Siasa za vyama vya upinzani zinasikitisha sana,sioni dalili za chama cha upinzani kushika Dola.
Kutokana na katiba yetu na baadhi ya sheria zetu,zinaweka mazingira magumu ya demokrasia ya vyama vingi,kiasi kwamba hakuna usawa katika mizani ya ushindani.
Kwenye awamu ya tatu wapinzani walikuja na baadhi ya madai ya kimsingi kabisa,wakitaka mabadiliko ya katiba na mabadiliko ya baadhi ya sheria za jamhuri na kanuni zinazosimamia sheria mbalimbali hasa za kiuchaguzi ili kuweka mizani ya kidemokrasia sawa.
Matokeo hatukuyaona zaidi waliishia kuvurugana tu,wakigombea ruzuku mwisho kusambaratika kabisa,hadi kufika uchaguzi wa 2005,hawakuwa na mgombea urais mwenye nguvu wala hawakuwa na agenda inayoeleweka hivyo hata madai yao kukosa nguvu,hivyo mgombea Urais wa CCM wakati huo mh. Kikwete kushinda kiulaini kabisa.
Katika miaka mitano ya kwanza ya awamu ya nne,wakaachana na madai ya katiba,na marekebisho ya sheria za uchaguzi na kanuni zake!!wakaja na agenda ya kuibua ufisadi iliyoasisiwa na katibu mkuu wa chadema enzi hizo DK Slaa.Agenda hio ikapata umaarufu sana,wananchi wakawaelewa,uchaguzi wa mwaka 2010 wakaleta changamoto kubwa kwa chama cha mapinduzi japo walishindwa ila walipata wabunge si haba.
Miaka mitano ya pili ya awamu ya nne wakaibua agenda yao ya toka awamu ya tatu, ya kutaka mabadiliko ya katiba wakaanzisha maandamano nchi nzima, mpaka mh.kikwete akakubali mchakato wa mabadiliko ukaanza,japokuwa walishindwa kujipanga vizuri mchakato ukafia njiani,tena mmoja wa aliesababisha mchakato ufie njiani ndie alikuja kuwa mgombea wao wa Urais mwaka 2015, na mwingine leo ndio mh. Rais wa jamhuri ya muungano wa awamu ya sita.
Mwaka 2015,kwenye uchaguzi mkuu katika hali isiyo ya kawaida dakika za mwisho kuelekea uchaguzi!! wakaleta mtu ambae wengi hawakutalajia ambae amekulia na kulelewa kwenye chama cha mapinduzi,ambae siku zote walikuwa wanamsema ni fisadi mkubwa.
Mtu mliekuwa mnamsema ni fisadi,mnamleta ili asimamie agenda yenu ya kukomesha ufisadi!!maajabu makubwa!! Mwisho wa siku wakokosa agendas ya kusimamia kwenye uchaguzi,wakaishia kuvurugana na mwisho kupoteza uchaguzi wenyewe, na CCM kuibuka mshindi kupitia kwa mgombea wake Hayati Magufuli.
Miaka mitano ya kwanza ya awamu ya tano, ilikuwa migumu sana kwao maana walikosa kabisa agenda,licha ya kupata wabunge wengi wakakosa namna ya kujipanga wakawa wanatoka bungeni hovyo bila sababu,wakakosa mbinu ya kupambana na utawala wa Hayati Magufuli,ambae alionyesha kutekeleza mambo mengi hivyo wananchi wengi walijenga imani nae,hasa baada ya wao kushindwa kusimamia agenda yao ya ufisadi waliokuwa Wana jaribu kuihubiri miaka yote.
Uchaguzi mkuu wa mwaka 2020,japokuwa walikuwa na mgombea mzuri upande wa chadema ila walikuwa hawana sera zinazoeleweka,zaidi mgombea wao alikuwa anahubiri tu madhara yaliyompata kutokana na kupinga sera za Hayati Magufuli!!kuliko kuwaeleza wananchi hatawafanyia nn?!!kuwaletea maendeleo.
Tunajua uchaguzi huo ulikuwa na changamoto kubwa sana,ila changamoto zingine zilisababishwa na wao kushindwa kujipanga na hasa kujifunza CCM uwa inafanya nini hasa inapokaribia kwenye uchaguzi mkuu!!walitegemea CCM ipate mpasuko,wanasahau CCM ndio mabingwa wa sayansi ya siasa. Na ili kukabiliana nao inabidi ufanye siasa za kisayansi zaidi pia ili uweze kuwashinda.
Leo tunaona wengi wa wapinzani wakishangilia kuondoka kwa mtawala wa awamu ya tano, Hayati Magufuli,ila wanasahau kuwa CCM ni ile ile ambayo inajibadili kama kinyonga,mama yetu mh.Rais Samia,kipindi cha kampeini uko mbeya alinukuliwa akisema kuwa:hata wananchi wasipoipigia CCM kura lakini wajue ndio itakayotangazwa na ndio itakayoongoza serikali!!na kweli tuliona CCM ikitangazwa kushinda katika baadhi ya majimbo na kata katika mazingira yaliyozua maswali mengi.
Lakini leo hii wapinzani hao hao ndio wanaomshangilia mama mh.Rais wakidai wana imani nae sana,hasa baada ya hotuba yake,pale aliposema atawaita ikulu waje wajadiliane nae!! Sasa maswali ni mengi je mama mh.Rais.hajui madai yao?!!je toka waanze kwenda ikulu enzi za mh kikwete ni nini walichokuwa wanajadili mpaka leo hawajawahi kupata muafaka?!!je sio kwamba ni mbinu za kisayansi za CCM kupoozesha washindani wake?!!
Wapinzani hawana agenda kiasi cha kutaka huruma ya mtawala ili wafanye siasa zao?!! Maswali ni mengi ila tunachoweza kuona ni kuwa wapinzani bado hawajawa na watu wakufanya siasa za kweli,wanachotaka tu ni huruma za mtawala ili wapate ruzuku na opportunities nyingine za kisiasa kwa manufaa yao na familia zao kwa mgongo wa upinzani.