Malinzi acha kutudanganya , tena acha.

Malinzi acha kutudanganya , tena acha.

Hata hivyo, Tenga alisema leo hii kiasi cha Sh. 664,000,000 kimehamishwa kutoka kwenye Akaunti za TBL kwenda kwenye Akaunti za TFF. Fedha hizo zitakuwa tayari kwenye Akaunti ya TFF ifikapo Jumanne wiki ijayo. Malipo haya yalikuwa yafanyike karibu miezi miwili iliyopita lakini yalicheleweshwa ili kutoa nafasi kwa zoezi la ukaguzi wa fedha za udhamini wa TBL kufanyika.
Tenga alisema zoezi limefanyika vyema na kufikia ukingoni, ndiyo maana malipo yamefanyika. Malipo mengine yanayofanana na hayo, ya Sh. 672,000,000 yanatarajiwa kufanyika wiki mbili kutoka sasa

haya 35,000,000 zilikua kwa AC
TBL walitoa 664 000 000 + 672 000 000

Jumla 1, 371,000,000

alizoachiwa na tenga, bado kuna makusanyo wamefanya. SASA hizo za wadau kulipa 120,000,000 zimetoka wapi ka si ufisadi


una uhakika na hizi hesabu?,usinilazimishe niongee ambayo hayaongeleki.
 
ameanza kuwa msanii mapema hv

ama nani amjui malinz

hzo pesa anajua anazirudishaje lakni c wale wa kuree bk

hawa rete soda hawa rete bia hao wape heineken

hapo ni harusn

tff c hatari

ahsante pdidy,Mungu ni wa wote.
 
Inavyoonekana uamuzi wa kumtimua Polsen ameufanya yeye binafsi ndio maana imebidi alipe fidia ya kuvunja mkataba.Sasa sijui hizo kamati alizounda na mshauri wake wanafanya kazi gani

Give me break!
 
Binafsi hawa huyu jamaa namuweka kwenye kundi la kina Rage na Ndolanga ni watu wanaofanya kazi kwa kujua fitina xa mpira wa bongo lakini kiukweli hawana uwezo wa kuongoza.

Biashara zake mwenyewe ni full ujanja wa mjini.
 
Mie niliisha muuliza sababu za kufuta (si kusitisha) utaratibu wa tickets za kielectronic lakini sababu alizotoa ni hafifu cha ajabu anatueleza eti TFF haina pesa!!!!! Bila kuficha utaratibu huu wanaoutumia ni kujinufaisha wao binafsi.
 
Uongozi kweli unahitaji moyo.

Sio moyo tu, hekima na bushara kubwa sanaaa.... usipoocheza na watu mkuu, utapata shida sana kuongoza TFF humu ndio walikupigia kampeni ukashinda leo umewatupa kwa uwazi, haki na kujibu majibu mepesi kwa maswali magumuuu

Ulilokosea kabisa ni....
 
Ndugu zangu,nia thabiti ya kujenga mpira tunayo.Ninakuombeni tushikamane katika kutimiza adhma hii.Tutake tusitake lazima mpira tuuendeleze kuanzia hatua za awali ,grassroot,na tukijaliwa hilo tutalifanya.Hakuna sababu ya kushughulikia mtu tushughulikie issues.Nashukuru Mungu alinipa kifua cha kupokea matusi ya kila aina bila kukasirika.
Ahsanteni wote,naiaga hii thread.
 
Mie niliisha muuliza sababu za kufuta (si kusitisha) utaratibu wa tickets za kielectronic lakini sababu alizotoa ni hafifu cha ajabu anatueleza eti TFF haina pesa!!!!! Bila kuficha utaratibu huu wanaoutumia ni kujinufaisha wao binafsi.

Jacobus i happen to be still around,la electronic nilikujibu,kama ulitaka yatokee maafa niambie.Tukisharekebisha kasoro utaratibu wa electronic ticketing utarudi,tuwe na subira.Unless Jacobus una alternative idea.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu zangu,nia thabiti ya kujenga mpira tunayo.Ninakuombeni tushikamane katika kutimiza adhma hii.Tutake tusitake lazima mpira tuuendeleze kuanzia hatua za awali ,grassroot,na tukijaliwa hilo tutalifanya.Hakuna sababu ya kushughulikia mtu tushughulikie issues.Nashukuru Mungu alinipa kifua cha kupokea matusi ya kila aina bila kukasirika.
Ahsanteni wote,naiaga hii thread.
Mkuu, hivi unajitambua kama ni rais wa taasisi kubwa inayosimamia soka hapa nchini? Sasa kujifanya kuwa mshauri wa klabu maana yake nini? Au ndo damu nzito kuliko maji? Unajishushia hadhi hata hivo.
 
Jacobus i happen to be still around,la electronic nilikujibu,kama ulitaka yatokee maafa niambie.Tukisharekebisha kasoro utaratibu wa electronic ticketing utarudi,tuwe na subira.Unless Jacobus una alternative idea.
Mkuu inakera kukusikia ukilalama kuwa TFF haina pesa wakati dawa ya kudhibiti mianya ya upoteaji pesa za mechi umeifungia kabatini. Nakupongeza kaka kwa hili la kuwa nasi humu japo maneno tutumiayo wakati mwingine yanakukera.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu zangu,nia thabiti ya kujenga mpira tunayo.Ninakuombeni tushikamane katika kutimiza adhma hii.Tutake tusitake lazima mpira tuuendeleze kuanzia hatua za awali ,grassroot,na tukijaliwa hilo tutalifanya.Hakuna sababu ya kushughulikia mtu tushughulikie issues.Nashukuru Mungu alinipa kifua cha kupokea matusi ya kila aina bila kukasirika.
Ahsanteni wote,naiaga hii thread.


