Mama Rwakatare aichongea JamiiForums

Mama Rwakatare aichongea JamiiForums

Washindwe na walegee!!!!

Serikali ilishashindwa kwa hili na jana tu waziri muhusika alisema kwamba JF is next level that got registration outside the country...it's beyond their neck!!
 
Tatizo la watawala wetu ni kutokusoma alama za nyakati na kupenda sana sifa na kutukuzwa kama miungu watu. Kukosolewa kwao ni hapana hata kama wanafanya mambo ya ovyo kabisa. Kwa nini kama ni kiongozi mkereketwa asimamie madaktari kuongezwa posho na kuboreshwa mazingira ya kazi zao ili wawahudumie watanzania kwa ubora zaidi? Kwa nini asisimame kidete kupinga uporaji wa rasilimali mbalimbali za Watanzania kama Wanyama kuibwa na kusafirishwa uarabuni kwa kutumia viwanja vyetu vya ndege? Uporaji wa madini kwa kisingizio cha mikataba mibovu? Uporaji wa NBC? Uporaji wa nyumba za serikali? Uporaji TANESCO kwa kutumia (Richmond/Dowans/Symbion, IPTL, SONGAS) TANGOLD, MEREMETA, TCRA kusomesha watumishi watatu (3) kwa zaidi ya billion 2.00.

Uongozi unaotanguliza ubinafsi na kukandamiza watu hauna nafasi tena. JF itaendelea kuweka kama sauti ya umma.
 
Nashindwa kuelewa kinacho mkwaza huyu Mbunge nini kwani

JF inataratibu zake na zinafuatwa mfano Member anaye toa lugha ya Uchochezi, Matusi, Ukabila, Udini anapigwa ban sasa tatizo ni nini ingelikuwa adhabu hazitolewi hapo ingelionekana JF inashabikia haya mambo

Huyu mama tatizo lake ni nini hasa ELIMU, DINI, SIASA za mlengo aliko UWEZO wa kuelewa mambo au nini hasa ?????????/


Kuna mtu ana CV yake? Itasaidia sana kuelewa asili ya madai yake.
 
Watu wengine bana sasa wewe Mbunge kule MK unatafuta nini jamani? Yaani ujiuguze kisha upige kelele kuwa unaungua!!!
 
Wabunge kujadili vitu kama hivi, ndio wanadai posho za 330,000/= ???:A S 13::A S 13:
Hiyo posho hawajui kwamba inatokana na kodi wanazolipa wananchi??...na kwamba wao ni watumishi wetu tuliyowachagua wakatuwakilishe? Hivi hawafahamu kwamba, kiongozi bora ni yule anayekubali kukosolewa?

Kuna dalili zote za kuuziwa mbuzi ndani ya gunia hapa. Inaelekea tumepoteza muda wetu kupanga foleni kupiga kura.
 
Kuhusu huyo mama na uchungaji wake ulivyo soma Ezekiel 34, utapata jibu

Huyu kajificha tu kwenye uchungaji, by the way anawalisha upepo waumini wake soma 1Timothy3:1-16 Hapo kila kitu kimeandikwa kwa ufasaha.
 
Maoni yanayotolewa humu na members hayana uhusiano wowote na wamiliki wa JF,na kulingana na ibara ya 18 kwamba kila mtanzania ana uhuru wa kutoa maoni ili mradi asivunje sheria za nchi,kusema maovu ya serikali na viongozi wake si kuvunja sheria,kama rais anatumia kodi zetu bure kwanin tusimwambie? Ni kodi zangu kila mwezi nakatwa(direct) na indirect nikipata bidhaa,mangura engineer ni mali ya walipa kodi kama amefilisi kwanin asisemwe?
 
kwa kadri siku sinavyoenda kama jamii haitasimama basi tutaamka siku moja na kukuta JF imefungwa kwani serikali inaweza kuanza kuwasiliana na makampuni makubwa yenye teknolojia kubwa duniani hili kuhujumu mtandao unaoleta mabadiliko na kufumbua watu macho wa jamii forum.

Nini kifanyike dhidi ya hujuma za JF?

Labda waifungie internet.....
 
JF inataratibu zake na zinafuatwa mfano Member anaye toa lugha ya Uchochezi, Matusi, Ukabila, Udini anapigwa ban sasa tatizo ni nini ingelikuwa adhabu hazitolewi hapo ingelionekana JF inashabikia haya mambo

Huyu mama tatizo lake ni nini hasa ELIMU, DINI, SIASA za mlengo aliko UWEZO wa kuelewa mambo au nini hasa ?????????/
Si members tu ambao ni tatizo, hii ni ile wanayoita katika lugha ya kikoloni "wake up call".I saw it coming!
Vilevile JF ifahamu sasa kuwa ina maadui wengi na wa aina mbalimbali;watu wa dini, wanasiasa,viongozi n.k .Hawa watu wakiungana kwa ajili ya kuihujumu JF itakuwaje?!
JF inabidi kubadilika na ijirekebishe, najuwa mabadiliko ni vigumu kukubalika lakini yanahitajika!
 
