naye kakimbia!”
“Hata akikimbia wewe umepungukiwa nini, hukutibiwa?”
“Nimetibiwa.”
“Sasa tatizo nini?”
“Mama hawezi kuondoka hivihivi lazima kuna sababu.”
“Mwaija mi nitajuaje, wewe ndiyo unanihusu wengine sijui chochote.”

“Mama sasa hivi sikubali lazima nijue sababu ya mzee Sambi kupotea ghafla tena kipindi cha matatizo mazito ambayo kwa upande mwingine ameyasababisha yeye.”

“Mwanangu wanaume wa sasa wanakupenda kwenye uzima yakikukuta unakula wewe na familia yako.”
“Mmh! Nitajua tu.”

“Utajua, lakini sasa hivi endelea kwanza kuimalisha afya yako. Sambi si muhimu kama afya yako ila sitaki kumuona kwa vile alikusudia kukuua.”
“Kivipi?”
“Mkewe aliyofanya madogo?”

“Sawa, lakini akija naomba usimfukuze ili aniambie sababu ya kunikimbia.”
“Hiyo mtajuana lakini kwangu sitaki kumuona.”
“Sawa, lakini kila kitu kitakuwa wazi.”

Kwa vile bado nilikuwa nahitaji msaada wa familia yangu kutokana na hali yangu kutengemaa taratibu sikuweza kurudi kwangu, niliendelea kukaa nyumbani.

Kwa vile muda ule kodi nayo ilikuwa imekaribia kwisha niliwatuma watu kuhamisha vitu vyangu vyote na kuvirudisha nyumbani. Kichwa changu kilikuwa kizito kuhusu kutoweka mzee Sambi bila taarifa. Pamoja na kujua mkewe ndiye mbaya wangu niliamini bado nikuwa nahitaji msaada wake.

Da’ Suzy ambaye alikuwa amekuja kwa muda Dar baada ya kuhamia Mwanza na mumewe. Alinieleza alivyonikuta siku aliyokuja kunitembelea.

“Mwaija Mungu mkubwa,” alisema huku akiniangalia kwa jicho la siamini.
“Kwa nini?”

“Nilivyokukuta siku ya kwanza na leo hii tunaongea hivi naamini Mungu mkubwa na Mungu yupo pia mama Amina mganga.”
“Kwani ilikuwaje?”
“Baada ya kufika Dar nilikuwa na hamu ya kuonana na wewe kipenzi changu japo niliondoka bila kukuaga na kubadili namba kwa ajili ya Emma.”
“Taarifa niliisikia.”

“Basi niliamua kuishi bila mawasiliano na mtu yeyote zaidi ya ndugu zangu. Baada ya kufika nilishinda siku moja na siku ya pili ndipo nilipokuja kwako ambako sikukuta mtu na ilionekana hakuna dalili za kuwepo.


Itaendelea Risasi Alkhamisi
 
MAMA YANGU ADUI YANGU -39-


ILIPOISHIA:
Da’ Suzy ambaye alikuwa amekuja kwa muda Dar baada ya kuhamia Mwanza na mumewe. Alinieleza alivyonikuta siku aliyokuja kunitembelea.
“Mwaija Mungu mkubwa,” alisema huku akiniangalia kwa jicho la siamini.
“Kwa nini?”
“Nilivyokukuta siku ya kwanza na leo hii tunaongea hivi naamini Mungu mkubwa na Mungu yupo pia mama Amina mganga.”
“Kwani ilikuwaje?”
“Baada ya kufika Dar nilikuwa na hamu ya kuonana na wewe kipenzi changu japo niliondoka bila kukuaga na kubadili namba kwa ajili ya Emma.”
“Taarifa niliisikia.”
“Basi niliamua kuishi bila mawasiliano na mtu yeyote zaidi ya ndugu zangu. Baada ya kufika nilishinda siku moja na siku ya pili ndipo nilipokuja kwako ambako sikukuta mtu na ilionekana hakuna dalili za kuwepo watu.
SASA ENDELEA...


Niliamua nije kwenu kukuulizia ndipo nilipofika na kukutana na mshtuko. Nilikuta watu wamekusanyika, nilipouliza niliambiwa umefariki.

Nilishindwa kuamini niliingia mpaka ndani na kushangaa kukuta watu wakijadiliana kuhusu hali yako. Wapo waliosema umekufa lakini mzee mmoja alikataa na kusema hujafa kwa vile kwa muda wote bado mwili wako ulikuwa na joto.
Walisema wasubiri siku mbili kama hali yako itabakia hivyo basi wakuzike. Mungu alinifungua akili ghafla ya kumkumbuka mama Amina.

Nilimpigia simu na kumwelezea hali yako, aliniambia nimpe muda kidogo. Baada ya muda alinipigia na kunieleza kuwa wewe ni mzima ila kilichotumwa kilikuwa katika hatua ya mwisho kukutoa uhai wako,” mmh! Zilikuwa habari zilizofanya nihisi mwili kusisimka.

Nilitulia nikimsikiliza da’ Suzy macho yamenitoka pima mkono shavuni kama akinihadithia mkasa wa kusikitisha wa mtu mwingine lakini ulikuwa wangu kwa vile yote yale yalipotokea sikuwa na fahamu nilikuwa nusu mfu.
Nimeamini katika maisha kama hujafa hujaumbika na kisemwacho kipo. Habari zilizokuwa zinanihusu nilisimuliwa na mtu mwingine nami kuwa msikilizaji.

Da’ Suzy aliendelea kunisimulia mkasa wangu mzito baada ya kuyaonja mauti na kuamini bila yeye ningezikwa ningali hai.
“Basi mdogo wangu baada ya kumuomba msaada wake wa haraka mama Amina, alitoa masharti tukubebe tukupeleke kwake kwa vile kwenu isingewezekana kukutibu.”

Kauli ile ilinishtua na kujiuliza kwa sababu gani tiba yangu isingewezekana nyumbani kwetu?
“Basi nilimweleza mama na kina dada kuhusu kukupeleka Mbagala kwa mama Amina walikataa kwa vile ilionesha familia yako ilikuwa imeisha kata tamaa na wewe kuwa hai.

“Kuna kipindi waliniambia maiti hii uipeleke wapi, nikuache ili mwili upoe waweze kukuzika.
Niliwakatalia kuwa wewe si maiti bali upo hai na kuwahakikishia ukipata tiba utapona. Kwa kweli ushindani ulikuwa mkubwa na kujikuta nikiangua kilio ili nikupeleke kwa mama Amina.

Walinikubalia huku nikipewa masharti kama umekufa basi mwili nitaurudisha mwenyewe bila kuwashirikisha. Huwezi kuamini Mwaija hali niliyokuona nayo ilinipa ujasiri wa ajabu na kukuchukua mpaka kwa mama Amina.

Nilipokufikisha nilishtuka kumuona hata mama Amina naye akishtuka baada ya kukuona jinsi ulivyokuwa. Mwaija ulikuwa mfu kabisa mdogo wangu na kuniuliza.
“Mmh! Wewe mbona kama mgonjwa ameisha kufa?”
“Yupo hivi siku ya pili leo na ulipo angalia yupo hivihivi.”
“Mmh! Ipo kazi.”

Tulikuingiza ndani na haraka alianza kazi ya kukutibu ikiwa kupakwa mafusho ambayo alisema yalipunguza nguvu ya mdudu aliyekuwa amekushika.

Alichukua dawa ya majani na kukuwekea puani na kutueleza baada ya muda utapiga chafya. Na kweli ilichukua nusu saa ulipiga chafya ndipo mama Amina alipokuja ndani kukuangalia na kusema umerudiwa na fahamu.

Mama yako hakuamini alikuwa na hamu ya kukuona. Tuliingia na kumsaidia mama Amina kukunywesha uji. Hali uliyokuwa nayo pamoja na mama Amina kutupa moyo bado sikuamini kama ningeweza leo kuongea na wewe hivi kweli Mungu mkubwa,” da’ Suzy alinisimulia kwa uchungu mpaka machozi yalimtoka.

Maelezo ya Da’ Suzy yaliusisimua mwili wangu na kujiuliza mateso kama yale mpaka lini. Moyo uliniuma lakini nilishindwa nifanye nini. Nilimshukuru da’ Suzy kwa ujio wake kwa kuamini kama asingetokea basi nilikuwa nazikwa hai. Pia nilimshukuru kwa

kujitolea kwa hali na mali kuhakikisha afya yangu inaimarika ikiwa pamoja na kunipeleka kwa mama Amina.

