Malisa na Mikopo ya Elimu ya Juu

Malisa na Mikopo ya Elimu ya Juu

Wanafunzi wakinyimwa/kucheleweshewa mikopo Nyuzi za kuilaumu GOT ni za kutosha!lipeni tuu haya madeni Waungwana,mapovu hayasaidii...ule ulikuwa ni mkopo.
 
Hao ndio wabongo sasa, wao wakati wakiwa shimoni waliwekewa kamba wakavutwa bila masharti, walipofanikiwa kutoka tu wakaivuta kamba na kuiweka kwapani, sasa wale wengine walio shimoni wamepewa masharti ya kutolewa shimoni, SELFISH , SELFISH , SELFISH
 
Rahis wa wanyonge mungu anamuona
Kuna vingine naona, anapewa lawama zisizo za lazima... Unajua kuna muda ukiwa mkubwa on top, mambo yanakuwa mengi hadi kiasi cha kushindwa kuyaona mengine... Lawama zinatakiwa ziende kwa wale wasaidizi ambao walikaa chini na kufanya mahesabu yao.. kisha kumpelekea hiyo sheria na kumuamisha... Yeye si wa kulaumiwa kwa kila jambo
 
Basi serkali isitishe kutoa mikopo kila mtoto ajilipie kuepusha kelele
Chief kinacho matter hapo ni isssue ya kufuta neno loan, bali kiitwe Ruzuku.
Yaani wanasisa wana pewa Ruzuku ila wanafunzi wanapewa Mkopo doesn't make sense.
 
Mbona watuwanalalamikatu bila kuchukua hatua kama wasomi. Hivi hii sheria ilipotungwa haikuletwa kwa wadau ili kuijadili? na kama ni hivyo bado inaweza kufanyiwa marekebisho. kinachotakiwa watu watafute wabunge waelewa ili wapendekeze marekebisho ya sheria hiyo kandamizi.
 
Basi serkali isitishe kutoa mikopo kila mtoto ajilipie kuepusha kelele
Akili zako zina Shida wewe. Huelewi kitu gani hapo? Akili zako unajua watu wanampinga JPM? Pimbi wewe
 
Aisee, hii 6% retention fee ni janga kwa wadaiwa wa bodi ya mikopo nchini. Hebu jisomee mwenyewe hapa chini

=======================================

Wengi waliosoma nje ya nchi kwa kulipiwa na bodi ya mikopo (HESLB) wanadaiwa fedha nyingi kulinganisha na waliosoma nchini. Nimeona jamaa ana mshahara 900K but anadaiwa 47M. Kwa mwezi atakatwa 143K, kwa mwaka 1.7M. Under "ceteris paribus" mwamba atahitji miaka 28 kumaliza deni lake. Lakini ukiongeza "rention fee" atahitaji miaka 35 kumaliza deni.

Assume ana mika 30 kwa sasa. Jumlisha 35 ya kulipa deni atakua na miaka 65. Umri wa kustaafu ni miaka 60. Maana yake atastaafu bila kumaliza kulipa deni. Ikitokea hivyo Bodi itaenda kukomba kiinua mgongo chake kumalizia deni (kama sheria inavyosema). Sasa jiulize je huku ni kumsaidia mtanzania au kumkomoa?

Kunapaswa kuwa na mjadala wa kitaifa kuhusu mikopo ya elimu ya juu. Wazazi wanaoweza kusomesha watoto wao kwa kuwalipia ni vizuri wafanye hivyo, badala ya kuwaingiza kwenye mikopo hii inayoumiza. Pili, wazazi wasio na uwezo serikali iwape watoto wao ruzuku (bursary) si mikopo (loan).

Awamu ya kwanza na ya pili serikali iliwapa ruzuku wanafunzi wote wa elimu ya juu. Awamu zilizofuata zikaondoa ruzuku na kuleta mikopo. Nyerere na Mwinyi waliweza nini ambacho kimewashinda waliofuata?

Wakati wa Nyerere na Mwinyi wanafunzi wa vyuo vikuu walikula bure, kusoma bure, na kulala bure. Na bado walipewa pesa ya kujikimu. Kuna kipindi nchi ilipita kwenye hali ngumu kiuchumi Nyerere akapunguza bajeti ya mayai kwenye breakfast ya wanafunzi wa UDSM. Wakafanya mgomo. Akawaita Ikulu na kuwatia bakora.

Wakati ule mwanafunzi hana pressure ya ada, kula wala kulala. Anapewa pesa ya stationeries, field na research. Asubuhi anapewa breakfast yenye mapochopocho kibao (maziwa, mkate, mandazi, pancacke, chees, jam, mayai, juice, sambusa, sosage etc). Halafu wanapunguziwa mayai wanaamua kugoma. Nyerere akawatia bakora. Akawaambia msijifanye nyie ni muhimu kuliko watanzania wengine.

Sasa wale waliosomeshwa kwa ruzuku na kupata fursa zote hizo, ndio wameleta kitanzi kinaitwa mikopo ya elimu ya juu. Kitanzi hiki kimewatesa sana watoto wengi wa maskini. Hivi Nyerere nae angeweka mikopo hawa viongozi wa leo wangesoma? Nashauri MIKOPO ifutwe wanafunzi wapewe RUZUKU kama zamani. Rasilimali tulizonazo kama tifa zinatosha.!

C&P[/b]
 
Daaah!!

........Kama una uwezo somesha mwanao hii mikopo ni mizigo mizito sana.
 
Sitegemei hii bodi itakuwepo miaka yote, Kuna serikali itakuja madarakani itafanya marekebisho, na hata fao la kujtoa tungoje Magufuli aondoke Kuna serikali ya kiongozi mwenye huruma tutapata ataondoa haya mateso yanayotengenezwa na binadamu maana haya si majanga ya asili.
 
Sitegemei hii bodi itakuwepo miaka yote, Kuna serikali itakuja madarakani itafanya marekebisho, na hata fao la kujtoa tungoje Magufuli aondoke Kuna serikali ya kiongozi mwenye huruma tutapata ataondoa haya mateso yanayotengenezwa na binadamu maana haya si majanga ya asili.
Kuishi kwa matumaini ambayo huna hakika kama yatakuja.
 
YEHODAYA CCM Ni CHANZO Cha Matatizo. Hebu ona, hapo mtoto wa mkulima anafanywa kuwa fukara wa kudumu.
Lengo la mikopo hii Ni kumfanya mtoto wa masikini awe mtumwa milele.
 
Idadi ya vijana wanaojiunga na elimu ya juu ikishuka watakosa manamba wa kuwakata. Mwisho tutaajiri wataalamu kutoka nchi jirani.
 
Serikali ina wajibu wa kuwaendeleza wananchi wake kielimu na kiuchumi.

Uwezeshwaji wa wanafunzi wenye uwezo wa kiakili kusoma elimu ya juu ni jambo la muhimu sana kwa mustakabali wa taifa.
Hata hivyo, kuwasomesha wote wanaohitaji ni changamoto.

Utaratibu wa zamani wa kuwalipia wale walioongoza kwa ufaulu ulikuwa mzuri.

Tatizo lilianza pale ambapo viongozi na watendaji wa serikali walipotaka watoto wao waliokuwa na ufaulu unaoridhisha tu wapate ufadhili wa serikali pia.

Kuna haja ya kurudisha utaratibu wa natural selection, ili serikali isomeshe idadi inayoweza kwa asilimia 100.

Pili, serikali inatakiwa kuweka sera za kuwaendeleza kiuchumi vijana wanaomaliza vyuo kwa kuwadhamini na kuwapa tax holiday kwa muda maalum kwa wale wanaojiajiri.
 
Wengi waliosoma nje ya nchi kwa kulipiwa na bodi ya mikopo (HESLB) wanadaiwa fedha nyingi kulinganisha na waliosoma nchini. Nimeona jamaa ana mshahara 900K but anadaiwa 47M. Kwa mwezi atakatwa 143K, kwa mwaka 1.7M. Under "ceteris paribus" mwamba atahitji miaka 28 kumaliza deni lake. Lakini ukiongeza "rention fee" atahitaji miaka 35 kumaliza deni.

Assume ana mika 30 kwa sasa. Jumlisha 35 ya kulipa deni atakua na miaka 65. Umri wa kustaafu ni miaka 60. Maana yake atastaafu bila kumaliza kulipa deni. Ikitokea hivyo Bodi itaenda kukomba kiinua mgongo chake kumalizia deni (kama sheria inavyosema). Sasa jiulize je huku ni kumsaidia mtanzania au kumkomoa?

Kunapaswa kuwa na mjadala wa kitaifa kuhusu mikopo ya elimu ya juu. Wazazi wanaoweza kusomesha watoto wao kwa kuwalipia ni vizuri wafanye hivyo, badala ya kuwaingiza kwenye mikopo hii inayoumiza. Pili, wazazi wasio na uwezo serikali iwape watoto wao ruzuku (bursary) si mikopo (loan)

Awamu ya kwanza na ya pili serikali iliwapa ruzuku wanafunzi wote wa elimu ya juu. Awamu zilizofuata zikaondoa ruzuku na kuleta mikopo. Nyerere na Mwinyi waliweza nini ambacho kimewashinda waliofuata?

Wakati wa Nyerere na Mwinyi wanafunzi wa vyuo vikuu walikula bure, kusoma bure, na kulala bure. Na bado walipewa pesa ya kujikimu. Kuna kipindi nchi ilipita kwenye hali ngumu kiuchumi Nyerere akapunguza bajeti ya mayai kwenye breakfast ya wanafunzi wa UDSM. Wakafanya mgomo. Akawaita Ikulu na kuwatia bakora

Wakati ule mwanafunzi hana pressure ya ada, kula wala kulala. Anapewa pesa ya stationeries, field na research. Asubuhi anapewa breakfast yenye mapochopocho kibao (maziwa, mkate, mandazi, pancacke, chees, jam, mayai, juice, sambusa, sosage etc). Halafu wanapunguziwa mayai wanaamua kugoma. Nyerere akawatia bakora. Akawaambia msijifanye nyie ni muhimu kuliko watanzania wengine.

Sasa wale waliosomeshwa kwa ruzuku na kupata fursa zote hizo, ndio wameleta kitanzi kinaitwa mikopo ya elimu ya juu. Kitanzi hiki kimewatesa sana watoto wengi wa maskini. Hivi Nyerere nae angeweka mikopo hawa viongozi wa leo wangesoma? Nashauri MIKOPO ifutwe wanafunzi wapewe RUZUKU kama zamani. Rasilimali tulizonazo kama taifa zinatosha.!

Malisa GJ
Hapo kwenye kuchapwa viboko kwa kulilia mayai kwenye kifungua kinywa "umechapia".
 
Back
Top Bottom