Makonda: Walimu kusafiri bure

Makonda: Walimu kusafiri bure

Naomba kuuuliza. Hivi hawa walimu wakipanda bure nani anakua kahusika kumsafirisha? Au serikali wanakua wanatenga fungu kuwapa wamiliki wa magari au wataruhusiwa kupanda kwenye uda? Kwa ushauri wa bure wanunuliwe mabasi yao ili hizi gharama ziwe za serikali kama ilivyo kwa watumishi wengine
 
makonda ana hoja nzuri tatizo ni namna ya kuitekeleza...
unajua tembo likisifiwa sana mgema hulitia maji, huyu jamaa akae apange strategies zake vizuri, lakini akitaka kutafuta sifa sana kazi itamshinda na kujikuta anaharibu kila kitu, mmiliki gani wa mabasi atakubali kusafirisha waalimu bure wakati wanafunzi wanalipa nauli. hao askari tu ni kwa vile wanauwezo wa kutumia mabavu, vinginevyo ingekuwa ngumi kila leo kwenye mabasi
 
Mi sio mchumi hivyo siwezi kujifanya naelewa sana. Ila kwa akili za kawaid bila shule, kama mapata ya serikali yanaongezeka kupitia kodi kama tunavyoelezwa, je haiwezi saidia kuongeza mishahara? Kama unataka uadilifu na ufanisi, je? motisha si utasaidia kwa watumishi wa umma?
Ni kweli mkuu ila ndio tuombe kasi ya ukusanyaji kodi iendelee kuwa hivi kwa mwaka mzima ndipo mengine yote mtabarikiwa
 
Uwezo wa kufikiri wa viongozi wetu ni wa kimaskini ndio maana unaona wanataka watu wapate huduma bure. Hawa ndio wakikaa ofisini wanajitahidi kuandika proposal za kusaidiwa na wafadhili. Kichekesho kinakuja siku huyo mfadhili anayekuja kukuletea huo msaada yeye anakuja na gari moja tena Rav4, huyo aliyeomba msaada anakuja na msafara wa maVX V8!! Nijuavyo mimi mafuta yameshuka bei sana duniani, ni kwanini asiibane serekali yake kuhakikisha mafuta yanashushwa bei hapa nchini ambapo itapelekea nauli kushuka, sambamba na kuboresha mishahara ya waalimu kila mmoja aweze kujilipia nauli? Ama kama ni mzalendo kweli auze shangingi lake litumike kulipia nauli za walimu na yeye apande daladala aone dhahama ilipo na wakati huohuo apendekeze mishahara ya wakuu wa wilaya ipunguzwe ili kupandisha mishahara ya waalimu, potelea mbali hata kama mapendekezo yake hayatatekelezwa lakini wangalau watu wataona uzalendo wake wa yeye kupakia daladala. Kama sio kusanifu watu na kutafuta sifa za kijinga ni nini. Wewe mkuu wa wilaya tena kijana unaenda kazini na kukata mitaa na shangingi linalokula mafuta kuliko tija yake, halafu ukawaombee watu wasafiri bure kwenye magari ya wafanya biashara na wakati huohuo unataka walipe kodi!!!

Wajibu wa serikali ni kuweka mazingira ya kufanya nauli iwe affordable kwa kila mtu. Maana yake ni miundombinu mizuri na ya kutosha.

Mambo ya kusema huyu alipe na yule asilipe ni ukosefu wa kuona mbali. Ni sawa na mtu anayefikiria njaa ya leo tu. Kila taaluma ni muhimu kwa maendeleo ya nchi. Mimi huwa sikubali kuwa kuna taaluma muhimu kuliko nyingine. Hata nyuki kwenye mizinga wana mgawanyo wa kazi ili aslai itoke. Kikikosekana kimoja tu, hamna asali!
 
Kama kweli anataka kuwasaidia ni serikali kuwapa posho ya mazingira magumu walimu na wale wafanyakazi wengine wa serikali wafanyao kazi katika mazingira magumu. Hilo la kupanda bure kwenye daladala nk, nafikiri anakurupuka kwani kwa sasa haliwezekani tuko kwenye uchumi wa kibepari. Kabla ya uamuzi huo anapaswa kujiuliza na kupata majibu ya maswali haya: Je anajua idadi yote ya walimu wote ? je wenye magari watafidiwaje katika hilo make wanafanya biashara na sio msaada, Je kada zingine nazo hazistahili kujaliwa kama walimu? Je ni walimu wa dar tu au wote nchi nzima? kama ni dar, je wengine walioko huko mikoani nk hawastahili kujaliwa kama hao wa dar? (Tena hao ndio wanafanya kazi katika mazingira magumu kweli kweli)
Nafikiri anapaswa kuwaza nje ya box kabla ya kuamua na kuchukua maamuzi hayo. Ni mtazamo tu
 
makonda ana hoja nzuri tatizo ni namna ya kuitekeleza...
Kha! Hivi daladala linamuisha mtu kazini? Na kama linawaisha watu kazini ina maana walimu wamekosa mia 4 ya nauli kwenda shuleni. Nafikiri kuwaambia wasafiri bure ndio watachelewa zaidi kazini Refer Wanafunzi gari moja wataambiwa apande mmoja wengine wasubiri magari mengine. Fikiria ukiwa nje ya Box na sio ndani ya box.
 
Ukisoma mawazo ya watu kwenye hoja hii utagundua wengi ya wanaochangia hawajaenda shule kabisa ndo maana hawajui hata waandike nini na waache nini-WALIMU WANA KAZI PEVU
 
Mimi naona ni Good idea, Kama mwanajeahi au askari anasafiri bure.. Kwa nini mwalimu asidafiri bure na yeye? Wawe na vitambulisho tu... Mwalimu ni mtu muhimu sana ...
Mawazo ya kijima haya. Hawalipwi mshahara? Hizo daladala zinapewa punguzo wakati wa matengenezo au kununua mafuta? Kwa nini wasipewe kuponi za kusafiria bure ambazo zitalipiwa na serikali?
 
Ukisoma mawazo ya watu kwenye hoja hii utagundua wengi ya wanaochangia hawajaenda shule kabisa ndo maana hawajui hata waandike nini na waache nini-WALIMU WANA KAZI PEVU
Mkuu, kwahiyo tulijulia wapi kusoma na kuandika?
Hahahaaa....
 
Kabla ya hizo hadithi, hebu lipeni malimpikizo, wapandisheni vyeo, wapatiwe likizo, wapatiwe Nyumba za kuishi.
 
Mimi naona ni Good idea, Kama mwanajeahi au askari anasafiri bure.. Kwa nini mwalimu asidafiri bure na yeye? Wawe na vitambulisho tu... Mwalimu ni mtu muhimu sana ...
ushasema wanajeshi na askari,these guys are scary..nani anamuogopa mwalimu mbeba fimbo!kwanza hata kuchapa siku hizi hawaruhusiwi..
 
ushasema wanajeshi na askari,these guys are scary..nani anamuogopa mwalimu mbeba fimbo!kwanza hata kuchapa siku hizi hawaruhusiwi..
Anachojaribu Kufanya hapa huyu Paul hamjamuelewa tu.. Mimi naona kuwa hapa huyu jamaa hata kama atashindwa kufikia muafaka wa waalimu kutolipa nauli ila lazima kuna avout flan ambazo waalimu watazipata na zitawapa ahueni...
 
Naunga mkono hoja ya Makonda but with one condition; hiyo kitu ifanyike kwa gharama za serikali na sio gharama za Wafanya biashara. Mmiliki wa daladala anunue mafuta, vipuri na gharama zingine kwa bei ya sokoni halafu serikali itafute sifa kwa kumsafirisha BURE mwalimu kwa gharama za mtu mwingine? Hapana, hilo halikubaliki kabisa.
 
Ni kweli mkuu ila ndio tuombe kasi ya ukusanyaji kodi iendelee kuwa hivi kwa mwaka mzima ndipo mengine yote mtabarikiwa
Ngoja mkuu akazane lakini nadhan kunatakiwa mfumo mzuri wa kodi, ili iwe rahisi kwa serikali kujua nani halipi na nani analipa bila kukwepa.
 
Angesema kila katikati ya mwezi walimu wapewe fedha ya nauli ata 50,000 ningemwelewa,wengine wanaenda sehemu hakuna daladala wanatumia bodaboda.
Polisi pia wasikamate walimu hovyo wanapokua na viusafiri vyao na Tra wasiwaghasi kwani kodi wanayolipa inatosha.
Tabia za makondakta nichafu Sasa tusiwagonganishe na walimu kisa mia tatu tatu,walimu wasijedhalilishwa kuwa hawana hâta miatatu

Mkuu yani walimu wakifanya makosa tra wasiwashike kisa wao walimu,nchi hii itakwenda kweli namna hiyo?
 
Back
Top Bottom