Mama yake alimuachia laana 'kamlalia vibaya', mambo yake yanamuendea kombo

Nitakujibu kwa machache:
1. Laana huwezi wewe kumlaani mtu ikampata kama wewe huna laana. Mtu yeyote mdhambi, tiyari kisha laaniwa. Hawezi kujikinga laana kwani laana tiyari ipo juu yake.
2. Hawezi kwenda kumuomba huyo mamake aliyekwisha kufa kwa sababu, Marehemu sasa kishatoka katika mwili na yeye yupo katika mwili. Utamuombaje asiyekuwepo pamoja nasi chochote?? Naomba uelewe kwamba ukiisha kufa, wewe moja kwa moja upo mahali pa kungojea hukumu tu. Kitabu cha Waebrania 9 : 27 Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja na baada ya kufa hukumu.
Hapo hakuna mahali popote ambapo panasema ati tunaweza kupatana naye tena.
3. Nimesema, Laana hutoka kwa mwenye laana, Mungu ndiye mwanzo wa kila kitu unachokijua, na hata usichokijua. Yeye ndiye Alfa na Omega. Mwanzo na Mwisho. Yaani, hata hiyo laana ni mali yake. Hupenda kufanya atakavyo. Alikuambia, Ukifanya hivi, HAKIKA laana itakupata. Ukifanya hivi, HAKIKA baraka zitakupata. Je, kuna mtu awezaye kumuambia mwingine hivyo?? Jibu ni, HAPANA. Ni Mungu tuu awezaye kusema nayo ikawa.
4. Kilicho nyuma ya laana nimekuambia kuwa, Kama mtu yupo chini ya laana yaani ni mdhambi, huyo akikulaani wewe uliye chini ya laana yaani mdhambi, utallanika.
5. Niliposema; Ampokee Yesu awe Bwana na Mwokozi wake ni kuwa; Yesu alikufa kwa ajili ya dhambi zetu. Imeandikwa; Amelaaniwa yeye aliyetundikwa juu ya mti. Hivyo Yesu alilaaniwa kwa ajili yetu ili sisi tuliokuwa chini ya kongwa la dhambi tuwe huru kwa kulipiwa hilo deni letu na uhai wake Yesu Kristo.
Njoo PM kwa mafundisho zaidi.
Mkuu nipo tofauti nawewe kidogo japokuwa unaonekana umesoma sana vitabu vya dini...
Mtu yoyote anaweza kukulaani katika haki yake.. ukiachana na mambo ya kidunia katika roho na kweli mungu ametuumba kila mtu na haki yake na sisi sote ni watoto wake..
Ikitokea umemdhulumu mtu haki yake(ukamkwamisha katika mambo yake au kumuweka katika wakati mgumu) na muhusika akasikitika sana.. basi ndugu yangu amini laana lazima ikuandame na mungu atakusamehe kupitia kwa huyo mtu uliyemdhulumu(umuombe msamaha kwa njia unayoijua wewe moyo wake uwe mweupe kabisa)
tofauti na hapo maisha yako yatakuwa magumu sana
 
Mkuu nipo tofauti nawewe kidogo japokuwa unaonekana umesoma sana vitabu vya dini...
Mtu yoyote anaweza kukulaani katika haki yake.. ukiachana na mambo ya kidunia katika roho na kweli mungu ametuumba kila mtu na haki yake na sisi sote ni watoto wake..
Ikitokea umemdhulumu mtu haki yake(ukamkwamisha katika mambo yake au kumuweka katika wakati mgumu) na muhusika akasikitika sana.. basi ndugu yangu amini laana lazima ikuandame na mungu atakusamehe kupitia kwa huyo mtu uliyemdhulumu(umuombe msamaha kwa njia unayoijua wewe moyo wake uwe mweupe kabisa)
tofauti na hapo maisha yako yatakuwa magumu sana
Acha nitofautiane na weye kidogo.
1' Laana hutokea kwa mlaaniwa. Kama yeye amelaaniwa atalaani.
2. Kama huna laana haiwezi kukupata kwa sababu weye haupo kwenye laana.
3. Kama hujamkosea mtu akikulaani ni bure tu na pia huwezi omba radhi kwa usilokosea.
4. Ukiisha jiingiza kwenye dhuluma au uonevu tiyari umejiingiza kwenye laana. Hivyo epuka mambo yawezayo kukuingiza ndani ya laana nawe utakuwa mbali na laana hivyo huto laanika
 
Mimi sikubali kuwapo kwa nguvu zisizo za kiasili (supernatural forces). Siamini uwepo wa Mungu, Malaika, Shetani, Uchawi, laana etc.

