strategist22
JF-Expert Member
- Jun 6, 2017
- 655
- 594
Wanabodi,humu nimekuwa nikijifunza mambo mengi sana toka nimejiunga hapa 2014 .Naamini kuna watu makini wenye uelewa mkubwa wa elimu ya ulimwenguni huku ,elimu au maarifa yasiyosemwa au yaliyopuuzwa na watu wengi zama hizi.
Naamini swala hili litapata ufumbuzi kama mengine mengi yanayoletwa humu. Nina mambo machache na hitaji kujifunza hapa, haya maswali yanaulizwa sana sana,wengi wanajiuliza hasa wakifiwa.Dini nyingi zimejaribu kujibu maswali haya ,nahitaji kujua zaidi ya majibu hayo.Mimi ni Mkristo,nimesoma na dini nyingine Kwa kiasi chake.
Wiki iliyopita nilirudi nyumbani,kwa zaidi ya miaka miwili hawakuniona.Nilipita kusalimia ndugu na jamaa,nilipita kwa baba wa rafiki yangu,kumjulia hali pia kumpa pole ,mke wake alifariki mapema mwaka 2018. Pamoja na hayo nilihitaji kujua alipo rafiki yangu,toka January nimekuwa nikimpigia simu bila mafanikio.
Rafiki yangu alikuwa anajihusisha na biashara na ufugaji,halipiga hatua sana.Tulimuona kijana wa mfano,kupambana na maisha,lakin hakuwa na mahusiano mazuri na wazazi wake.Mama yake alimwambia,asisogelee jeneza lake akifa.Saivi ni mwaka na miezi kadhaa kilakitu amekwama ,amerudi hatua nyingi nyuma. Kama kapagawa ,anashinda ndani au la maporini .
Mazungumzo na baba yake kwa ufupi ni kuhusu matatizo ya rafiki yangu na utatuzi wake.anasema
"Mwenzako yupo gizani,ameandamwa na mikosi,Mama yake amemlalia vibaya huko,ananung'unika hata kwenye msiba hakumuona.Mshauri rafiki yako akaombe msamaha ,pia akubali kufanyiwa mila nyingine atoke kizani,Mimi hataki hata kuniona,nimemtumia wadogo zake,aje nyumbani hataki ,nimemfata kwake mara4 anajifungia ndani"
Baada ya mazungumzo hayo nikajaa na maswali haya.
1:Kudharau au kupuuza mila kunaweza kukuletea matatizo?
2;Je wafu wanaweza kuzuia mambo yetu?kwa namna gani?
3:Je wafu wanasikia ? Wanaona?
4:Je wanasamehe?
5:Je wanachukia?nini kinafanya wachukie?
6:Je wanaweza kutusaidia?kwa jinsi gani?
7;Wapo wapi ?wanafanya nini?
8:Je tunaweza kuonana nao?
9:Ongeza cha ziada,kama kipo kupanua zaidi mada.
NB:Nahitaji kujua , haya nje ya mfumo wa dini,watu wanaelewa nini ? wanafanya nini?, Katika mazingira kama haya.
Asanteni
Naamini swala hili litapata ufumbuzi kama mengine mengi yanayoletwa humu. Nina mambo machache na hitaji kujifunza hapa, haya maswali yanaulizwa sana sana,wengi wanajiuliza hasa wakifiwa.Dini nyingi zimejaribu kujibu maswali haya ,nahitaji kujua zaidi ya majibu hayo.Mimi ni Mkristo,nimesoma na dini nyingine Kwa kiasi chake.
Wiki iliyopita nilirudi nyumbani,kwa zaidi ya miaka miwili hawakuniona.Nilipita kusalimia ndugu na jamaa,nilipita kwa baba wa rafiki yangu,kumjulia hali pia kumpa pole ,mke wake alifariki mapema mwaka 2018. Pamoja na hayo nilihitaji kujua alipo rafiki yangu,toka January nimekuwa nikimpigia simu bila mafanikio.
Rafiki yangu alikuwa anajihusisha na biashara na ufugaji,halipiga hatua sana.Tulimuona kijana wa mfano,kupambana na maisha,lakin hakuwa na mahusiano mazuri na wazazi wake.Mama yake alimwambia,asisogelee jeneza lake akifa.Saivi ni mwaka na miezi kadhaa kilakitu amekwama ,amerudi hatua nyingi nyuma. Kama kapagawa ,anashinda ndani au la maporini .
Mazungumzo na baba yake kwa ufupi ni kuhusu matatizo ya rafiki yangu na utatuzi wake.anasema
"Mwenzako yupo gizani,ameandamwa na mikosi,Mama yake amemlalia vibaya huko,ananung'unika hata kwenye msiba hakumuona.Mshauri rafiki yako akaombe msamaha ,pia akubali kufanyiwa mila nyingine atoke kizani,Mimi hataki hata kuniona,nimemtumia wadogo zake,aje nyumbani hataki ,nimemfata kwake mara4 anajifungia ndani"
Baada ya mazungumzo hayo nikajaa na maswali haya.
1:Kudharau au kupuuza mila kunaweza kukuletea matatizo?
2;Je wafu wanaweza kuzuia mambo yetu?kwa namna gani?
3:Je wafu wanasikia ? Wanaona?
4:Je wanasamehe?
5:Je wanachukia?nini kinafanya wachukie?
6:Je wanaweza kutusaidia?kwa jinsi gani?
7;Wapo wapi ?wanafanya nini?
8:Je tunaweza kuonana nao?
9:Ongeza cha ziada,kama kipo kupanua zaidi mada.
NB:Nahitaji kujua , haya nje ya mfumo wa dini,watu wanaelewa nini ? wanafanya nini?, Katika mazingira kama haya.
Asanteni