Malawi gives Tanzania's ambassador 48 hours to leave Malawi!

Status
Not open for further replies.
Sasa Balozi Tsere kajieleza kivyake kuwa ni msimamo wa WaTZ, JK anahusikaje hapo kwa Balozi kupewa 48hrs Raiswetu amziiee au aipuge Malawi
Kuna siku watu na matusi yao watataka JK akawapige mswaki
 
wakati hili sakata linaanza nilitoa wito wa amiri jeshi mkuu kupeleka vikosi mpakani akafikiri ni mzaha haya ndio matokeo yake
 
Katika vitu ambavyo tunatakiwa kushikamana ni wakati wa chokochoko ya vita. Sidhani kama una uzalendo kwa haya unayoandika, leo hii TZ ikipigana na Malawi waumiao ni ndugu zetu walioko kule mpakan na wapiganaji wetu, wengine nao tutaumia manake itabidi mambo mengi yasimame kwa ajili ya vita.

Lile ziwa tunahitaji strategy kubwa mno kumaliza huo mgogoro ambao haujaanza leo. SADC na AU wameshaelezwa, UN pia. Mazungumzo wamalawi wamejitoa, sababu mojawapo ni kutolewa ramani mpya ikionesha mpaka unapita kati ya Ziwa. Hii ni sababu ya kitoto mno, manake ramani zote za TZ zilikuwa zikionesha huo mpaka, sasa kwa nini tutoe ramani mpya mpaka tusiuoneshe?. Tumewapiga bao la kwanza wao kujitoa katika mazungumzo, bao la pili wanaanza wao kumfukuza Balozi wetu. Kama wanajianzaa kwa vita, sisi kwa itifaki tutawaacha mbali mno hivyo kuweza kutumia nchi nyingine kuwadunda.

Hivyo nakusihi, kwa hili hata kama unamchukia JK, unahitaji kuonesha uzalendo kwa nchi yako. Kumbuka chokochoko hizi ni kwa mafuta ya Ziwa Nyasa tu yanayotafutwa, zitakuja nyingi sana utakaposikia kuwa na Baharini kuna mafuta. Usidhani Malawi wanayofanya wameamua tu, kuna mkono/mikono ya watu. TAFAKARI.
Nakubaliana nawe ktk mambo yote isipokuwa hapo uliposema kuna mkono/mikono ya watu. Huu mgogoro huu ulikuwepo toka wakati wa uhuru kwa hiyo hatuwezi kusingizia mikono ya watu isipokuwa viongozi walizembea sana maana nao hawakuona umuhimu wa kulinda mpaka wetu ndani ya ziwa waliwaacha wamalawi wavue samaki upande wa Tz bila hata kuulizwa halafu leo wanajifanya wanaujua mpaka. Tunagharamia majeshi halafu tunakwepa kuyatumia mpaka pale tu maslahi ya wachache wanaoingia mikataba kwa niaba ya watz. Kama wangekuwa na uchungu na raslimali zinazowanufaisha wengi wangekuwa wamedhibiti wizi wa samaki uliofanywa na wamalawi kwa miaka mingi. Malawi wameona kuna udhaifu wa uongozi ktk Tz ndo maana wanataka wapandishe presha ili TZ itetereke maana wanajua CCM kwa sasa haina uhakika kama ikiamua vita baadae wataweza kukusanya silaha kutoka kwa wapiganaji, wanahofia isije ikawa baada ya kuipiga malawi kitakachofuata ni kuiangusha ccm.
 
mungu pitisha mbali,tanzani ni nchi ya amani na wenye uamuzi wa kuilinda amani hiyo ni sie wenyewe na vizazi vyetu
 
hapa kuna mind game kama ya babu wa loliondo CCM wanatafuta half-time nyingine, ni mchoro wa kitoto wenye akili tunajua kinachoendelea. Mungu kaijalia hii nchi wajinga wengi, wengi wetu hatuwezi kufikiri wala kuhoji.
[JFMP3][/JFMP3]
 
Hichi kimalawi kinataka nini??
Yaani ningekuwa Raisi ningewatumia F16 na F35
Au zile drones tatu tu ki nchi kinakuwa majivu hebu nisiongee mengi

Halafu utawasikia wenyewe wanasema
"Ooooh tukiwezeshwa tunaweza"
nisije pigwa ban bure
 
fukuza wa malawi pia sasa tz ifanye trade embargo kwa malawi,, kusiwe na chakula, mafuta na bidhaa nyingine za malawi kupita tz,,
 
Really now?..............then its on
"I am the Commander-in-chief and have not given any order for military action. I therefore would like to reassure our people that we have no plans to go to war with our neighbours over this or any other issue that can be resolved diplomatically," Jakaya Kikwete
 
Tanzania iimpe balozi wa Malawi masaa mawili awe ameshaondoka Dar es salaam,Na raia wa Malawi wapewe nusu saa wawe wamefutika katika ardhi ya Tanzania

Huyu mama si bure..kuna mtu anampa jeuri ya kufanya haya
 
Hichi kimalawi kinataka nini??
Yaani ningekuwa Raisi ningewatumia F16 na F35
Au zile drones tatu tu ki nchi kinakuwa majivu hebu nisiongee mengi

Halafu utawasikia wenyewe wanasema
"Ooooh tukiwezeshwa tunaweza"
nisije pigwa ban bure
 
Ukweli husemwa:

This is not about Tanzania and Malawi dispute, it's about big national and oil hungrler playing their incentive card to these poor Nation and It's going well to them.

Tanzania has left with no option now than to expell The Malawi ambassador.

When will Africa learn from their stupid mistake?.
 
Mshamba kikwete hata padri nyerere hampati kwa hekima busara na umakini na uelewa wa mambo, Mkatoliki nyerere aliacha haya matatizo bila ufumbuzi Aliacha tatizo la zanzibar bila ufumbuzi kikwete akalimaliza. Aliacha burundi bila ufumbuzi kikwete akaliweza
Kenya aliwapatanisha Comoro aliweza Na malawi ataliweka sawa wakati huyo bwana wenu nyerere kaacha matatizo kwani hakuwa kiongozi mwenye busara aliamini kwenye nguvu Hivo huyu mswahili wa bagamoyo atatua chia maelewano na malawi Zidumu fikra za mwalimu! Na zidumae fikra za wagalitia


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Balozi si yule aliyekuwa anashindana na Dr.Slaa Karatu Patrick Tsele kama sikosei...

Ndio huyo mkuu. Huyu hapa

patrick%20tsere.jpg
 
Hivi hawa hawategemei bandari ya Dar es salaam kwa imports and exports?
 
Ni wakati wa kumwaga ugali na sisi! Na tukianza hamna kurudi mezani tena, breki ya kwanza Lilongwe tunawapeleke na bonge la bili kama walivyofanyiwa waLibya
 
Bila shaka huyu Joyce banda kuna nchi inampa kiburi hiki alichonacho.....wasimfukuze barozi wa malawi ila Trade embargo inahusika sana....nchi za magharibi wanapenda mafuta yaani wako tayari hata watu wauane na unashangaa kuna watu huwaunga mkono katika migogoro wanayoisababisha Mashariki ya Kati sasa imehamia TANZANIA oooh my God
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom