EP cosmetics
JF-Expert Member
- Oct 18, 2015
- 2,469
- 3,840
(Sehemu ya Kwanza)
UTANGULIZI
Andiko langu hili limelipanga katika sehemu mbili. Sehemu ya kwanza inahusu nadharia tete zangu kuhusiana na mdororo wa elimu na mmomonyoko wa maadili katika nchi za Kiafrika na kati ya watu weusi tuishio barani Afrika kwa ujumla. Sehemu ya pili inahusu mkasa unaotazamiwa wa kufutwa kwa somo la Falsafa katika taasisi zetu za elimu.
Kama nitakayosema si kweli basi ni nadharia zangu tete. Kama mambo hayo hayapo sasa basi labda yanakuja. Bila shaka, kila mzazi na mwanadamu anayejali na anayetazama vizuri maendeleo ya dunia, anafuatilia maendeleo ya watoto, vijana na Waafrika kwa ujumla.
Swali lake la maana ni “Kuna nini?” Kuna nini kwani kuna nini? Hili ni swali linaloendesha mbio mioyo ya wazazi na walezi wengi wenye kujali. Wasiojali wanatazama mambo haya kama watazamaji waliojihudhurisha kushuhudia mechi fulani ya mpira wa miguu. Kifupi, kuna ishara nyingi za kuporomoka viwango vya elimu barani mwetu.
I. KUTENGENEZEKA MATAAHIRA
Sikilizeni king’ora changu. Tunatengenezeka mataahira. Miaka 100 ijayo Afrika itajaa mazombi, mataahira wasioweza kujua jema/zuri wala ubaya. Natoa mifano mine kushadidia neno hilo. Mifano yangu nimeichapua kutoka sehemu nne nyeti: ofisi ya maamuzi, darasani, kwenye umma na kanisani. Ofisi ya Maamuzi
Vyombo vya juu vya elimu vinashinikiza kuondoa somo la Falsafa katika mfumo wa elimu. Kuna shida. Yaani watu wenye PhD wanataka somo la Falsafa liondolewe vyuoni sijui likishaondolewa “PhD” itamaanisha nini tena. Hisia zangu ni kwamba watu hao wenye vyeti vilivyoandikwa “PhD” hawajui hata maana ya “Ph” katika “PhD” walizopata. Inatisha. Je, si ishara ya mdororo wa elimu huo?
Darasani Kuna wanafunzi hata wa shahada wasiojua mambo ya msingi. Inasikitisha maana elimu ya Chuo Kikuu ndiyo elimu ya juu kuliko ya sekondari. Kama juu kunavuja, chini kumelowaje? Wanasema Waswahili, “Ukiona kilemba kimechafuka, usiulize makubasi!” Nina ushahidi. Nimeshuhudia mwanafunzi wa shahada ya kwanza ya ualimu katika historia asiyejua historia ya nchi yake, Tanzania. Aliombwa azitaje tawala tatu zilizotokana na utawala wa Mbwambo wa Upare akaandika eti ni Afrika ya Kusini, Burkina Faso na Palestina. Hii maana yake hata Jiografia ya Tanzania hajui. Sasa mtu kama huyu atawafundisha nini watoto? Mwalimu wa historia asiyejua historia ya nchi yake mwenyewe atafundisha nini?
Kwenye Umma Nina ushahidi watoto wetu kuzidi kuwa wazito madarasani zaidi na zaidi. Lakini kusudi eti waonekane wamefaulu ufaulu wa juu, alama A imeshushwa ianzie 75%. Pamoja na kushushwa hivyo “maksi”, baadhi ya wanafunzi wanamaliza masomo pasipo kujua kuandika wala kuhesabu.
Hapa usiseme wanaomaliza masomo pasipo kujua kuandika vizuri pamoja na kushindwa kushika masomo wanayofundishwa. Hali ni mbaya mintarafu matumizi ya alama za uandishi, uandikaji maneno na matumizi ya aina za maneno, hususani nomino, vivumishi na vitenzi. Kwa mtu anayejua kanuni za lugha inakera sana vijana wanapoamua kujionesha kuwamo katika lugha za kigeni kama Kiingereza wakisema “Kiswanglish.” Hapo utasikia au utasoma vitu kama “kudefence”, “kuperfomance”, “kuleft” n.k. Yaani wanachukua nomino au vitenzi vilivyo katika muda uliopita kutengenezea vitenzi vya wakati uliopo jambo ambalo ni sawa na kujenga maneno kama “kumlo”, “kuchakula”, “kumasomo”, “kulikwenda” n.k.
Si haya tu, mdororo wa elimu unaakisiwa kwa nguvu mitandaoni kwa vijana wengi kushindwa kujibu hoja na badala yake kujibu kwa litania za matusi. Mtu anaandika kitu, anakuja mtu anamtukana tu.