Lakini, nakubali kwamba, hizi zote ni vitu ambavyo Kiingereza vinaitwa "memes".

Ni mambo fulani yaliyo katika utamaduni na jamii, yamejengeka kwa watu kufuatilia mambo kwa miaka mingi, na kuja na taratibu fulani, ambazo hata kama hazina ukweli wa moja kwa moja, msingi wake una mantiki fulani.

Nitakupa mfano.

Watu fulani wa kijijini ambao hawakuwa na elimu, hawakuwa wasomi, hawakujua kemia, walikumbwa na tatizo, kisima chao kilipata kupitia kwenye mawe fulani yenye sumu, maji ya kisima yakawa yameingia sumu, yakawa yanawapa watu magonjwa na kuwaua.

Kwa kuwa wale watu hawakujua habari za kemia za miamba na sababu halisi iliyofanya maji yale yaue watu, walijitungia hadithi yao, kwamba, kisima kile kimeingiliwa na mizimu na majini, na hivyo watu waache kunywa maji, wakinywa maji yale, watakufa.

Sasa, akaja mtu kutoka mjini, msomi. Akasikia habari za isima chenye majini. Yeye msomi, hakubali uwepo wa majini. Akasema nyinyi watu wa kijijini washenzi, mnaamini majini wakati hakuna kitu kama hicho. Mimi nitawaonesha kwamba hakuna majini. Nitakunywa maji ya hicho kisima mnachosema kina majini, na majini yenu hayatanifanya kitu.

Alijua kwamba hakuna majini. Akanywa maji. Maji yakamdhuru, akaanza kuumwa, akawahishwa hospitali, kumpima, wakakuta kwamba, kuna usafishaji wa dhahabu unaotumia madini yenye sumu hapo karibuni, na madawa yale ya kuchimba dhahabu yameingia kwenye water table na kufanya kisima kiwe na sumu.

Hospitalini wakampa dawa za kumuuguza.

Ikaja kuonekana kwamba, ile hadithi ya "msinywe maji ya kisima hiki, kisima kina majini" ingawa ilikuwa si kweli kwa maana ya kwamba kisima hakikuwa na majini, hadithi ile ndiyo ilikuwa inaeleweka vizuri kabisa na watu wa pale kuwakataza wasinywe maji.

Tukienda kwenye laana, hakuna kitu kama laana kusema mama anampa laana mwanawe halafu inampata. Ndiyo maana mtoto ambaye hajafanya baya akipewa laana na mama yake haimuathiri.It is symbolic.

Kinachotokea ni kwamba, mzazi kikawaida ni mtu mwenye mapenzi na mwanawe, hususan mama. Kwa hivyo, si rahisi kusema maneno ya kutoa laana bila sababu. Kinachotokea ni kwamba, mpaka mama kusema maneno ya laana, mtoto tayari anakuwa kashafanya mambo ya kuharibikiwa. Ile laana inatolewa baada ya mtoto kuonesha kuharibikiwa, ni matokeo ya kuharibikiwa, si sababu ya kuharibikiwa.

Sasa kwetu Waswahili tukiona mama anasema ananawa mikono, kuhusu mtoto wake, kwa sababu mtoto mwizi, anatumia madawa etc, halafu huyo mtoto akaja kuuawa kwa wizi, tunasema amekuja kuuawa kwa sababu ya laana, wakati laana ilitolewa wakati mtoto kashaonesha ana muelekeo mbaya tayari.

Hakuna mama mwenye akili timamu anayeweza kumsemea maneno ya laana mtoto wake kama mtoto anafanya mambo vizuri tu.

Na laana hiyo ikitolewa, haitakuwa na lolote baya litakalotokea.
Asante nimekuelewa zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom