Makondakta wa Daladala wanawanyanyasa wanafunzi, Mamlaka chunguzeni mchukue hatua

Dumas the terrible

JF-Expert Member
Jan 20, 2021
4,104
8,339
Salamu wakuu,

Poleni na changamoto za January naamini zitapita tu Kama upepo wa kisulisuli

Husika na kichwa cha habari hapo juu,
Katika hali ya kushangaza na kustaajabisha kama sio kukera sana ni suala la makondakta wa Daladala kuwanyanyasa wanafunzi waendapo shuleni asubuhi na jioni wakati wa kurudi.

Kuna tabia ya ajabu nimeishuhudia hapa Tegeta kwa Ndevu watoto wakizuiliwa kupanda Daladala za kwenda mjini kwa kisingizio limejaza huku wakiruhusu watu wazima.

Vilevile katika hatua hiyo watoto wanapogombania kupanda husukumwa vibaya na makondakta hao na kuanguka na kusabasha majeraha na hatari kubwa bila huruma.

Kikubwa cha kushangaza ni abiria wa Tegeta kukaa kimya kama hawaoni sababu ya ubinafsi mkubwa. Note: Hakuna raia wa ajabu Kama wa hii Bagamoyo road ni watu wasiojali tofauti na wa Buza wenye ushirikiano mkubwa na umoja.

Ifike mahali Watanzania tubadilike Kama tusipojali Mambo madogo makubwa yatatupiga mweleka.

Imagine hawa watoto wanajengewa roho mbaya na kutokujali siku wakija kua viongozi wasipojali maslahi ya wengi tusilaumu maana Mtu roho mbaya haziliwi nayo Bali hujifunza hapa hapa.

Imagine watoto wanaosukumwa waje kua Trafiki mbeleni halafu waaanze kuwafanyia roho mbaya msije mkalaumu.

Kesho yetu hujengwa na leo Makondakta mbadilike muwe na huruma. Vilevile napendekeza wahusika hasa kitengo cha usalama barabarani tunaomba angalau kwenye vituo vya Daladala kuwe na Askari maalumu wa kuwasaidia watoto Hawa maana huteseka Sana bila msaada!

The terrible!
 
Salamu wakuu,Poleni na changamoto za January naamini zitapita tu Kama upepo wa kisulisuli

Husika na kichwa Cha habari hapo juu...
Utaki mtoto wako asukumwe kwenye basi ishi karibu na shule au mpeleke shule binafsi awe anapanda basi la shule au hama jiji hilo halaka kwani dar kuna mateso sana mtoto anaishi goba anasoma mwenge au Mbezi kuamka saa 11 asubuhi kuludi saa 12 jioni mvua yake jua lake njaa yake kiu chake ndio maana mimi niliamua kuhama jiji hilo hivi sasa naishi shamba watoto wanaenda shule kwa baisikeli kilomita 3 shule iko karibu kuishi dar ni utumwa
 
Huku Buza kuna askari napendaga kazi anayoifanya, akikamata gari likiwa na kosa dogo anachokifanya anapanda kwenye hilo gari mpaka kituo cha daladala aidha Buza Kanisani, Kwa Lulenge au penginepo kisha anatoa amri wanafunzi wooote waliopo kituoni waingie mule wapelekwe shule.

Yule askari namkubali sana.
 
Utaki mtoto wako asukumwe kwenye basi ishi karibu na shule au mpeleke shule binafsi awe anapanda basi la shule au hama jiji hilo halaka kwani dar kuna mateso sana mtoto anaishi goba anasoma mwenge au mbezi kuamka saa 11 asubuhi kuludi saa 12 jioni mvua yake jua lake njaa yake kiu chake ndio maana mimi niliamua kuhama jiji hilo hivi sasa naishi shamba watoto wanaenda shule kwa baisikeli kilomita 3 shule iko karibu kuishi dar ni utumwa
Mkuu soma mada vizuri, Mimi sina mtoto ila nimeguswa na hili.

Hivi hii Tanzania Kila mtu anaweza kusomesha Kama uwezavyo wewe?

Acha kua mbinafsi mkuu haya maisha watu wote hatuwezi kua sawa aisee think twice!
 
Huku Buza kuna askari napendaga kazi anayoifanya, akikamata gari likiwa na kosa dogo anachokifanya anapanda kwenye hilo gari mpaka kituo cha daladala aidha Buza Kanisani, Kwa Lulenge au penginepo kisha anatoa amri wanafunzi wooote waliopo kituoni waingie mule wapelekwe shule.