Kanisani Baadhi ya viongozi na walimu wa dini waliotarajiwa kuwa wajuzi kusudi wafundishe kweli wanadhihirisha dhahiri shayiri kwamba nao ni wale wale.
Nimeliona andiko moja la mwalimu wa kutegemeeka sana katika Karismatiki akijadili kwa namna ya kusikitisha mada ya kuwinga pepo. Kiongozi huyo anajidai kujua Kiingereza. Lakini maneno anayojinasibu kuyajua wala hayajui. Anajinasibu kuwa anatofautisha “deriverlance” na “exoticism” vitu ambavyo sijui ni nini. Hii maana yake kama hajui hata kuandika (spell) istilahi anazozijadili hajui maana yake. Maneno unayoyajua lazima ujue yanavyoandikwa. Jiulize katika mfano huu “deriverlance” na “exoticism” ni nini? Natumaini anamaanisha “deliverance” na “exorcism.” Maskini mwalimu, eti hawezi kuona tofauti hapa!
Hadi hapa, naomba uhisi kitu. Kuna kitu. Kuna namna ya mdodoro wa kielimu. Kuna ujinga. Lakini shida si jambo hili tu. Kimaadili, tunastaajabu heshima na adabu vinavyomong’oka. Watoto na vijana wetu wanakazana kuyatoa mambo ya vyumbani hadharani.
Wasanii wetu wengi wakiimba wanaimba matusi na wakicheza wananengua viuno pasipo soni. Kifupi, wasanii wetu wanauziwa propaganda zozote hata zile za kuwadhalilisha wenyewe kijinsia na wanazinunua kwa rejareja. Hii maana yake akili yao imekaa henamu sana hawawezi kujitegemea katika kufikiri. Kwa maneno mengine akili ya kuambiwa hawachanganyi na zao.
Wasanii wengi wamekoma kuwa vioo vya jamii. Kwa kisa hicho, wamekuwa rahisi kupokea hata propaganda za ushoga na usagaji. Katika hili, hali ya kustaajabisha ni hiyo kwamba mtoto wa kiume anaweza kukubali kutumika kama mwanamke na mtoto wa kike kujigeuza kidume. Kwa nini mambo yanakwenda hivi? Zifuatazo ni nadharia zangu tete kuelezea mkasa huo.
Mzee wenu Pd. Titus Amigu.
Copy & Paste.
UTANGULIZI
Andiko langu hili limelipanga katika sehemu mbili. Sehemu ya kwanza inahusu nadharia tete zangu kuhusiana na mdororo wa elimu na mmomonyoko wa maadili katika nchi za Kiafrika na kati ya watu weusi tuishio barani Afrika kwa ujumla. Sehemu ya pili inahusu mkasa unaotazamiwa wa kufutwa kwa somo la Falsafa katika taasisi zetu za elimu.
Kama nitakayosema si kweli basi ni nadharia zangu tete. Kama mambo hayo hayapo sasa basi labda yanakuja. Bila shaka, kila mzazi na mwanadamu anayejali na anayetazama vizuri maendeleo ya dunia, anafuatilia maendeleo ya watoto, vijana na Waafrika kwa ujumla.
Swali lake la maana ni “Kuna nini?” Kuna nini kwani kuna nini? Hili ni swali linaloendesha mbio mioyo ya wazazi na walezi wengi wenye kujali. Wasiojali wanatazama mambo haya kama watazamaji waliojihudhurisha kushuhudia mechi fulani ya mpira wa miguu. Kifupi, kuna ishara nyingi za kuporomoka viwango vya elimu barani mwetu.
I. KUTENGENEZEKA MATAAHIRA
Sikilizeni king’ora changu. Tunatengenezeka mataahira. Miaka 100 ijayo Afrika itajaa mazombi, mataahira wasioweza kujua jema/zuri wala ubaya. Natoa mifano mine kushadidia neno hilo. Mifano yangu nimeichapua kutoka sehemu nne nyeti: ofisi ya maamuzi, darasani, kwenye umma na kanisani. Ofisi ya Maamuzi
Vyombo vya juu vya elimu vinashinikiza kuondoa somo la Falsafa katika mfumo wa elimu. Kuna shida. Yaani watu wenye PhD wanataka somo la Falsafa liondolewe vyuoni sijui likishaondolewa “PhD” itamaanisha nini tena. Hisia zangu ni kwamba watu hao wenye vyeti vilivyoandikwa “PhD” hawajui hata maana ya “Ph” katika “PhD” walizopata. Inatisha. Je, si ishara ya mdororo wa elimu huo?
