Makonda: Walimu kusafiri bure

Makonda: Walimu kusafiri bure

Madaktari ni watu muhimu zaidi kuliko waalimu... nao wasafiri bure tena wakiwa ndani ya mabasi wasisimame!!
Madaktari ni watu muhimu kwa wagonjwa na sio kwa kila mtu... Hata wewe kama ni fundi umeme una umuhimu wako.. Kwa sababu ukizima umeme hao madaktari watachajia simu zao kwenye nini?
Kila kitu kina umuhimu wake... Hapa Makonda kaangalia tabaka la waalimu lilipo. Umuhimu wao kwenye jamii na sehemu waalimu waliyopo.. Japo wanatakiwa wawe kama walivyo na mishahara yao ndio inatakiwa iwe hivyo kutokana na nature ya kazi ila .. Kuwapa ahueni sio jambo baya...
Gotcha?
 
Wanajeshi, Polisi na Askari Magereza wanasafiri bure. Sasa inapendekezwa Walimu nao wasafiri bure. Baadaye kidogo itapendekezwa Madaktari na Wauguzi nao wasafiri bure. Hautapita muda mrefu kila mtu atakuwa na kitambulisho cha Mwl au Daktari/Muuguzi.

Nani atalipa nauli kwenye daladala?

Uwezo wa kufikiri wa viongozi wetu ni wa kimaskini ndio maana unaona wanataka watu wapate huduma bure. Hawa ndio wakikaa ofisini wanajitahidi kuandika proposal za kusaidiwa na wafadhili. Kichekesho kinakuja siku huyo mfadhili anayekuja kukuletea huo msaada yeye anakuja na gari moja tena Rav4, huyo aliyeomba msaada anakuja na msafara wa maVX V8!! Nijuavyo mimi mafuta yameshuka bei sana duniani, ni kwanini asiibane serekali yake kuhakikisha mafuta yanashushwa bei hapa nchini ambapo itapelekea nauli kushuka, sambamba na kuboresha mishahara ya waalimu kila mmoja aweze kujilipia nauli? Ama kama ni mzalendo kweli auze shangingi lake litumike kulipia nauli za walimu na yeye apande daladala aone dhahama ilipo na wakati huohuo apendekeze mishahara ya wakuu wa wilaya ipunguzwe ili kupandisha mishahara ya waalimu, potelea mbali hata kama mapendekezo yake hayatatekelezwa lakini wangalau watu wataona uzalendo wake wa yeye kupakia daladala. Kama sio kusanifu watu na kutafuta sifa za kijinga ni nini. Wewe mkuu wa wilaya tena kijana unaenda kazini na kukata mitaa na shangingi linalokula mafuta kuliko tija yake, halafu ukawaombee watu wasafiri bure kwenye magari ya wafanya biashara na wakati huohuo unataka walipe kodi!!!
 
Hapa wanataka walimu tudhalilishwe tu. Konda ataropoka na kutoa kashifa mfano hili sio darasa nimeshabeba walimu wametosha kwa leo, wengine kesho. Na mkumbuke hata polisi na JWTZ wanapanda kibabe tu wala makonda hawapendi lkn wanaogopa kinachoweza kuwatokea. Nadhani serikali kama ina nia njema wawawekee posho ya usafiri kwenye pay rolls.
 
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni amesema yupo kwenye mpango wa kuwezesha walimu kusafiri bure kwenye daladala kwenda kazini kama njia ya kuwasaidia kuwahi na kuwapunguzia makali ya maisha.

Makonda ameyasema hayo wakati wa hafla ya kumuaga mke wa Rais mwl Janet Magufuli ambaye amekiri kuwa kwa sasa ana majukumu mengi hasa ya kumsaidia mheshimiwa Rais.

Sasa hapa najiuliza hawa wamiliki wa magari watakubali? Na je walimu watakuwa na unifomu au watalazimika kila wakati kuonesha vitambulisho? Na je hilo litakuwa suluhisho la kudumu? Na je watumishi wengine wao watajisikiaje ? Source Azam tv- habari ya saa 2 usiku.

Mkuu hizi ni siasa tu hakuna kitu;
 
Sioni namna ya waalimu kusafiri bure na wala hakuna sababu.

