Barbarosa
JF-Expert Member
- Apr 16, 2015
- 22,584
- 27,838
Mbona ulishajibiwa ndugu?. Katiba iko wazi kwa hicho nilichosema usome na ni jambo linahusu kinga aliyo nayo. Ni mimi nimeshindwa jibu swali au wewe umeshindwa elewa?.
Pia mimi nimejibu na nikatoa way forward. Wewe unazungumziaje hilo?. Maana umekazania yuko juu ya sheria. Lakini hujui kuwa rais wa nchi anaongozwa na katiba?, je hujui kuwa kiongozi wa nchi ana immunity?. Je ni kweli katiba unaisoma au tunaandika tu kwa kile tulicho sikia bila kusoma katiba yenyewe?.
Ndiyo maana inatuwia ugumu sana. Mfano katiba ya sasa wengi hawaijui, hiyo mpya tuitakayo tunaitoa kwenye misingi ipi?.
Vyema tusome. Lakini tusijifunge ufahamu wetu kwa kuangalia leo. Tuitazame kesho pia. Leo tunaongozwa na viongozi ambao kwa namna moja ama nyingine wanafuata katiba.
Je kesho tunajua atakaye tuongoza?, tunajua atatumiaje madaraka aliyo pewa na katiba ya sasa?. Katika hili usiangalie chama.
Ni jamii gani Dunia hii watu husoma Katiba ukiachia wale ambao wanautumia kwenye shughuli zao? Sijawahi kukutana na mtu yoyote yule Dunia hii akisoma Katiba!