Yule askari namkubali sana.
Abarikiwe Sana huyo Askari daaa hali ni mbaya Sana asubuhi na jioni kwa Hawa watoto mkuu watu wabinafsi mno!
 
Mkuu soma mada vizuri, Mimi sina mtoto ila nimeguswa na hili.

Hivi hii Tanzania Kila mtu anaweza kusomesha Kama uwezavyo wewe?

Acha kua mbinafsi mkuu haya maisha watu wote hatuwezi kua sawa aisee think twice!
Sijasema kuwa unamtoto ila maisha ya dar nichangamo ya kubwa sana tabua kwa Makonda walio wengi ni wavuta bhange pia usafiri huo wa dala dala ni wawatu wadalaja lachini sana kimaisha usitegee usitarabu
 
Sijasema kuwa unamtoto ila maisha ya dar nichangamo ya kubwa sana tabua kwa Makonda walio wengi ni wavuta bhange pia usafiri huo wa dala dala ni wawatu wadalaja lachini sana kimaisha usitegee usitarabu
Ndio hivyo mkuu japo hatua zichukuliwe kupunguza tatizo
 
Salamu wakuu,

Poleni na changamoto za January naamini zitapita tu Kama upepo wa kisulisuli

Husika na kichwa cha habari hapo juu,
Katika hali ya kushangaza na kustaajabisha kama sio kukera sana ni suala la makondakta wa Daladala kuwanyanyasa wanafunzi waendapo shuleni asubuhi na jioni wakati wa kurudi.

Kuna tabia ya ajabu nimeishuhudia hapa Tegeta kwa Ndevu watoto wakizuiliwa kupanda Daladala za kwenda mjini kwa kisingizio limejaza huku wakiruhusu watu wazima.

Vilevile katika hatua hiyo watoto wanapogombania kupanda husukumwa vibaya na makondakta hao na kuanguka na kusabasha majeraha na hatari kubwa bila huruma.

Kikubwa cha kushangaza ni abiria wa Tegeta kukaa kimya kama hawaoni sababu ya ubinafsi mkubwa. Note: Hakuna raia wa ajabu Kama wa hii Bagamoyo road ni watu wasiojali tofauti na wa Buza wenye ushirikiano mkubwa na umoja.

Ifike mahali Watanzania tubadilike Kama tusipojali Mambo madogo makubwa yatatupiga mweleka.

Imagine hawa watoto wanajengewa roho mbaya na kutokujali siku wakija kua viongozi wasipojali maslahi ya wengi tusilaumu maana Mtu roho mbaya haziliwi nayo Bali hujifunza hapa hapa.

Imagine watoto wanaosukumwa waje kua Trafiki mbeleni halafu waaanze kuwafanyia roho mbaya msije mkalaumu.

Kesho yetu hujengwa na leo Makondakta mbadilike muwe na huruma. Vilevile napendekeza wahusika hasa kitengo cha usalama barabarani tunaomba angalau kwenye vituo vya Daladala kuwe na Askari maalumu wa kuwasaidia watoto Hawa maana huteseka Sana bila msaada!

The terrible!
Serikali inunuea Mabasi ya wanafunzi, sio jukumu la Wamiliki wa Dalaladal kusafirisha wanafunzi
 
Umaskini ndio unasababisha hayo yote, watoto wote wa shule walipaswa wawe wanaenda shule kwa gari maalum za wanafunzi na sio kuchanganyikana na watu wa kila aina wakienda au kurudi shule tena kwa huruma za konda tu.
 
Ni vizuri watu wazae watoto wanaoweza kumudu kuwahudumia vizuri. Usizae watoto kwa kutugemea serikali au watu wengine waje kukusafirishia watoto wako kwenda shuleni katika hali bora.
Mkuu soma mada vizuri, Mimi sina mtoto ila nimeguswa na hili.

Hivi hii Tanzania Kila mtu anaweza kusomesha Kama uwezavyo wewe?

Acha kua mbinafsi mkuu haya maisha watu wote hatuwezi kua sawa aisee think twice!
 
Watoto wa siku hizi nao ni nyoronyoro za sana enzi hizo tungeweza kumpa kichapo huyo konda kwa ushirikiano
 
Back
Top Bottom