Kwame Nkrumah
JF-Expert Member
- Dec 2, 2008
- 886
- 376
Uamuzi huo ulikuwa umechangiwa kwa kiasi kikubwa na maoni shawishi ya mmoja wa Wenyeviti wa Mikoa, Mwenyekiti wa Mkoa wa Mara, Charles Makongoro Nyerere, aliyesema watu wa kawaida walikuwa wakishangazwa na CCM kuendelea kukumbatia watu waliokuwa wakionekana wanashiriki katika ufisadi.
Akichangia wakati huo katika tathmini na mapendekezo ya Kamati Kuu ya kutaka Chenge, Lowassa na Rostam wawajibike, Makongoro Nyererealisema isingewezekana Chenge, Lowassa na Rostam kuendelea kuwa na nafasi za uongozi ndani ya chama.
Alisema wakati huo mtoa habari wetu: Kwanza alianza kwa kumwambia Mwenyekiti kwamba japo yeye ni Mwenyekiti wa Taifa, yeye (Makongoro) naye ni Mwenyekiti wa Mara na kwamba NEC ndio waajiri wa Mwenyekiti Taifa.
Akasema anapokaa Mwenyekiti wa Taifa ni mahala patakatifu na kwa ajili hiyo pasingeweza kusogelewa na shetani, hata kama siku moja Mungu alipata kukutana na shetani barabani.
Akasema kule site (kwenye eneo la ujenzi ambako yeye ndiko anakoshinda akichanganya zege na kupiga bati) wanasema na wanataka watuhumiwa wote wa ufisadi watoke kwenye nafasi zao.
Lowassa ni ndugu yangu.Sina matatizo naye.Najua ananipenda, nami nampenda.Lakini kule site wanasema hapana.Atoke. Tena nawe Mweyekiti ulipokwenda Monduli, ukainua mkono wake juu, ukasema hujapata kuona kama yeye (Lowassa), kule site wakauliza, sasa hii ndiyo nini?
Rostam simfahamu vizuri. Ninakotembelea yeye hawezi kuja na mimi siwezi kwenda anakotembelea. Sina ugomvi naye.Lakini kule site wanasema naye hapana. Ulipokwenda Igunga ukamuamsha mkono ukasema ni kama timu ya mpira iliyokamilika watu kwenye site wakauliza sasa hii ndiyo nini?
Nasikia Chenge wanamwita Mzee wa Vijisenti. Ni ndugu yangu. Sina hakika kama anavyo vijisenti kiasi hicho. Lakini kwenye site, si mimi, watu wanasema naye hapana, alikaririwa akisema Makongoro.
SOMA ZAIDI HAPA: Raia Mwema | Lowassa apambana
Lowasa ana nguvu kiasi gani mpaka wanachama milioni 4 wa CCM wanashindwa kumtoa?
JK hawezi kumtoa Lowasa hata siku moja, kwa kutoa siri zao kidogokidogo ni kama vile Lowasa anamwambia JK angalia sana, nina mengi zaidi ya kusema. JK ameshikwa mateka na Lowasa. Lowasa hana cha kupoteza kama ataongea yote.
Akichangia wakati huo katika tathmini na mapendekezo ya Kamati Kuu ya kutaka Chenge, Lowassa na Rostam wawajibike, Makongoro Nyererealisema isingewezekana Chenge, Lowassa na Rostam kuendelea kuwa na nafasi za uongozi ndani ya chama.
Alisema wakati huo mtoa habari wetu: Kwanza alianza kwa kumwambia Mwenyekiti kwamba japo yeye ni Mwenyekiti wa Taifa, yeye (Makongoro) naye ni Mwenyekiti wa Mara na kwamba NEC ndio waajiri wa Mwenyekiti Taifa.
Akasema anapokaa Mwenyekiti wa Taifa ni mahala patakatifu na kwa ajili hiyo pasingeweza kusogelewa na shetani, hata kama siku moja Mungu alipata kukutana na shetani barabani.
Akasema kule site (kwenye eneo la ujenzi ambako yeye ndiko anakoshinda akichanganya zege na kupiga bati) wanasema na wanataka watuhumiwa wote wa ufisadi watoke kwenye nafasi zao.
Lowassa ni ndugu yangu.Sina matatizo naye.Najua ananipenda, nami nampenda.Lakini kule site wanasema hapana.Atoke. Tena nawe Mweyekiti ulipokwenda Monduli, ukainua mkono wake juu, ukasema hujapata kuona kama yeye (Lowassa), kule site wakauliza, sasa hii ndiyo nini?
Rostam simfahamu vizuri. Ninakotembelea yeye hawezi kuja na mimi siwezi kwenda anakotembelea. Sina ugomvi naye.Lakini kule site wanasema naye hapana. Ulipokwenda Igunga ukamuamsha mkono ukasema ni kama timu ya mpira iliyokamilika watu kwenye site wakauliza sasa hii ndiyo nini?
Nasikia Chenge wanamwita Mzee wa Vijisenti. Ni ndugu yangu. Sina hakika kama anavyo vijisenti kiasi hicho. Lakini kwenye site, si mimi, watu wanasema naye hapana, alikaririwa akisema Makongoro.
SOMA ZAIDI HAPA: Raia Mwema | Lowassa apambana
Lowasa ana nguvu kiasi gani mpaka wanachama milioni 4 wa CCM wanashindwa kumtoa?
JK hawezi kumtoa Lowasa hata siku moja, kwa kutoa siri zao kidogokidogo ni kama vile Lowasa anamwambia JK angalia sana, nina mengi zaidi ya kusema. JK ameshikwa mateka na Lowasa. Lowasa hana cha kupoteza kama ataongea yote.