kweli kabisa, wanafanya biashara, wanafunguwa mashule kwa majina ya watakatifu na kuyahusisha na makanisa, yote kukwepa kodi tu. Hizi sheria zifanyiwe mabadiliko. Vyombo vyote vya dini vijiendeshe bila kutegemea misamaha ya kodi wala ruzuku za serikalini. Wajanja wachache wanatumia dini kuwanyonya wengine. Huo ndio ukweli.
nadhani umefika wakati wa huyu mama mdhaifu g. Lwakatare kuiomba msamaha jf, nasi tutamsamehe. La sivyo tutamchachafya mpaka kile kiti cha kupewa kiwe cha moto!
 
wakuu msiwe na hofu.Mh Kikwete hawezi kuruhusu huu mtandao ufungwe!! Amini usiamini habari ndio hiyo! Kama kuna wanaofikiri JF ni adui wa Mh Kikwete wameingia choo cha kike! Hutaki piga mbizi!
 
Mkuu Max/invisible tupe muongozo kuhusu hili tishio..
Mwongozo gani mkuu? Wao wamejitoa sana kizalendo.wao hawatungi sheria sasa ni wajibu wa sisi tunaofaidika ku play our part! How? Just be smart as JF member kwa jinsi tunavyoutumia mtandao huu ili kupunguza areas for concentration waweze kupata tym ya kubuni mambo mapya zaidi.
 
Hapa Mweshimiwa Kitwanga katumia utahalamu wake wa ICT anajua mambo haya vizuri sana. Labda cha kumsaidia mama Dr. Rwakatale kama vile yeye anavyo hubiri maadili katika dini na hivyo hivyo ajitahidi sana, watu wengine wana-hubiri huwajibikaji kwa njia nyingine.

Hii ndiyo challenge iliyopo mbele yetu. Hizi tovuti za mtindo huu haziko Tanzania tu hata kabla hatujaenda twitter, facebook nk kwa ulimwengu wa sasa kila nchi ina mahala pa kupumulia.Hivi hajasoma kama jamiiforum watu walikuwa wanatafuta kero za wananchi kupitiamtandao huu (mimi naona hili ni jambo zuri).

Mbona sasa hayo mazuri hajayasema?
Kwanza hawa ndio wawakilishi wa wananchi inasaidia hatawatawala kujua wananchi wao wanawafikiliaje kama ni kujirekebishaunajirekebisha. Kama kuna jambo ambalo linaonekana kukera mtu aeleze.

Na pia nafikiri katika mijadala ya mitandaoni mama Dr.Rwakatale anaweza kujitetea kama yeye au kutumia mtu yeyote Yule kutoaufafanuzi pale anapoona upotoshwaji. Tanzania hatuwezi kuwa kisiwa katika maswala ya habari. Sasa hivi karibia watawala wote wako mitandaoni. Hatuwezi kurudi miaka ya 47.

Sasa hivi tumetengeneza mitandao, imekuwepo na tunasonga mbele, au hakumbuki msemo huu wa chama. Haya ndio maendeleo yaliyofikiwa na chama kuelekea kuazimisha kuzaliwa kwake. Sheria zitakuwepo lakini pia ukweli utabaki ukweli na utasemwana kukubarika bila kificho.

Wengi wetu hapa mitandaoni tunajifunza mengi sana. Na nafikiri hata madhambi ya uvunguni ambayo tulikuwa hatuyajui angalautunayajua japo kidogo.
Miaka si mingi ijayo mitandao itatumiwa na waheshimiwa wabungeeither kufanya kampeni au kuongea na wananchi wao.

Sasa mama Dr. Rwakatarewakati watu wanaimba mtandao mpaka vijijini kwa ajiri ya maendeleo naonaakipewa uwaziri wa mawasiliano atahakikisha hakuna kinachoendelea.

Hata nina uhakikamama Dr. Rwakatare muda si mrefu provided yuko bungeni ataomba baadhi yawatumia mitandao wampambe hili either aweze kupata jimbo kupitia njia yakawaida au viti maalumu.
 
mama rwakatare kakosa kitu cha maana cha kuuliza, yaani miaka yote yuko kimya afu leo kaibuka na swali la aina hii. bora viti maalum vifutwe, kawaaibisha wenzake sana, afu analipwa 330,000 kwa siku, aibu.
 
Napendekeza siku tukiamka tukakuta imefungwa,tuingie facebook kwenye page ya jamiiforums apo ndo tutadiscus cha kufanya,hawa watu wana akili fupi hawashindwi kufunga...ila mwanajf mwenzetu naibu wazr atalisimamia maana tuko pamoja.
 
Vijana wangu waendeshaji wa JF.........najua mlishachukua tahadhari.............lakini hii ni kama reminder.............kuweni waangalifu sana huko mnakopita...msije mkamwagiwa tindikali..........au msije "mka-Mwakyembeiwa".........i don't trust these Rwakatare + CCM criminals..........
 
​kama wakifungia bado inaweza kujiend​esha kupitia proxy system
 
Back
Top Bottom