Mama Kilango v/s Sophia Simba ndani ya uchaguzi wa UWT...

HIYO SIYO KWELI; NDANI YA CCM wanataka kuondoa Ubunge wa viti Maalumu toka UWT kwahiyo sidhani kama Kilango ataacha Jimbo anende kwenye JUMUIA...

Soma Habari Chini...

[h=2]Sophia Simba awashukia wabunge viti maalumu[/h]JUMATANO, 14 MACHI 2012 07:34 NA DEBORA SANJA, DODOMA.

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT), Sophia Simba, amedai kushangazwa na baadhi ya wabunge wa viti maalumu kumtuhumu kuwa ni yeye aliyeanzisha suala la kuwapo kwa ukomo wa ubunge wa viti maalumu vya CCM.
Kauli hiyo aliitoa mjini hapa jana, wakati akifungua semina elekezi kwa wenyeviti wa UWT wa mikoa na wilaya za Tanzania Bara na Visiwani.

Alisema suala la kuwapo kwa ukomo wa ubunge wa viti maalumu hakulianzisha yeye ndani ya UWT, lakini alisema si vibaya likawepo.

"Ni kweli kuwa mimi ni muumini wa uwapo kwa ukomo wa ubunge wa viti maalumu lakini siye niliyeanzisha.

"Suala hili lilikuwapo tangu mwaka 1995 na lilianzishwa na waasisi wa UWT kwa nia njema tu, akiwamo Anna Abdalah, Anna Komu na Thabita Siwale.

"Lakini nashangaa baadhi ya wabunge wa viti maalumu wakipita mikoani wanalalamika wakisema kuwa mimi ndiye niliyelianzisha suala hili la ukomo wa ubunge wa viti maalumu.

"Kauli hizi za wabunge zinanishangaza kwa kuwa si ukweli kuwa mimi ndiye niliyelipeleka suala la ukomo wa ubunge wa viti maalumu katika Baraza Kuu la UWT, wakati ukweli unajulikana," alisema Simba.

Alisema wapo baadhi ya wabunge wa viti maalumu waliopo sasa anawafahamu awali walikuwa wanataka kuwapo na ukomo wa ubunge huo kabla hawajawa wabunge, lakini kwa sasa wanapinga.

Alisema pamoja na malalamiko hayo bado ukomo ni muhimu, kwa kuwa unawezesha wengine nao kushika nafasi za ubunge kupitia viti maalumu.

Alisema lengo la kupendekeza kuwapo kwa ukomo wa kugombea ubunge wa viti maalumu lilikuwa ni kuwajengea uwezo wanawake ili nao baada ya muda fulani waweze kusimama wenyewe kugombea.

"Kama wewe umesoma umefika darasa la saba bado tu unang'ang'ania hapo hutaki kutoka, hao wa darasa la sita waende wapi sasa," alisema Simba.

Aidha, aliwataka wanawake hao kulijadili suala hilo la ukomo wa viti maalumu kwa makini na kutoa uamuzi unaofaa.

Aliwataka wanawake nchini kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika chaguzi za chama na jumuiya zake.

Mbali na kujitokeza kugombea nafasi hizo, aliwataka kujitokeza kutoa maoni kuhusiana na uundwaji wa Katiba mpya.

"Nia ni kuhakikisha mambo yote muhimu ambayo mwanamke anastahili kulindwa katika Katiba yanapata nafasi ya kuingizwa kwa manufaa ya akina mama wa Tanzania," alisema Simba.
 
Zul, ni kweli mimi niliishawahi kutangaza nia ya kugombea Uenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa, na tena azma yangu hii ni ya siku nyingi na niliishawaambia wengi walio karibu yangu, na hii ni azma yangu binafsi na wala haina shinikizo hata ushawishi wa mtu yeyote yule! Sijawahi kuwa na mazungumzo ya faragha na mtu yeyote yule anayetajwa kuwania Urais 2015 na mimi nadhani muda bado sana kuchagua ni nani nitakayemuunga mkono. wanaCCM wenzangu wenye uwezo wa kuwania Urais ni wengi sana tu na ni mapema mno kuchagua wa kumuunga mkono, vipi kama mimi mwenyewe nikiamua kugombea Urais? Sasa kwa nini ufikirie kuwa ninatumwa na mtu yeyote yule?!

sina mapenzi na CCM lakini kuna watu ndani ya CCM naamini walipotea njia sababu wana mtizamo usiofanana na u-CCM. wewe nakuona ni mmoja wapo nadhani hukupaswa kuwa huko sababu sidhani kama wanakuelewa na ndio maana Hawa Ghasia hakuona tabu kukuchambua wakati ulikuwa uko sahihi kabisa. Anyway labda itafika wakati ambapo CCM itaongozwa na watu kama wewe, Deo Filikunjombe na Januari Makamba ili muibadilishe maana kwa sasa chama chenu kimeoza. Ni mtazamo wangu tu huu
 
Kigwangala mbona unaoneka umri wako bado mdogo kuwa mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi?. Mimi nilijua Jumuia hii ni ya wazee, kama ilivyokuwa kwa walipita akina, Gibons Mwaikambo, Idd Simba and Mhina mbao nawajua kwa umri wangu. Kumbe hamzingatii umri ni mvurugano tu. Sitashangaa mzee Ngombale akichukua form ya UVCCM akichuana na Beno Malisa LOL!

Swali la msingi sana hili.
 
Zul, ni kweli mimi niliishawahi kutangaza nia ya kugombea Uenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa, na tena azma yangu hii ni ya siku nyingi na niliishawaambia wengi walio karibu yangu, na hii ni azma yangu binafsi na wala haina shinikizo hata ushawishi wa mtu yeyote yule! Sijawahi kuwa na mazungumzo ya faragha na mtu yeyote yule anayetajwa kuwania Urais 2015 na mimi nadhani muda bado sana kuchagua ni nani nitakayemuunga mkono. wanaCCM wenzangu wenye uwezo wa kuwania Urais ni wengi sana tu na ni mapema mno kuchagua wa kumuunga mkono, vipi kama mimi mwenyewe nikiamua kugombea Urais? Sasa kwa nini ufikirie kuwa ninatumwa na mtu yeyote yule?!

Duh Mkuu kihistoria huwa naona kama hii nafasi inakamatwa na wazeee wazee vile; naona kama wewe bado kijana sana kugombea hiyo nafasi japokuwa sijui Umoja wa Wazazi wa CCM wanachama wake ni wa aina gani.
 
Kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama ni haki ya wanachama lakini ni vizuri muhusika akajipima kwanza kama anafaa badala ya kuongozwa na hisia na tamaa ya madaraka! Kwa kumlinganisha Sophia Simba na Anna Kilango,namuona Sophia ni bora kwa vigezo vyote. Kilango hafai kabisa,abakie ndani amtunze mzee wake! Mwalimu Nyerere alituepusha na scandal kubwa kwasababu Malecela angeukwaa urais na huyu mama akawa first lady tungemkoma!
 
Duh Mkuu kihistoria huwa naona kama hii nafasi inakamatwa na wazeee wazee vile; naona kama wewe bado kijana sana kugombea hiyo nafasi japokuwa sijui Umoja wa Wazazi wa CCM wanachama wake ni wa aina gani.
.
Kimsingi mtu yoyote mwenye umri wa miaka 18 na kuendelea anaruhusiwa kujiunga na Jumuiya ya Wazazi ya CCM. Kwa hiyo mh.dkt yuko sahihi kutangaza nia ya kugombea uongozi katika jumuiya hiyo kwa lengo la kutimiza haki yake ya kuchagua na kuchaguliwa.
 
Zul, ni kweli mimi niliishawahi kutangaza nia ya kugombea Uenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa, na tena azma yangu hii ni ya siku nyingi na niliishawaambia wengi walio karibu yangu, na hii ni azma yangu binafsi na wala haina shinikizo hata ushawishi wa mtu yeyote yule! Sijawahi kuwa na mazungumzo ya faragha na mtu yeyote yule anayetajwa kuwania Urais 2015 na mimi nadhani muda bado sana kuchagua ni nani nitakayemuunga mkono. wanaCCM wenzangu wenye uwezo wa kuwania Urais ni wengi sana tu na ni mapema mno kuchagua wa kumuunga mkono, vipi kama mimi mwenyewe nikiamua kugombea Urais? Sasa kwa nini ufikirie kuwa ninatumwa na mtu yeyote yule?!

Ingawa mimi siipendi kabisa CCM kwasababu ya unafiki wao. Lakini tuwa support hawa Wabunge vijana kwani ndiyo wanaoweza kuleta mabadiliko ndani ya CCM ambayo ni faidi kwetu Watanzania. Watu kama Hawa Ghasia ni wa kupuuzwa kwani tunafahamu ubunge alipata kwa kubebwa (alishika nafasia ya 2, 2005) na huo Uwaziri apewa kama zawadi.
Wabunge vijana kama January Makamba, Hamis Kigwangalah, Alfaxad Lugola, Deo Filikunjombe etc ingawa wako CCM lakini at least they can stand and be accounted kwa kuwawatea wananchi, ingawa pia wapo wabunge Vijana ndani ya CCM ambao pia ni bogus kama Wazee mfano Mwigulu Nchemba, George Simbachawane, Peter Serukamba etc.

Go go goo Dr. Hamis Kigwangalah you have my support
 
Ingawa mimi siipendi kabisa CCM kwasababu ya unafiki wao. Lakini tuwa support hawa Wabunge vijana kwani ndiyo wanaoweza kuleta mabadiliko ndani ya CCM ambayo ni faidi kwetu Watanzania. Watu kama Hawa Ghasia ni wa kupuuzwa kwani tunafahamu ubunge alipata kwa kubebwa (alishika nafasia ya 2, 2005) na huo Uwaziri apewa kama zawadi.
Wabunge vijana kama January Makamba, Hamis Kigwangalah, Alfaxad Lugola, Deo Filikunjombe etc ingawa wako CCM lakini at least they can stand and be accounted kwa kuwawatea wananchi, ingawa pia wapo wabunge Vijana ndani ya CCM ambao pia ni bogus kama Wazee mfano Mwigulu Nchemba, George Simbachawane, Peter Serukamba etc.

Go go goo Dr. Hamis Kigwangalah you have my support
Kigwangala gombea huo uenyekiti kwa vile ubunge hupati tena
 
Daktari jaribu kutafari uwepo wako ndani CCM,nadhani unao ubora sahihi wa kujiunga na chama makini CDM,
Uwezo wako wa kutetea wanyonge unakubalika,
 
Kama sio kesho basi kesho kutwa ccm itaweza kubadilika na hili litawezekana tu endapo viongozi wake wataweza kuzisoma alama za nyakati. Kwa kulitambua hili wabunge wake baadhi wameamua kwenda nao tofauti kabisa. Shida kubwa ni ukiwa muwazi basi lazima uambiwe ww ni wa kundi fulani inategemeana na uwazi wako huo umeegemea upande gani.
 
