Mama Magufuli aaga rasmi shule ya Mbuyuni

Mama Magufuli aaga rasmi shule ya Mbuyuni

Kwanini ameacha kufundisha,hawezi kuwa mke wa rais na kuwa mwalimu,?

Au anaenda kuanzisha WAMA nyingine.
 
Kumbe Mama ni left hand! What a coincidence!
 
Sijui why uwezo wa kufikiri wa members wengi humu ni mdogo,?

Yaani wengine wameshaconclude kabisa kuwa hizo simu za hao watoto ni zao!
Kujiongeza kufikiri Mara mbili hawataki
 
Haya wale UKAWA mnaodharau ualimu semeni sasa

1.Nyerere na Maria NYERERE wote walikuwa walimu wakaingia IKulu
2.Mwinyi alikuwa mwalimu na mkuu wa chuo cha ualimu Zanzibar na mkewe alikuwa mwalimu chuo cha Lugha ZA kigeni Zanzibar wakaingia ikulu
3.Kikwete alikuwa mwalimu wa Siasa JESHINI NA mkewe Salma alikuwa mwalimu wakaingia Ikulu
4.Magufuli alikuwa Mwalimu na mkewe MWALIMU wameingia ikulu

Katika maraisi watano wa nchi hii wanne wote walikuwa walimu.Walimu wana nyota ya IKULU.

Na Tanzania wenyewe hiyo iko wapi kiuchumi duniani?
 
Hao watoto dhahiri inaonyesha wamepewa Simu na walimu/wageni waalikwa wawasaidie kupiga picha. Labda muwalaumu kujua kupiga picha kwa kutumia smartphone wakiwa katika umri huo.
 
Haya wale UKAWA mnaodharau ualimu semeni sasa

1.Nyerere na Maria NYERERE wote walikuwa walimu wakaingia IKulu
2.Mwinyi alikuwa mwalimu na mkuu wa chuo cha ualimu Zanzibar na mkewe alikuwa mwalimu chuo cha Lugha ZA kigeni Zanzibar wakaingia ikulu
3.Kikwete alikuwa mwalimu wa Siasa JESHINI NA mkewe Salma alikuwa mwalimu wakaingia Ikulu
4.Magufuli alikuwa Mwalimu na mkewe MWALIMU wameingia ikulu

Katika maraisi watano wa nchi hii wanne wote walikuwa walimu.Walimu wana nyota ya IKULU.
mama kakimbia vumbi .

swissme
 
Hao watoto walio na smartphone ni watoto wa Kiislamu(ANGALIA MAVAZI YAO).Waislamu ni wakali kwa kushinikiza mambo.Angalia hata walivyoshinikiza hiyo uniform ya shule wavae kihijabu tofauti na wanafunzi wengine.Watakuwa wameshinikiza kuwa watoto wao lazima wawe na smartphone shuleni.Mwalimu atafanyeje? Na viboko vilishafutwa mashuleni?

Shuleni wakristo wengi hawataki watoto wao waende shule na simu ili wa concentrate kwenye masomo.Hilo la simu ni jipu ambalo waislamu wenyewe ndio wanatakiwa walitumbue.
Wewe ni mwehu
 
Naona msaka uwaziri ndg Paul makonda ameitumia fursa ipasavyo. Jamaa kwa kujikomba ni ni noma. Mara afunge kamba za viatu, mara ambebe mtoto wa mfalme, mara amkumbatie makamu, mara.....daaah!! Yataka moyo wa kiwendawazimu kwakweli..
 
Hii shule itakua inautapiamlo wa maadili..
Watoto wa shule ya msingi wanakuja na smartphones shuleni..??
Kweli elimu bure inatekelezeka...

Tena mtoa mada ukaweka mapicha kamasifa..NINI kimekufanya huiondoe hiyo ya hao mabint na smartphone zao tena saa za masomo..??/
 
Mke wa rais awaahidi walimu nchini kumkumbusha rais matatizo yao.
yaukweli17.jpg



Mke wa rais Mama Janeth Magufuli amewaahidi walimu nchini kuwa atahakikisha anamkumbusha rais changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo walimu ili ziweze kutatuliwa kwa wakati kwani anazifahamu na amezipitia.

Mama Janeth ametoa ahadi hiyo jijini Dar es Salaam alipokwenda kuwaaga wanafunzi na walimu wa shule ya Mbuyuni ambayo mbali na kufundisha kwa miaka 17 lakini pia alikuwa mwanafunzi wa shule hiyo ambapo ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa wazazi na walezi nchini kutosahau majukumu yao kisa dhana ya elimu bure.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo Bi Doroth Malechela akatumia ipasavyo ujio wa mke wa rais kumuomba afikishe kilio cha walimu nchini kwani wanakabiliwa na matatizo lukuki ikiwemo mazingira magumu ya kazi, fedha za likizo kutokupatikana kwa wakati kutopanda madaraja kwa wakati na wakipanda upatikanaji wa stahiki zao imekuwa matatizo.

Katika risala yao wanafunzi wa shule ya msingi Mbuyuni mbali na kumweleza mke huyo wa rais mapungufu yaliyojitokeza pindi tu alipoondoka wamemuomba asiwasahau kama wanavyoeleza.

Chanzo: http://www.itv.co.tz/news/local/181...imu_nchini_kumkumbusha_rais_matatizo_yao.html
 
Mama yetu,, First lady Ameyasema hayo pindi alipoitembelea shule ya Msingi mbuyuni kuwaaga wanafunzi wake na walimu wenzake.. ameahidi atamkumbusha Mh Rais changamoto za walimu kwani zinafanana nchi nzima.Na anazifahamu..
Viva Mama yetu, Walimu tupo Nyuma yako usituangushe...
 
Matatizo ya walimu ni wao wenyewe sio mtu mwingine anaweza yabadilisha
 
Nimshauri tu kama yumo humu akalifanyie kazi. Aanzishe NGO kama za watangulizi wake ya kuwajengea walimu nyumba karibu na mashule ili kuwapunguzia adha za wenye nyumba. Hili litamtofautisha na wale wenye WAMA na fursa sawa kwa wote kwani ataishi kwenye mioyo ya watanzania milele. Na hili linawezeka likiratibiwa na kusimamiwa vema. Anipm kwa msisitizo.
 
Mke wa Rais Magufuli ameyasema hayo maneno leo alipokua anawaanga wanafunzi wake na wafanyakazi wenzake (walimu). Ikumbukwe bi Janet kitaaluma ni mwalimu,na ameifanya hiyo kazi zaidi ya miaka kumi, aidha mama huyo amesisitiza kumkumbusha mume wake kutatua changamoto za walimu.
 
Wakumbuke Mama na wasikilize...maana unaweza kuwakumbuka ila usiwasikilize.Mwanzo mzuri,hatimaye walimu wataona nuru maana wapo kwenye giza tena totoro.
 
Back
Top Bottom