Malezi ya wazazi wa siku hizi na dosari zake!

Hom tuliwahi kuishi na watu baki tu ila hakuna aliyewahi kuinua mdomo kumwambia mtu kuwa Ondoka hapa sio kwenu wala kukataa kutumwa na wale tuliokuwa tunaishi nao.
Niliwahi kuambiwa na mtoto wa baba mdogo kuwa ung'ang'ania na wewe upewe, kwani hapa kwenu, si uende kwenu. Nilikwenda kwao xmas moja hivi nikiwa mdogo, roho iliniuma mno siku hiyo, mama mtu alisikia vizuri yale maneno ila akakausha tu
Kuna sehem nilienda ile nafika tu mtoto wa miaka 7 ananiuliza "unaondoka lini" mama ake kasikia akacheka tu, mda wa kula ile nachukua chakula akaropoka " wewee unamaliza chakula " na mama ake kimya nilijiskia vibaya nikanyamaza nikamaliza kilichonipeleka nkasepa zangu.Nilijiuliza mtoto anawezaje ongea vile kwa mgeni na mzazi umenyamaza tu.
 
Hom tuliwahi kuishi na watu baki tu ila hakuna aliyewahi kuinua mdomo kumwambia mtu kuwa Ondoka hapa sio kwenu wala kukataa kutumwa na wale tuliokuwa tunaishi nao.
Niliwahi kuambiwa na mtoto wa baba mdogo kuwa ung'ang'ania na wewe upewe, kwani hapa kwenu, si uende kwenu. Nilikwenda kwao xmas moja hivi nikiwa mdogo, roho iliniuma mno siku hiyo, mama mtu alisikia vizuri yale maneno ila akakausha tu
Shukuru sana kupata malezi stahiki na hata mimi pia.Ki africa ni ngumu sana kukuta kuna usawa katika malezi...tumepitia vitu vingi sana katika maisha ila malezi ya huko awali ndio yametujenga kwa kiasi kikubwa mpaka sasa.

Niliwahi kwenda familia flani ..mama mwenye nyumba na watoto walikuwa peace sana ila kilichonikuta ni baba mwenye nyumba.Alinikuta sebuleni..nikamsalimia hakuitikia sasa wakati anafanya hilo tukio kuna watu waliona walikuwa kwenye dining.

Baadae baba yule mzee kwenda chumbani akarudi kuanza kujichekesha ...nafikiri aliaambiwa kuwa huyo ni mtoto wa flani.Yule ndugu alikuwa ni Doctor..alijisikia vibaya sana.Mana next day niliondoka ..
Kilichowauma zaidi huwa wakija kwetu hakuna habari za ajabu ajabu na kuna baadhi walikulia kwetu mzee wao akiwa huko alikokuwa.
Niliapa kutokwenda kwa ndugu yule hata kama naitwa,japo mzee aliomba msamaha na ile familia pia.Nina mpa sifa kubwa sana mama wa ile familia..mzee mpaka alinifuata yeye binafsi.
Si wazazi watu wote wapo hivyo..tunaumizwa na mambo mengi sana katika maisha yetu ya kila siku..na ndio sehemu ya malezi yetu kwa vizazi hivi na vijavyo...
 
Mathayo 23
13 Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.
14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu.
Screenshot_2019-07-12-10-31-40.jpeg
 
Na kipigo cha miaka hiyo ndicho kimepelekea utumwa kwa nchi zetu.

Sijawahi kuona wanyama wakipiga watoto wao. Kwanini wewe binadamu mwenye akili upige mtoto?

Mtoto hanyooshwi kwa kipigo. Bali maelekezo na mafundisho yaliyoambatana na kuona. Yaani mtoto anachoelekezwa ndicho anachopaswa kukiona kwenye jamii.

Nje ya hapo, ni kuumizana na kutiana uoga
Suala sio kipigo mkuu, jambo la muhimu ni maelekezo. Kinachozungumziwa ni kwamba wazazi wa siku hizi hasa wakike hawatoi hata hayo maelekezo au kuonya watoto wao wanapo misbehave

Kwako unaona ni jambo la kawaida mtoto kumdunda ngumi na mateke mama yake halafu mama anaishia kucheka na kusema pleeease acha basii!!!

Au mtoto wa miaka mitano anaibamiza chini kwa makusudi simu ya mama yake kisha mama anaishia kusema "mmmh leo huyu sijui kakasirika nini?'
 
Zaman haikuwa hv najiuliza sijui n uzaz kuwa mgumu au tatizo nini jaman
Tunaita maendeleo. Tunawapenda watoto kama property sio kama wanadamu

Fahari ya mzazi wa zamani ilikua ni kumuona mwanae anaishi kwenye jamii kama mtu aliyelelewa katika maadili

Fahari ya wazazi wa siku hizi ni kuona watoto wao wakiwa tofauti ki muonekano wa mavazi, elimu na hata maadili

Kwao wao akimpa mtoto mahitaji ya kimwili kama nguo na vitu vya kuchezea vya thamani na shule nzuri baaasi, imetosha maadili sio priority tena
 
Duh!,ndugu nimepigwa na butwaa by the way asante kwa kushare nasi.
Jumapili iliyopita nilihudhuria kwenye msiba wa ndugu wa rafiki yangu, Miongoni mwa waombolezaji alikua dada mmoja mwenye miaka kama 26-30, alikuwa na mwanae wa kama miaka minne hivi

Sijui ilikuaje lakini mara yule dogo akaanza kulia na kisha kumvurumishia ngumi na mateke mama yake. Mama mtu akabakia kusema tu " Brian stooop banaa". Mpaka mama mmoja alipokuja akamwambia hiyo ni aibu mwanao hata kama ni mdogo unamuachia akupige hivyo hebu ingieni kule chumbani mkabembelezane

Watoto wote wadogo sio ajabu kuwa na utundu lakini utundu mwingine nahisi kama ni wa kukosa adabu na unaendekezwa na wazazi hasa wakike.

Nimewahi kushuhudia mtoto wa chini ya miaka mitano akiipasua simu ya mama yake kwa makusudi kwa kuibamiza chini na mama mtu anasema "mmmh leo sijui kakasirika nini huyu!" halafu akaanza kumbembeleza!

Kuna mtoto wa shangazi yangu aliwahi kumtupia usoni mfuko wa chips mama yake baada ya kugundua alicholetewa sio alichomuagiza wakati anaenda kazini!

Hapo kwenye msiba baada ya tukio la huyo mama na mtoto watu walisema mengi sana kuhusu dosari za kimalezi za wazazi wa kike wa siku hizi. Kuna mzee mmoja akawa anasema dunia inavokwenda huko baadae hayo mapenzi ya mama na mwana yanaweza kufikia hatua ya aibu zaidi hata mama "kumuonjesha" mwanae atakapo balehe

Sina hakika kama haya mambo ya kudekeza watoto kiasi hiki yalikuwepo zamani ila nahisi mengine ni kuwapotosha watoto kwa kuwapa malezi yasiyofaa.
 
Yani aibu..nilichofanya nikakachukua nikakapeleka chemba kifinyo alichokipata nahisi alisimulia baba ake..maana kuna siku aliniambiaga nimepata habari zako kwa mwanangu..nikamjibu likizo mlete kwangu aje kukupa habari zaidi

Sipendagi ujinga na watoto wapumbavu
Hahahahahahhahaha unaona sasa mpaka mtoto anakosa adabu sababu ya kumchekeachekea.... Hapo akilia tu unamwangalia kwa jicho fulani hivi hahahahaha sura umeikunja mtoto anajua mmmh hapa sipo kidogo anaingiwa woga.....
 
Yani aibu..nilichofanya nikakachukua nikakapeleka chemba kifinyo alichokipata nahisi alisimulia baba ake..maana kuna siku aliniambiaga nimepata habari zako kwa mwanangu..nikamjibu likizo mlete kwangu aje kukupa habari zaidi

Sipendagi ujinga na watoto wapumbavu
Hahahahahahaha safiii ndo dawa yao wenyewe si wanamchekea toto gani lina domo chafu kama choo cha stendi
 
Boss ni mzazi mwenyewe tu sisi tumelelewa na mzee pamoja na maza tena home mzee Alikuwa hajui kupiga wala kugombeza mtoto na haongeagi tu.... Ila maza alitunyoosha kweli kweli tena mnoo akikutuma umekataa stiki, umesusa kula fimbo, ukiomba kitu kwa mtu akijua tu kipigo, umetumwa sehemu umechelewa kurudi fimbo,yaani kama vitani vile dingi hana huo Muda maza anakalisha watoto wa kiume jikoni mzee anawaka kwa nini!, maza anamwambia mimi ndiye niliyezaa we subiri tu nifundishe watoto, aseee yaani maza katuburuza kweli kweli hakuna mtoto mtukutu kati yetu.... Yaani ni adabu mwanzo mwisho.... Mimi nasema mama ndiye zaidi kwenye malezi sababu nimeyaona sijahadithiwa...
Mama zetu wanafanana haki tena..sisahau nilikua nahesabiwa masaa ya kurudi shule dah! Anajua shule unatoka muda Fulani kwahiyo unatakiwa hadi muda fulani uwe umeshakanyaga home sasa chelewa uone
 
Nakumbuka enzi za malezi yetu ukitaka kujaribu kufanya ujinga mama alikua na ishara zake mbili.ya kwanza kukukata jicho yapili ile sauti kama ya mtu mwenye kifua kikavu..ukiona amekupa sign hizo aisee hutamani hata kufanya ulichokua wataka kukifanya
Hahahahahahhahahahaha hapo kwenye kukata jicho namkumbuka bi mkubwa... Anakukata jicho hiloo na mdomo ameuvuta hahahahaha lazima uone mambo tofauti wenge unaacha wenyewe yaani lile jicho la karaha kabisa
 
Mama zetu wanafanana haki tena..sisahau nilikua nahesabiwa masaa ya kurudi shule dah! Anajua shule unatoka muda Fulani kwahiyo unatakiwa hadi muda fulani uwe umeshakanyaga home sasa chelewa uone
Hahahahahaha uuuwi wapewe heshima zao kwakweli..... Mimi nikiona mtoto anamtukana au kumjibu vibaya mamake au mtu mzima yeyote nashangaa kweli sijui inakuwaje yaani maza aseme kitu unyanyue mdomo!, hehehehe unavutwa shavu linasindikizwa kofi moja hilooo weeee hujakaa Sawa unawekwa bao la mdomo kesho hurudii
 
Hakika
Hapo hapo, mama alikuja kumdekeza dogo anaenifuata leo hii ni bomu la hatari, na huwa tunamwambia kabisa kwa huyo uliyataka mwenyewe wewe hangaika nae mwenyewe sababu yule dogo hawezi kwenda kuishi kwa mtu.
Ni kweli mtoto ukimlea vibaya hawezi kukaa na mtu.... Kuna dogo yupo form two ni wa kike anakaa na mamake utadhani mke mwenzie jamani mama mtu nae utakuta anaenda kulalamika kwa WiFi yake " mwanangu hanisikilizi nikimtuma hataki" eeeiiiish sasa unajiuliza yeye mwenyew hamuwezi huyo WiFi atamuweza?
 
Hahahahahaha uuuwi wapewe heshima zao kwakweli..... Mimi nikiona mtoto anamtukana au kumjibu vibaya mamake au mtu mzima yeyote nashangaa kweli sijui inakuwaje yaani maza aseme kitu unyanyue mdomo!, hehehehe unavutwa shavu linasindikizwa kofi moja hilooo weeee hujakaa Sawa unawekwa bao la mdomo kesho hurudii
Kuna vitoto vya mpangaji wetu vilikuja havina adabu ..vinamjibisha mama yao..vinakauli chafu..yani tabia za ovyo ovyo..nikawashikisha adabu mwanzo mama yao alikua anakasirika nikasema kasirika utanishukuru baadae..sasa hivi vimenyooka heshima na adabu..yani hata kusalimia mkubwa kwao ilikua shida siku hizi vikitoka shule hata kama nipo ndani vinagonga mlango shikamoo mamdogo c nawaambia namna hiyo..hadi baba yao anashangaa mabadiliko ya watoto wake
 
H
Nakumbuka enzi za malezi yetu ukitaka kujaribu kufanya ujinga mama alikua na ishara zake mbili.ya kwanza kukukata jicho yapili ile sauti kama ya mtu mwenye kifua kikavu..ukiona amekupa sign hizo aisee hutamani hata kufanya ulichokua wataka kukifanya
Hao ndio kina Super Mama, rolmodo, kina mama wa ukweli na ndio maana utaona hata yna2 leo ni mtu mbele za watu mwenye heshima na adabu zake tele

Hongera mama yna2
 
Hahahahahahhahahahaha hapo kwenye kukata jicho namkumbuka bi mkubwa... Anakukata jicho hiloo na mdomo ameuvuta hahahahaha lazima uone mambo tofauti wenge unaacha wenyewe yaani lile jicho la karaha kabisa
Hahahahaha mama zetu walijua kutulea jamani..kipindi Niko mtoto nilikua naona ni uonevu but now namshukuru kwa malezi Yale ..naweza ishi popote pasipo kulalama
 
Back
Top Bottom