Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,500
- 9,279
Mali imemfukuza balozi wa Ufaransa kuhusiana na "matamshi ya kiuadui" yaliotolewa na maafisa wa mkoloni wake wa zamani, katika ongezeko jipya la mzozo kufuatia mapinduzi ya kijeshi. Uhusiana wa mataifa hayo umedorora.
"Serikali ya Jamhuri ya Mali inaufahamisha umma wa kitaifa na kimataifa kwamba leo...balozi wa Ufaransa mjini Bamako, Mh. Joel Meyer..aliarifiwa juu ya uamuzi wa serikali kumuomba aondoke katika ardhi ya taifa katika muda wa masaa 72," ilisema taarifa iliyosomwa kwenye televisheni ya taifa.
Uhusiano kati ya Mali na Ufaransa umezorota tangu jeshi lilipotwaa madaraka mnamo Agosti 2020.
Wiki iliyopita, waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian aliwaambia waandishi habari kwamba utawala wa kijeshi wa Mali ulikuwa "haramu" na maamuzi yake "siyo ya uwajibikaji."
DW Swahili
"Serikali ya Jamhuri ya Mali inaufahamisha umma wa kitaifa na kimataifa kwamba leo...balozi wa Ufaransa mjini Bamako, Mh. Joel Meyer..aliarifiwa juu ya uamuzi wa serikali kumuomba aondoke katika ardhi ya taifa katika muda wa masaa 72," ilisema taarifa iliyosomwa kwenye televisheni ya taifa.
Uhusiano kati ya Mali na Ufaransa umezorota tangu jeshi lilipotwaa madaraka mnamo Agosti 2020.
Wiki iliyopita, waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian aliwaambia waandishi habari kwamba utawala wa kijeshi wa Mali ulikuwa "haramu" na maamuzi yake "siyo ya uwajibikaji."
DW Swahili