Makumira University kumekucha!

Serikali ya JK sasa hivi inafanya kazi kama zima moto. walitumia hela nyingi kwenye uchaguzi kwa sababu ya kuchakachua matokeo yake ndio hayo sasa hazina hela.
 
First year Muco BIG UP!

VIONGOZI WA KIBONGO BILA NGUMI MAMBO HAYAENDI!

VIONGOZI TULIONAO HAWANA TOFAUTI NA AKINA GBABO.

UKOMBOZI HAUPATIKANI CHUMBANI ILA UWANJA WA MAPAMBANO.

SI MNAWAONA WENZETU KULE TUNISIA? MABOMU,RISASI, VIFARU,NA VIKOSI VYA WANAJESHI HAVIFUI DAFU MBELE YA MIOYO ILYO JIDHATITI!
 


mmh, Zimekuruka lini mwenzetu, maana haya si maneno
 
mmh, Zimekuruka lini mwenzetu, maana haya si maneno

jamani mbona mnakuwa hivyo? nilikuwa najaribu kujiuliza mbona serikali haijatoa kauli? na kwamba kauli yao tuliyoizoea ni hiyo, kwamba wanafunzi wanatumiwa na wanasiasa wa upinzani, kwamba hii nchi ni masikini sana serikali inajitahidi kadri iwezekanavyo, na kwamba lazima tuenzi amani na utulivu.

Nilidhani mngenielewa kwamba nakejeli
 
Jamani vumilieni bado tunalipa madeni ya kampeni, mlipopewa kanga, tshirts na kofia mlithani pesa ilitoka wapi. Endeleeni kufunga mikanda jama!
 

Mkuu ukiona unamgeukia Mungu hiyo ni dalili ya kukata tamaa!

Mungu hakuleta haya maswaibu yatupatayo sasa; TUMEYACHAGUA WENYEWE!

Tuwajulishe vijana wetu kuwa hali si nzuri, wakiweza kupata kwenye huu mgomo wajue wana bahati. Si wote tumesika eti polisi walipoitwa kwenye tukio la utekeji gari uko SEKENKE walisema magari yao hayana MAFUTA!

Hii ni ndani ya siku 100 za kwanza za JK, kazi anayo.............!
 
Kutoka IPPMEDIA.COM;


  • Wanachuo wa Chuo Kikuu cha Tumaini sehemu ya Makumira wafunga barabara ya Moshi/Arusha.Polisi watumia mabomu ya machozi kuwatawanya.

Nina imani hawa MATAAHIRA wetu wanaofikiri kwa kutumia matumbo yao, watasema kuwa ni CHADEMA wamesababisha haya. Kweli nchi hii inaongozwa na Chadema maana wafanyakazi wanawaogopa Chadema badala ya Rais na Serikali yake.
 
ndo serikali yetu hiyoooooooooooo
pesa zote ccm wamemiliki
na bado tutalia sana
mpaka deni la dowans liishe
 
Naskia hata vijana wa KIU-Dar Es salaam Campus(Gongo la Mboto) wako stranded

Watawala wanajua kulipa mikataba feki-feki bila kujali taifa pia linahitaji kuelimishwa kwa rasilimari alizotujalia mwenyezi Mungu.
 
hapa ni bla bla, huwezi kudai ambapo wakuu hawajaweka, maskini bwana mikopo mnantia majaribuni , tatizo ni serikal, imekimbilia kuilipa Dowans, wakulaumiwa si mtoa Mikopo pale Wizarani wakulaumiwa ni Kikwete Mwenyewe kwani hizo hela Hajazituma Hazina Hakuna kitu kumekauka kabisa, Haspolipa Dowans unategemea RA na EL watamfanyaje, si ulisikia mkono anadai basi wapunguziwe mzigo lakini walipwe, unafikiri zitatoka wapi
 
Gurudumu, nilisema nini kuhusu kugomea ukosefu wa fedha na kutokugomea sababu za ukosefu huo? Mara nyingi humu jamvini watu wamekuwa wakijiuliza nini cha kufanya kuzuia Dowans wasilipwe, nilijibu kwamba pressure groups such as vyuo ni wabinafsi sana! Watagomea kukosa mikopo lakini hawatagoma kupinga malipo ya Dowans! Maamuzi ya kipuuzi yanayosababisha kukosekana kwa mikono!
 

ni kweli. Badala ya kuweka pressure Dowans isipate ata senti,wanasubiri mikopo ikwame ndo wawakimbilie watetezi. Ingekuwa heri kama wanavyuo wote wangeandamana siku moja Tanzania kudai katiba mpya na kutolipwa Dowans. Lakini most of the time Tanzania tunatibu tatizo badala ya kuzuia dalili. Prevention is better than cure. Watanzania hamka tutoe kinga kabla ya kusubiri kutibu vidonda!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…