Mimi siamini sana katika factor ya umri (mkubwa ama mdogo) kwenye uongozi. Mimi naamini zaidi kwenye uwezo wa kiuongozi. Tunategemea viongozi wenye umri mdogo wawe wabunifu sana kuliko wale wazee, lakini mara nyingi tumeona matokeo kinyume na matarajio haya. Tumeona pia mafanikio makubwa yakiletwa na viongozi vijana sehemu mbalimbali, ambako viongozi wazee wameshindwa. Mfano wa Joseph Kabila Kabange anavyoimarisha demokrasia kule DRC na pia anavyojenga mabarabara na viwanja vya ndege sasa hivi kule nchini kwake, anavyojenga mahospitali na anavyotetea nchi yake kufaidika na madini na rasmlimali - haya yaliwashinda baba zake akina Kabila Sr na Mobutu Sseseseko Kukungwendu wa Zabanga (aliyekuja kufa kidhalili kabisa), tunaona mambo makubwa aliyoyafanya Paul Kagame wa Rwanda. Tunaona mafanikio makubwa ya kuleta mabadiliko ya mahusiano kati ya watu weusi na weupe kule Marekani thru non-violence movements ya kijana Dr. Martin Luther King Jr, tunaweza pia kujifunza kutoka kwa akina Mwl. Nyerere na wenzake na makubwa waliyoyafanya kwa nchi yetu na Dunia kwa ujumla...and the list goes on! Tujiulize hawa wote walikuwa wazee?

Ukiwa muumini wa mabadiliko ya ukweli basi kwa vyovyote vile utatakiwa kuniunga mkono mimi na wanamapinduzi wengine wanaojitokeza kuomba nafasi za uongozi wa chama chetu, na kisha utanipa mawazo yako bila kujali ni kijana ama ni mzee kiasi gani. Sina nia nyingine yoyote ile zaidi ya kutaka kuingia kwenye vikao vya juu vya maamuzi ya chama changu ili kushawishi mabadiliko kutokea. Chama Cha Mapinduzi kinahitaji wanamapinduzi kama mimi kwa sasa, kwanza kwa ajili ya succession planning na pili kwa ajili ya nguvu mpya ya mabadiliko wanayoyahitaji waTanzania wa sasa. Kisipoamka na kuchukua nguvu mpya on board, kitayumba na hii itapelekea Taifa pia kuyumba. Tulio na nia nzuri na nchi yetu, na chama chetu tunachukua hatua kwa kuingia ndani na kushawishi mabadiliko! Wenzetu mjue kuwa tunachukua risk kubwa sana na mnachoweza kufanya si kingine tu bali kutuunga mkono na zaidi kututia moyo.

Najipanga kuomba kibali cha kugombea na nina imani kabisa chama changu kitanipa fursa hiyo ili nifike mbele ya wanachama wenzangu wa jumuiya hiyo kutafuta ushindi na ninaamini wapiga kura watanielewa na kunipa kura za ushindi ili tufanye kazi pamoja.
 
Dr. Hamisi Kigwangalla, MD, MPH, MBA
Mabadiliko ya kweli yataletwa na sisi...!:A S-frusty2:
:A S 13::A S 13:
progress.gif
 
Mimi siamini sana katika factor ya umri (mkubwa ama mdogo) kwenye uongozi. Mimi naamini zaidi kwenye uwezo wa kiuongozi. Tunategemea viongozi wenye umri mdogo wawe wabunifu sana kuliko wale wazee, lakini mara nyingi tumeona matokeo kinyume na matarajio haya. Tumeona pia mafanikio makubwa yakiletwa na viongozi vijana sehemu mbalimbali, ambako viongozi wazee wameshindwa. Mfano wa Joseph Kabila Kabange anavyoimarisha demokrasia kule DRC na pia anavyojenga mabarabara na viwanja vya ndege sasa hivi kule nchini kwake, anavyojenga mahospitali na anavyotetea nchi yake kufaidika na madini na rasmlimali - haya yaliwashinda baba zake akina Kabila Sr na Mobutu Sseseseko Kukungwendu wa Zabanga (aliyekuja kufa kidhalili kabisa), tunaona mambo makubwa aliyoyafanya Paul Kagame wa Rwanda. Tunaona mafanikio makubwa ya kuleta mabadiliko ya mahusiano kati ya watu weusi na weupe kule Marekani thru non-violence movements ya kijana Dr. Martin Luther King Jr, tunaweza pia kujifunza kutoka kwa akina Mwl. Nyerere na wenzake na makubwa waliyoyafanya kwa nchi yetu na Dunia kwa ujumla...and the list goes on! Tujiulize hawa wote walikuwa wazee?

Ukiwa muumini wa mabadiliko ya ukweli basi kwa vyovyote vile utatakiwa kuniunga mkono mimi na wanamapinduzi wengine wanaojitokeza kuomba nafasi za uongozi wa chama chetu, na kisha utanipa mawazo yako bila kujali ni kijana ama ni mzee kiasi gani. Sina nia nyingine yoyote ile zaidi ya kutaka kuingia kwenye vikao vya juu vya maamuzi ya chama changu ili kushawishi mabadiliko kutokea. Chama Cha Mapinduzi kinahitaji wanamapinduzi kama mimi kwa sasa, kwanza kwa ajili ya succession planning na pili kwa ajili ya nguvu mpya ya mabadiliko wanayoyahitaji waTanzania wa sasa. Kisipoamka na kuchukua nguvu mpya on board, kitayumba na hii itapelekea Taifa pia kuyumba. Tulio na nia nzuri na nchi yetu, na chama chetu tunachukua hatua kwa kuingia ndani na kushawishi mabadiliko! Wenzetu mjue kuwa tunachukua risk kubwa sana na mnachoweza kufanya si kingine tu bali kutuunga mkono na zaidi kututia moyo.

Najipanga kuomba kibali cha kugombea na nina imani kabisa chama changu kitanipa fursa hiyo ili nifike mbele ya wanachama wenzangu wa jumuiya hiyo kutafuta ushindi na ninaamini wapiga kura watanielewa na kunipa kura za ushindi ili tufanye kazi pamoja.

Kwa comment zako, CCM haikufai, sema bahati mbaya hata upinzani hakuna TZ, kama ungenipa nafasi nikushauri ningekushauri urudi kwenye fani yako.
 
Ingawa mimi siipendi kabisa CCM kwasababu ya unafiki wao. Lakini tuwa support hawa Wabunge vijana kwani ndiyo wanaoweza kuleta mabadiliko ndani ya CCM ambayo ni faidi kwetu Watanzania. Watu kama Hawa Ghasia ni wa kupuuzwa kwani tunafahamu ubunge alipata kwa kubebwa (alishika nafasia ya 2, 2005) na huo Uwaziri apewa kama zawadi.
Wabunge vijana kama January Makamba, Hamis Kigwangalah, Alfaxad Lugola, Deo Filikunjombe etc ingawa wako CCM lakini at least they can stand and be accounted kwa kuwawatea wananchi, ingawa pia wapo wabunge Vijana ndani ya CCM ambao pia ni bogus kama Wazee mfano Mwigulu Nchemba, George Simbachawane, Peter Serukamba etc.

Go go goo Dr. Hamis Kigwangalah you have my support


Simfahamu vizuri huyu Daktari............. Lakini inaelekea anajisia sana. Au alishawahi kuwa best student somewhere!!!
 
Nakubaliana na wewe katika hili, lakini nakuhakikishia kwa hali ilivyo ndani ya chama chenu (ingawa mimi si mwanachama wa chama chochote) hiyo risk mliyochukua NI ZAIDI YA RISK..na zaidi sana kupabadilisha humo, kwa nature ya waliomo na waliweka mizizi ya uozo, inachukua zaidi idadi ya miaka aliyotumia Nyerere kuingia kwenye siasa hadi kupatikana kwa Uhuru mwaka 1961! kwa maneno mengine, kuibadili Tanzania yetu ili iondokanae na uozo huo sio lazima kuwa ndani ya CCM.

Sikukatishi tamaa, wewe na walio wa kariba yako kama kina J..Makamba na wengineo, lakin ninachomaanisha ni kuwa ikifikia mahali nia zako au zenu zilizo njema zinauliwa kwa mbinu zote (kama hayo uliyofanyiwa na kina Ghasia, na ule mkwala uliopigwa kuhusu yale maswala ya mgodini), si dhambi kutafuta njia mbadala, kwani naamini siku zote anayesimama katika ukweli atashinda, hata kama kiwiliwili chake hakitashuhudia ushindi huo-lakini Roho yake itaushuhudia! (umetoa mfano wa Dr. Martin Luther King)
Mimi siamini sana katika factor ya umri (mkubwa ama mdogo) kwenye uongozi. Mimi naamini zaidi kwenye uwezo wa kiuongozi. Tunategemea viongozi wenye umri mdogo wawe wabunifu sana kuliko wale wazee, lakini mara nyingi tumeona matokeo kinyume na matarajio haya. Tumeona pia mafanikio makubwa yakiletwa na viongozi vijana sehemu mbalimbali, ambako viongozi wazee wameshindwa. Mfano wa Joseph Kabila Kabange anavyoimarisha demokrasia kule DRC na pia anavyojenga mabarabara na viwanja vya ndege sasa hivi kule nchini kwake, anavyojenga mahospitali na anavyotetea nchi yake kufaidika na madini na rasmlimali - haya yaliwashinda baba zake akina Kabila Sr na Mobutu Sseseseko Kukungwendu wa Zabanga (aliyekuja kufa kidhalili kabisa), tunaona mambo makubwa aliyoyafanya Paul Kagame wa Rwanda. Tunaona mafanikio makubwa ya kuleta mabadiliko ya mahusiano kati ya watu weusi na weupe kule Marekani thru non-violence movements ya kijana Dr. Martin Luther King Jr, tunaweza pia kujifunza kutoka kwa akina Mwl. Nyerere na wenzake na makubwa waliyoyafanya kwa nchi yetu na Dunia kwa ujumla...and the list goes on! Tujiulize hawa wote walikuwa wazee?

Ukiwa muumini wa mabadiliko ya ukweli basi kwa vyovyote vile utatakiwa kuniunga mkono mimi na wanamapinduzi wengine wanaojitokeza kuomba nafasi za uongozi wa chama chetu, na kisha utanipa mawazo yako bila kujali ni kijana ama ni mzee kiasi gani. Sina nia nyingine yoyote ile zaidi ya kutaka kuingia kwenye vikao vya juu vya maamuzi ya chama changu ili kushawishi mabadiliko kutokea. Chama Cha Mapinduzi kinahitaji wanamapinduzi kama mimi kwa sasa, kwanza kwa ajili ya succession planning na pili kwa ajili ya nguvu mpya ya mabadiliko wanayoyahitaji waTanzania wa sasa. Kisipoamka na kuchukua nguvu mpya on board, kitayumba na hii itapelekea Taifa pia kuyumba. Tulio na nia nzuri na nchi yetu, na chama chetu tunachukua hatua kwa kuingia ndani na kushawishi mabadiliko! Wenzetu mjue kuwa tunachukua risk kubwa sana na mnachoweza kufanya si kingine tu bali kutuunga mkono na zaidi kututia moyo.

Najipanga kuomba kibali cha kugombea na nina imani kabisa chama changu kitanipa fursa hiyo ili nifike mbele ya wanachama wenzangu wa jumuiya hiyo kutafuta ushindi na ninaamini wapiga kura watanielewa na kunipa kura za ushindi ili tufanye kazi pamoja.
 
Nakubaliana na wewe katika hili, lakini nakuhakikishia kwa hali ilivyo ndani ya chama chenu (ingawa mimi si mwanachama wa chama chochote) hiyo risk mliyochukua NI ZAIDI YA RISK..na zaidi sana kupabadilisha humo, kwa nature ya waliomo na waliweka mizizi ya uozo, inachukua zaidi idadi ya miaka aliyotumia Nyerere kuingia kwenye siasa hadi kupatikana kwa Uhuru mwaka 1961! kwa maneno mengine, kuibadili Tanzania yetu ili iondokanae na uozo huo sio lazima kuwa ndani ya CCM.