Mheshimiwa kuna hoja za msingi sana zimezungumzwa huku lakini unazikwepa,naomba utolee ufafanuzi yafuatayo


1.Kuvunja mikataba ya waajiriwa wa TFF ambayo ilikuwa inakaribia kwisha(Osiah,Polsen,Marsh)

2.Ameteua kamati nyingi ambazo nyingi hakuna kazi wanayofanya,kuna nyingine tena ya miaka 50

3.Kulazimisha kuanza kutumia mfumo wa electronics tickets bila maandalizi ya kutosha

3.Kuajiri mtu ambae hana vigezo kutokana na job description waliotangaza mwenyewe(Mwesigwa)

4.Kuteua timu ya Taifa wakati yeye sio kocha
 
Nimeshtuka sana leo asubuhi, baada ya kusikia taarifa katika kituo cha RFA kipindi cha MATUKIO -michezo kuwa Jamal Malinzi Rais wa TFF atatoa pesa zake mfukoni kufidia malipo ya kukatisha mkataba wa Kocha wa timu ya taifa ndugu Poulsen.

Hapa ndo naanza kuona harufu ya ufisadi hapa na kwa sababuJamal Malinzi yuko humu basi ntamuomba aje kutoa ufafanuzi wa yafuatayo.

  • Ukiwa kama Rais wa TFF, Je shirikisho lina mgogoro wa kifedha kiasi kwamba haliwezi kabisa kulipa fidia hiyo?
  • Je huoni kwamba unatujemgea wasiwasi kua unajenga mazingira ya kujilipa hapo baadaye, tena zaidi kwa njia zisizo halali?
  • Je hii sio njia ya kuwa intimidate viongozi wengine ili waogope kuhoji baadhi ya matumizi yako ya pesa kwa kuwa tu umeanza na visingizio vya kutumia pesa zako Binafsi.
  • Je huoni kuwa hii ni conflict of interest?? Kwa nini utumie Pesa yako tena bila kuutangazia uma ni kiasi gani wakati shirikisho lina uwezo wa kulipa pia
  • kama kweli una nia hiyo thabiti, kwa nini msiwatangazie wana michezo kiasi halisi unachojitolea wewe mfukoni mwako... na kiasi anachodai Poulsen


Ndugu Jamal Malinzi, kwa watu wanaofanya "critical thinking" hii ni njia mojawapo inayotumiwa ni viongozi kujenga mazingira ya UFISADI hapo baadaye.

Tunakumbuka miaka ta tisini "CCM" iishindwa kuwalipa watumishi wake mikoani kwa takribani miezi sita, mpaka ROSTAM AZIZ alipojitolea pesa zake mfukoni na kuipa CCM ili iwalipe watumishi (nilikua pia CCM wakati huo so najua hili) lakini wote tunajua jinsi gani alijilipa hizo pesa na zaidi. mifano ya namna hii ni mingi sana.

Tupe hoja zako, unajipambanuaje katika hili??la sivyo ni kujenga mazingira ya ufisadi tuuu.

Waandishi watanzania kiboko.. Nikiskia kwa maskio yangu Malinzi alisema hivi makubaliano ya kuhitimisha mkataba na poulsen ni siri kati ya Serikali, Poulsen na TFF... sasa yule mwandishi akasema kuwa malinzi kasema katoa fedha zake mfukoni... nikajiuliza wapi amesema au ni kutoka nyuma ya kabati??.? Mwenye vidhibitisho aanike....
 
Last edited by a moderator:
Kwenye ile thread yake nilimuuliza alifuata nini kwa Lowassa na hajajibu mpaka leo.............mbabaishaji tu.......unamuondoa Paulsen na kumpa timu Madadi?

PIC.JPG

Tatizo la watanzania ni kwamba eti hata ukifanya kosa either la ukweli ama urongo basi lazima utengwe, why??? Kwani lowassa na malizni hawawezi kuwa marafiki???? Mbona tuna mawazo finyu sana... kwamba nikiongea na lowassa badi ninampango nae!!! Acheni kuwa na fikra potofu sio kila muongea na muhalifu basi nae ni muhalifu na huyo lowassa mna mhukumu wakati hamjui ni nini kilichopo nyuma ya pazia sisis tuna hukimu kwa kusikia maneno ya waandishi amabao wengi wauongo...
 
Uongozi kweli unahitaji moyo.

Jibu hoja mkuu, acha kulalamika..Kuna bullet tano kwenye hoja yangu zinazoitaji majibu.
kwani ulitegemea ukiwa kiongozi tusikuhoji??kweli?? tupe ufafanuzi please
 
Kuna makabila mawili ukimkuta Muhaya kasoma nani boss ni tabu sanaaaaa atakuwa anafanyakazi zote peke yake, au muha ni tabu sanaaaaaa.....
Bosi akiwa Muha inakuwaje Mheshimiwa, napenda kujua.
 
kaka yangu Jamali malinzi nakupongeza sana kwa kuweza kujibu maswali ya wadau kwa ufasaha na kadri ulivyo weza. Kwa hakika baadhi ya maswali ya wadau yatakujenga katika mabadiliko ya utendaji wako. Ila tambua maswali mengine yanatoka kwa wapinzani wako ambayo kimsingi utayafahamu tu. Uvumilivu na hekima uliyo nayo ndio msingi. Ushauri wangu kwako gawa majukumu kwa asilimia 75 na wewe ubakiwe na asilimia 25. Ni hilo tu kaka.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom