Ugeni si kitu chema, Mpoto ndoalosema,
Pema usijapo pema,JF hakika ni pema,
Mimi mwingi wa hekima,nina mengi ya kusema,
Mstakabali ndo jina langu,nipokeeni wenzangu.
Ugeni si kitu chema, Mpoto ndoalosema,
Pema usijapo pema,JF hakika ni pema,
Mimi mwingi wa hekima,nina mengi ya kusema,
Mstakabali ndo jina langu,nipokeeni wenzangu.
usimfuate mpoto, upotoke kama foto,
miguu kama ufito, ewe malenga mtoto,
mizani gongo la mboto, na vina kwako ni ndoto,
hekima kitu adhimu, tutakupa tukipenda!
Wewe hunayo hekima, kisa umejiunga nasi
jitofautishe na kima, uyamenye mananasi,
vitani sikae nyuma, kwenye milio ya risasi
hekima kitu adhimu, tutakupa tukipenda.
Piga ngoma na kucheza, hii uliona wapi,
kiwete hawi mcheza, yeye bingwa wa pipi
mtini acha jikweza, tavuliwa mpaka chopi,
hekima kitu adhimu, tutakupa tukipenda,
kama kweli wewe ndiye, tusimulie kwa vina
ukiwa na kiseyeye, jei efu iko pina,
hatuchezagi uyeye, sijaribu kuguguna,
hekima hujipi wewe, jipambanue tukujue,
msikilize na Paw, vigezo uzingatie,
kama sheria ya faw, Invisible aipitie,
kama umezoea waw, ban Fang sikupitie
kweli wewe mgeni, kambayo guuni sitoe.
Karibu malenga mgeni, ukiweza wewe tiririririririririka, usiogopeshwe na vina vya jogi wala mizani ya Paw. Ukipatwa na maumivu mwone Painkila. Hapa ban kupenda, na tena utatamanishwa, mizingu gonga repoti utajibiwa na fang na si ffu
Mgeni Isaacbest hakika ujuvi, nia na utashu vimekuleta,
Nikuhabarishe kuwa ujio wako wa pekee na ni heri kukuleta, Invisible, Fang, Paw jukwaa la utambulisho umewaleta?
Hakika picha yajiri Isaac Newton jina lae pako ni sawia limegota.
Paw, isaacbest na jogi wanisamehe,
kwani mimi mashairi nachakachaua lol
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.