Hata hivyo, katika mfumo wa kisasa wa mtandao wa usafiri ambamo mtu anaweza kukata tiketi hata ya mwezi mzima au muhula mzima. Kama DART wana mfumo wa kisasa wa kukata tiketi hili linawezekana. Maana yake ni kwamba Makonda kwa kushirikiana na uongozi wa halmashauri ya wilaya ya kinondoni wanaweza kutenga fungu kwa ajili ya kulipa DART/UDA ili waalimu wenye tiketi hizo za kipindi fulani wasafiri bila shida.

Bure haiwezekani kabisa; siku zote yuko anayelipia gharama. Kama Makonda mpaka leo hajui kuwa hakuna huduma za bure basi sijui namna JPJM anaweza kumbeba.
You are a great thinker! ni kweli kwamba hakuna huduma ya bure lazima kuna mtu mahali fulani anailipia. sasa kuwa na mpango wa kuwalipia walimu nauli kwenda na kurudi kazi inawezekana kwa kuweka mipango thabiti kama kuongea na makampuni yatakayo wasafirisha kisha wakalipwa baada ya kutoa huduma.Siyo lazima kila kitu tuige kwa wenzetu, vingine sisi wenyewe tunaweza kuvianzisha na wengine wakatuiga kama vinafanyakazi vizuri. kujenga nyumba karibu na shule kwasasa ni jambo gumu kwani shule nyingi hazina maeneo lakini pia walimu ni wengi sana mathalani unaweza kukuta shule moja ina walimu zaidi ya 100! kujenga nyumba hizo unahitaji fedha nyingi na eneo kubwa sana.

kuna watu wana kuja na hoja kwamba kwanini walimu pekee na siyo manesi, madaktari n.k., ukweli ni kwamba hapa duniani baada ya wazazi wako anaye fuata kwa malezi ya kila binadamu ni mwalimu. walimu ndio wanao elekeza Taifa la baadae liwe na muelekeo gani.Nchi yenye walimu walio kata tamaa na legelege haliwezi kuwa na maendeleo.Kiongozi mbunufu asibezwe bali tumsaidie kulifanya wazo lake kuwa bora zaidi.Hongera makonda umeonesha njia, wewe ni mbunifu.
 
SHIDA Kubwa Ya Viongozi Ambao Ni WATEULIWA Wa RAIS, Muda Huu Wanakurupuka Tu Hovyo, Ili Mradi Waonekane Na ANAYETUA Kama Nao Wapo Na Wanafanya Kazi!!! MATOKEO Yake Ndio Haya Sasa, Ni Kukurupuka Tu!! IKIWA Wanafunzi Wetu, Ambao Wamiliki Na Wanaoendesha BIASHARA Ya Daladala, Wameridhia Kuwasafirisha Kwa Nusu Ya Nauli Ya Mtu Mzima, Japo Kwa Shingo Upande Na Malalamiko Lukuki, Tunawaona Wanavyoteseka VITUONI Na Ndani Ya Mabasi Hayo!!! LEO Uje Kuwaongezea Na WAALIMU Wao, TENA Wao Wawe Wanasafiri Bure Kabisa!!!! KWANZA Wenye Hayo Mabasi HAWATAKUBALI Hata Kwa FFU Na Mabomu Yao!!!! LABDA Kwa Yale Ya MWENDOKASI Yao!!! YAANI Polisi, Mwanajeshi Ni BURE, SASA Wao Wanalipa Wakiwa Out Uniform Na Bure In Uniform!!! JE, Hao WAALIMU Watakuja Na Uniform Au Vitambulisho!!!!?? KAMA Ni Hivyo, SERIKALI Yake INATAKA Kuwapungizia WAALIMU Adhabu Ya USAFIRI, Basi Ifanye Vitu 3 Muhimu, Walau Kimoja Tu Ili Kuwapumbaza Hao WAALIMU Wao!! KWANZA, Wanunue Mabasi MAALUM, Ambayo Yatakuwa Yanatoa Hiyo Huduma Kwa WAALIMU Hao, Hizo Staff Bus Ziwe Chini Ya Ama TAMISEMI, MANISPAA Au WIZARA YA ELIMU!! PILI Wawajengee NYUMBA Za KUISHI Ktk Maeneo Ya MASHULE Au Jirani, Ili Kuwaepusha Na Hiyo Adha!!TATU Wawalipe Transport Allowance, Ambayo Itawazesha Kutumia Usafiri Wowote, Ama Wakopesheni Walau Mapikipiki Yao Binafsi Au Magari!! KAMA Taasisi Nyingine Wafanyavyo!!! KAMA Kweli SERIKALI Ya Makonda Inawajali Na Kuwathamini Waalimu Wao!!!! OTHERWISE Ni Propaganda Na Kukurupuka Tu, Na Kuota Ndoto Za Mchana Wakiwa Macho MAKAVU!!!!
 