Kutokana na moyo wa utu ilibidi apitishe muda wake wa kuondoka ili kuhakikisha anakuwa na mimi mpaka muda ule. Siku za mwanzo kuwa kwa mama Amina nilikuwa na da Suzy pamoja na ndugu zangu.

Aliendelea kunipa moyo na kunihakikishia matatizo yanayonikabili yataisha na kurudi kwenye hali yangu.
“Da Suzy kwa nini kila maisha yangu yakianza kuwa mazuri napata matatizo makubwa? Unafikiri lini nitayafurahia maisha kama wengine?”

“Mdogo wangu kila kitu chenye mwanzo hakikosi mwisho, ipo siku utasahau yote haya yatakuwa simulizi kwa wanao.”
“Mmh! Sina uhakika wa kupata mtoto kwani kila tatizo huanzia kwenye ujauzito.”
“Mwaija hili umelitaka mwenyewe, mama Amina alikueleza urudi lakini kwa kiburi chako ukaona ulielezwa mambo ya kitoto,” da’ Suzy alinilaumu.
“Dadaa, niliogopa kumshirikisha mzee Sambi kuwa ujauzito wangu umetokana na kutumia miti shamba. Kingine muda mwingi alikuwa karibu yangu na wewe ukaondoka ghafla nikakosa mtu wa kunisukuma kwenda kwa mama Amina.”
“Umeelezwa matatizo yako unafanya mchezo, Mwaija wewe si mtoto mdogo dunia ya leo bila kuhangaika unakufa unajiona.”
“Unajua mpaka sasa sielewi kabisa.”
“Kitu gani?”
“Alivyoondoka mzee Sambi hana tofauti na mume wangu Beka.”
“Mwaija kwa nini usimweleze mama Amina nina imani atakusaidia.”
“Sawa, itabidi nikifuata dawa ya kuchua nitamweleza.”
“Vipi kwanza miguu?”
“Sijambo, sasa hivi naweza hata kukimbia. Sijui mama Amina nimpe zawadi gani.”
“Yoyote, mbona yule mama hana tamaa za kijinga.”

Baada ya wiki da’ Suzy aliondoka kuelekea Mwanza. Nilimtakia safari njema na kumuombea kila lenye heri limtangulie na kumuepusha na kila la shari. Niliamini sikuwa na uwezo wa kumlipa yote aliyonifanyia bali Mungu peke yake.

Nami hali yangu ilitengemaa na kuweza kufanya kitu chochote bila msaada wa mtu. Nilitoka siku moja bila kumtaarifu mtu na kwenda saiti kuangalia nyumba yangu japokuwa mama alinikataza niachane na kila kitu cha mzee Sambi.

Nilipanda daladala hadi Mwenge na kuunganisha kuelekea Bunju. Nilipofika kwa mbali niliona jumba limependeza likiwa limekamilika.
Uzio ulikuwa umeisha jengwa na kuwekwa geti la chuma. Nilisogea mpaka pale getini, bahati nzuri mlango mdogo wa geti la kuingilia ulikuwa wazi.

Niliingia ndani, nilipotupa macho kwa mbele nilishtuka kumuona mzee Sambi na mkewe na mwanaume mwingine akiwa na mkewe wakizungumza.

Sikujua walikuwa wakizungumza nini na wale watu. Nilirudi nje haraka ili wasinione, wakati huo nao walionekana wanatoka, niliwachungulia kupitia kwenye tundu la mlangoni na kuona wote wakiingia kwenye magari yao ili waondoke.

Nilimuona mlinzi akisogea mlangoni kufungua geti, nilijificha nyuma ya mti uliokuwepo pale. Baada ya muda gari zilitoka na kuelekea mjini. Pamoja na kuyaona yale yote bado sikujua nini kinaendelea.

Magari yalipotoka na geti kufungwa nilisogea getini ili kutaka kujua zaidi kuhusu ile nyumba yangu. Niligonga geti na mlinzi alitoka na kuniuliza:

“Nikusaidie nini dada, kama kazi sasa hivi hakuna nyumba imemalizika. “
“Sina shida hiyo.”
“Una shida gani?”
“Samahani kaka una muda gani hapa?”


Itaendelea Jumamosi ijayo......
 
Yaan utamu unakuja afu unakata!!
Ayaaaah!
Kwa hasira nakuja j.mos ileee ya tatu(sjui kama ntaweza lkn ntajtahd) ili nikute kama ni mchicha basi umeota vizur mkubwa mkubwa
 
Back
Top Bottom