Sikukatishi tamaa, wewe na walio wa kariba yako kama kina J..Makamba na wengineo, lakin ninachomaanisha ni kuwa ikifikia mahali nia zako au zenu zilizo njema zinauliwa kwa mbinu zote (kama hayo uliyofanyiwa na kina Ghasia, na ule mkwala uliopigwa kuhusu yale maswala ya mgodini), si dhambi kutafuta njia mbadala, kwani naamini siku zote anayesimama katika ukweli atashinda, hata kama kiwiliwili chake hakitashuhudia ushindi huo-lakini Roho yake itaushuhudia! (umetoa mfano wa Dr. Martin Luther King)
ahsante kwa ushauri. nitaufanyia kazi...
 
Mimi siamini sana katika factor ya umri (mkubwa ama mdogo) kwenye uongozi. Mimi naamini zaidi kwenye uwezo wa kiuongozi. Tunategemea viongozi wenye umri mdogo wawe wabunifu sana kuliko wale wazee, lakini mara nyingi tumeona matokeo kinyume na matarajio haya. Tumeona pia mafanikio makubwa yakiletwa na viongozi vijana sehemu mbalimbali, ambako viongozi wazee wameshindwa. Mfano wa Joseph Kabila Kabange anavyoimarisha demokrasia kule DRC na pia anavyojenga mabarabara na viwanja vya ndege sasa hivi kule nchini kwake, anavyojenga mahospitali na anavyotetea nchi yake kufaidika na madini na rasmlimali - haya yaliwashinda baba zake akina Kabila Sr na Mobutu Sseseseko Kukungwendu wa Zabanga (aliyekuja kufa kidhalili kabisa), tunaona mambo makubwa aliyoyafanya Paul Kagame wa Rwanda. Tunaona mafanikio makubwa ya kuleta mabadiliko ya mahusiano kati ya watu weusi na weupe kule Marekani thru non-violence movements ya kijana Dr. Martin Luther King Jr, tunaweza pia kujifunza kutoka kwa akina Mwl. Nyerere na wenzake na makubwa waliyoyafanya kwa nchi yetu na Dunia kwa ujumla...and the list goes on! Tujiulize hawa wote walikuwa wazee?

Ukiwa muumini wa mabadiliko ya ukweli basi kwa vyovyote vile utatakiwa kuniunga mkono mimi na wanamapinduzi wengine wanaojitokeza kuomba nafasi za uongozi wa chama chetu, na kisha utanipa mawazo yako bila kujali ni kijana ama ni mzee kiasi gani. Sina nia nyingine yoyote ile zaidi ya kutaka kuingia kwenye vikao vya juu vya maamuzi ya chama changu ili kushawishi mabadiliko kutokea. Chama Cha Mapinduzi kinahitaji wanamapinduzi kama mimi kwa sasa, kwanza kwa ajili ya succession planning na pili kwa ajili ya nguvu mpya ya mabadiliko wanayoyahitaji waTanzania wa sasa. Kisipoamka na kuchukua nguvu mpya on board, kitayumba na hii itapelekea Taifa pia kuyumba. Tulio na nia nzuri na nchi yetu, na chama chetu tunachukua hatua kwa kuingia ndani na kushawishi mabadiliko! Wenzetu mjue kuwa tunachukua risk kubwa sana na mnachoweza kufanya si kingine tu bali kutuunga mkono na zaidi kututia moyo.

Najipanga kuomba kibali cha kugombea na nina imani kabisa chama changu kitanipa fursa hiyo ili nifike mbele ya wanachama wenzangu wa jumuiya hiyo kutafuta ushindi na ninaamini wapiga kura watanielewa na kunipa kura za ushindi ili tufanye kazi pamoja.
Mimi siamini sana katika factor ya umri (mkubwa ama mdogo) kwenye uongozi. Mimi naamini zaidi kwenye uwezo wa kiuongozi. Tunategemea viongozi wenye umri mdogo wawe wabunifu sana kuliko wale wazee, lakini mara nyingi tumeona matokeo kinyume na matarajio haya. Tumeona pia mafanikio makubwa yakiletwa na viongozi vijana sehemu mbalimbali, ambako viongozi wazee wameshindwa. Mfano wa Joseph Kabila Kabange anavyoimarisha demokrasia kule DRC na pia anavyojenga mabarabara na viwanja vya ndege sasa hivi kule nchini kwake, anavyojenga mahospitali na anavyotetea nchi yake kufaidika na madini na rasmlimali - haya yaliwashinda baba zake akina Kabila Sr na Mobutu Sseseseko Kukungwendu wa Zabanga (aliyekuja kufa kidhalili kabisa), tunaona mambo makubwa aliyoyafanya Paul Kagame wa Rwanda. Tunaona mafanikio makubwa ya kuleta mabadiliko ya mahusiano kati ya watu weusi na weupe kule Marekani thru non-violence movements ya kijana Dr. Martin Luther King Jr, tunaweza pia kujifunza kutoka kwa akina Mwl. Nyerere na wenzake na makubwa waliyoyafanya kwa nchi yetu na Dunia kwa ujumla...and the list goes on! Tujiulize hawa wote walikuwa wazee?

Ukiwa muumini wa mabadiliko ya ukweli basi kwa vyovyote vile utatakiwa kuniunga mkono mimi na wanamapinduzi wengine wanaojitokeza kuomba nafasi za uongozi wa chama chetu, na kisha utanipa mawazo yako bila kujali ni kijana ama ni mzee kiasi gani. Sina nia nyingine yoyote ile zaidi ya kutaka kuingia kwenye vikao vya juu vya maamuzi ya chama changu ili kushawishi mabadiliko kutokea. Chama Cha Mapinduzi kinahitaji wanamapinduzi kama mimi kwa sasa, kwanza kwa ajili ya succession planning na pili kwa ajili ya nguvu mpya ya mabadiliko wanayoyahitaji waTanzania wa sasa. Kisipoamka na kuchukua nguvu mpya on board, kitayumba na hii itapelekea Taifa pia kuyumba. Tulio na nia nzuri na nchi yetu, na chama chetu tunachukua hatua kwa kuingia ndani na kushawishi mabadiliko! Wenzetu mjue kuwa tunachukua risk kubwa sana na mnachoweza kufanya si kingine tu bali kutuunga mkono na zaidi kututia moyo.

Najipanga kuomba kibali cha kugombea na nina imani kabisa chama changu kitanipa fursa hiyo ili nifike mbele ya wanachama wenzangu wa jumuiya hiyo kutafuta ushindi na ninaamini wapiga kura watanielewa na kunipa kura za ushindi ili tufanye kazi pamoja.

Mkitazama mabandiko utafahamu Hkigwangala na Zulqranain ni mtu mmoja, teh teh teh teh teh acha kutuchezea Dogo
B:
 
@Kigwangala
Sijui kwanini upo kwenye siasa kama lengo lako ni kutetea maslahi ya wanyonge Mungu akubariki na atakuwa nawe daima ila kama lengo lako ni kuchukua chako mapema kama wenzio wa chama chako Mungu akusamehe sana ila Watanzania (hasa vizazi vijavyo) hawatakusamehe,walau kwa sasa hivi unamwelekeo wa kutetea wanyonge simama imara na wapiganie wanyonge usikatishwa tamaa na umri na makundi ndani ya chama chako (Japokuwa natamani sana ungekuwa kwenye magwandwa na sio kwenye Magamba ulipo) unaweza kuwa chachu ya mabadiliko ndani ya chama chako kilichooza
 
Back
Top Bottom