Makonda mbunifu, tumpe mda kabla yakuponda
Ubunifu upi? kama angekuwa mbunifu si angenunua magari yake yatoe huduma hiyo kwani ni wazi wanafunzi wanatozwa nauli halafu eti walimu wasafirishwe bure hayo magari ya baba yake? Ni wazi ukurupukaji unaendelea kwa hawa wateule wa Magufuli na sidhani kama tutafika salama.
 
The man has an idea. Ila tumeshauri sana, hakuna haja ya walimu kusafiri bure. Jaman kuna nyumba za national housing zilizo karibu na shule au umbali mfupi tu kwa kwenda shuleni, kwann isifanyike reallocation walimu wakakaa hapo badala wa wahindi ambao hawatoi huduma kama public servant? Mfano pale buguruni na manespaa ya ilala kuna shule hapo hapo kuna national housing toa raia wale weka walimu na wakbaini maeneo yote yenye fursa hizo biashara imekwisha. kupanda bure gari tumelipia TRA, load lience, mwarabu n.k? Usifanye tuanze kudharirishwa aiseh
 
Solution ni kuhakikisha mwalimu anaishi karibu na anapoishi. Hizi zingine sinema tu. Haileti maana mwalimu anaishi Kibamba halafu anafundisha Kigamboni. Hata watoto wangeweza kusoma wanakoishi tungekuwa na nafuu sana ya foleni. Sasa hivi Shule zikifungwa tu barabara nyeupe
 
The man has an idea. Ila tumeshauri sana, hakuna haja ya walimu kusafiri bure. Jaman kuna nyumba za national housing zilizo karibu na shule au umbali mfupi tu kwa kwenda shuleni, kwann isifanyike reallocation walimu wakakaa hapo badala wa wahindi ambao hawatoi huduma kama public servant? Mfano pale buguruni na manespaa ya ilala kuna shule hapo hapo kuna national housing toa raia wale weka walimu na wakbaini maeneo yote yenye fursa hizo biashara imekwisha. kupanda bure gari tumelipia TRA, load lience, mwarabu n.k? Usifanye tuanze kudharirishwa aiseh


Mkuu kumbuka hata hizo nyumba za NHC zinaendeshwa kibiashara, kwa mfano nyumba kila nyumba kwa mwezi mpangaji analipa sio chini ya sh laki 2. Lakini mwalimu anashindwa kulipa nauil ya shilingi wangalau 120,000 kwa mwenzi, sasa huoni kama utaenda kumtoa anayelipa laki 2 na kumleta anayetaka asamehewe 120,000 itakuwa majanga makubwa kwa hilo shirika?
 
Povu lanini mkuu, relax haiwezekani unachofikiria wewe ndo sahihi. Tumpe mda au tumshauri namna nyingine yakufanikisha coz nchi hii yetu sote bila kujali vyama
hongera kwa point maridhawa hii. watu wengine toka wajue duniani kuna upinzani basi wao watapinga kila kitu ilimradi tu kiwe kimetolewa na upande usio wake. kimsingi Nchi hii ni yetu sote.hata walimu siyo wote ni ccm ila Makonda ameamua kuwajali kama kundi muhimu sana kwenye jamii yetu.kumwambia amekurukupa haikusaidii wewe wala Makonda.toa wazo mbadala ambalo linaleta workable solutionhapo utakuwa umelisaidia Taifa.
 
Hii itakuwa motisha au kumdhaalilisha mwalimu?Hebu fikirieni vizuri hili wazo.Walimu wajiandae kupachikwa majina ya hovyo hovyo na kudharaulika.
Unamsaidia mwalimu kwa kumuumiza mwenye gari. kwa nini msaada usitoke kwa mwenye kutaka kuutoa?
 
Labda awalipie sababu hata askari wanatakiwa walipe cose hakuna gari yyte inasamehewa kodi
 
Back
Top Bottom