Darasani Kuna wanafunzi hata wa shahada wasiojua mambo ya msingi. Inasikitisha maana elimu ya Chuo Kikuu ndiyo elimu ya juu kuliko ya sekondari. Kama juu kunavuja, chini kumelowaje? Wanasema Waswahili, “Ukiona kilemba kimechafuka, usiulize makubasi!” Nina ushahidi. Nimeshuhudia mwanafunzi wa shahada ya kwanza ya ualimu katika historia asiyejua historia ya nchi yake, Tanzania. Aliombwa azitaje tawala tatu zilizotokana na utawala wa Mbwambo wa Upare akaandika eti ni Afrika ya Kusini, Burkina Faso na Palestina. Hii maana yake hata Jiografia ya Tanzania hajui. Sasa mtu kama huyu atawafundisha nini watoto? Mwalimu wa historia asiyejua historia ya nchi yake mwenyewe atafundisha nini?
Kwenye Umma Nina ushahidi watoto wetu kuzidi kuwa wazito madarasani zaidi na zaidi. Lakini kusudi eti waonekane wamefaulu ufaulu wa juu, alama A imeshushwa ianzie 75%. Pamoja na kushushwa hivyo “maksi”, baadhi ya wanafunzi wanamaliza masomo pasipo kujua kuandika wala kuhesabu.
Hapa usiseme wanaomaliza masomo pasipo kujua kuandika vizuri pamoja na kushindwa kushika masomo wanayofundishwa. Hali ni mbaya mintarafu matumizi ya alama za uandishi, uandikaji maneno na matumizi ya aina za maneno, hususani nomino, vivumishi na vitenzi. Kwa mtu anayejua kanuni za lugha inakera sana vijana wanapoamua kujionesha kuwamo katika lugha za kigeni kama Kiingereza wakisema “Kiswanglish.” Hapo utasikia au utasoma vitu kama “kudefence”, “kuperfomance”, “kuleft” n.k. Yaani wanachukua nomino au vitenzi vilivyo katika muda uliopita kutengenezea vitenzi vya wakati uliopo jambo ambalo ni sawa na kujenga maneno kama “kumlo”, “kuchakula”, “kumasomo”, “kulikwenda” n.k.
Si haya tu, mdororo wa elimu unaakisiwa kwa nguvu mitandaoni kwa vijana wengi kushindwa kujibu hoja na badala yake kujibu kwa litania za matusi. Mtu anaandika kitu, anakuja mtu anamtukana tu.
Kanisani Baadhi ya viongozi na walimu wa dini waliotarajiwa kuwa wajuzi kusudi wafundishe kweli wanadhihirisha dhahiri shayiri kwamba nao ni wale wale.
Nimeliona andiko moja la mwalimu wa kutegemeeka sana katika Karismatiki akijadili kwa namna ya kusikitisha mada ya kuwinga pepo. Kiongozi huyo anajidai kujua Kiingereza. Lakini maneno anayojinasibu kuyajua wala hayajui. Anajinasibu kuwa anatofautisha “deriverlance” na “exoticism” vitu ambavyo sijui ni nini. Hii maana yake kama hajui hata kuandika (spell) istilahi anazozijadili hajui maana yake. Maneno unayoyajua lazima ujue yanavyoandikwa. Jiulize katika mfano huu “deriverlance” na “exoticism” ni nini? Natumaini anamaanisha “deliverance” na “exorcism.” Maskini mwalimu, eti hawezi kuona tofauti hapa!
Hadi hapa, naomba uhisi kitu. Kuna kitu. Kuna namna ya mdodoro wa kielimu. Kuna ujinga. Lakini shida si jambo hili tu. Kimaadili, tunastaajabu heshima na adabu vinavyomong’oka. Watoto na vijana wetu wanakazana kuyatoa mambo ya vyumbani hadharani.
Wasanii wetu wengi wakiimba wanaimba matusi na wakicheza wananengua viuno pasipo soni. Kifupi, wasanii wetu wanauziwa propaganda zozote hata zile za kuwadhalilisha wenyewe kijinsia na wanazinunua kwa rejareja. Hii maana yake akili yao imekaa henamu sana hawawezi kujitegemea katika kufikiri. Kwa maneno mengine akili ya kuambiwa hawachanganyi na zao.
Wasanii wengi wamekoma kuwa vioo vya jamii. Kwa kisa hicho, wamekuwa rahisi kupokea hata propaganda za ushoga na usagaji. Katika hili, hali ya kustaajabisha ni hiyo kwamba mtoto wa kiume anaweza kukubali kutumika kama mwanamke na mtoto wa kike kujigeuza kidume. Kwa nini mambo yanakwenda hivi? Zifuatazo ni nadharia zangu tete kuelezea mkasa huo.
Mzee wenu Pd. Titus Amigu.
Copy & Paste.