Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 10,129
- 35,153
Upeo wako wa mambo ya kiimani uko chini sana. Umeandika upotofu kwa 99%.Salaam, Shalom!!
UTANGULIZI.
Ndani ya nyumba zetu, Pana mijusi yenye RANGI nyeupe tofauti na mijusi wa nje. Na KAZI ya mijusi KIMWILI Huwa ni kutafuta na kula WADUDU watambaao na warukao nk nk.
MADA: MAKINIKA NA MIJUSI/ UPANDE WA PILI WA MIJUSI YA NDANI YA NYUMBA.
Kuna mjusi alikuwa akiishi ndani ya nyumba yetu, na tulimchukulia kawaida tu kama mijusi wengine. Tukiwa sebuleni utamuona juu katulia tulii anatuangalia,
Tukiingia chumbani, yupo, Kuna time tulitilia mashaka ,lakini sababu hatukuwa na HAKIKA kuwa Si mjusi wa kawaida, tulipuuza.
Siku moja tumelala, usiku, nikajikuta kwenye vita kubwa sana katika Roho, nilikuwa napambana na mijusi wakubwa sana, mijusi giant ambao nilikuwa napambana nao Hadi JASHO linanitoka,
Nilikuwa nakemea, Kwa Jina la YESU, Damu ya Yesu, vita ilikuwa Kali sana, nilijiuliza kwanini Leo vita imekuwa Kali sana tofauti na vita za siku zingine, niliemdelea kukemea.
Nikiwa katika vita nikashtuka na kuamka, kumbe, mke wangu pia alikuwa akipambana vita kama yangu nae aliposhtuka tukaanza kuulizana nini kilikuwa kinatokea,
Tulijiuliza labda ni wachawi walikuwa wametuvamia, tulipowasha taa, tulishangaa sana kumkuta mjusi ambaye alikuwa akikaa juu ya dari, ameingia ndani ya neti yetu ametulia pembeni mwa Kuta ya Net. Baada ya kumvizia tumuue, alituponyoka na kukimbia.
Tangu siku hiyo, Niko makini sana na mijusi wa aina hiyo ndani ya nyumba na WADUDU wenye kutilia mashaka sababu mijusi wanaweza kutumiwa kama Antenna za kichawi. Yaani unarushiwa makombora Toka kuzimu kupitia mjusi au paka au mbwa au mdoli uliyenunua au kumfuga mwenyewe!!
Pia mijusi ndani ya nyumba wanaweza kukaribisha mapepo ambayo yanaweza kushambulia kupitia mwili wa mjusi.
Pepo halina mwili, hivyo likipata mdoli au kinyago ndani ya nyumba Yako, hupata Mahali pa kukaa na kukushambulia Kwa karibu na nguvu zaidi. Vita ya Wana wa Mungu ni katika Ulimwengu wa Roho, Vita zetu huanzia Rohoni kabla ya kuja mwilini.
SOLUTION.
1. Hakikisha huweki vinyago, midoli ndani ya nyumba. Mapepo yanaweza kuingia ndani ya vinyago na ukapata vita direct Kutokea vitu hivyo.
2. Acha mara Moja kufuga paka na kuishi naye ndani ya nyumba, paka au mbwa, Pepo anaweza kuwaingia na akawatumia kukuattack.
3. Puliza dawa ya kuua mijusi na WADUDU ndani ya nyumba, maana nyumba ya kuishi haipasi kuwa makazi ya chawa, mende, kunguni, viroboto, mijusi ,panya nk nk.
NB: Si mijusi wote ni kama niliyepambana nae Mimi, ni kukupa tu tahadhari kutokupuuzia mambo!!
ANGALIZO: Usilale bila kufanya maombi, funga milango Yako Kwa Damu ya Yesu, zungusha ulinzi katika anga lako na ardhi unayomiliki.
Ikiwa hujaokoka fuatisha Sala hii:
EE MUNGU KATIKA JINA LA YESU KRISTO, NINAKUKIRI WEWE KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE, NINAOMBA UNISAMEHE, ULIFUTE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU, ULIANDIKE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA UZIMA. NINAOMBA UWEZO WA KUSHINDA DHAMBI, NIWEZESHE NIISHI MAISHA MATAKATIFU. Amen
Mungu akubariki.
Amen
Nitachambua hapa hapa.
1. Mapepo, uchawi, vimbwengo nk ni roho, hakuna namna yoyote ile vinaweza kumuathiri mtu yoyote pasipo kuhusianisha imani. Kama wewe unaamini katika Mungu (Yesu Kristo) maana yake hakuna chochote kinaweza kukudhuru wala kukugusa. Ni very automatic phenomenon.
2. Damu ya Yesu ilimwagika msalabani mara moja tu na kutukomboa na kila kitu katika ulimwengu wa kiroho. Hatuhitaji tena kufanya chochote, ni suala la sasa kutambua tu hilo lilishafanyika na kuamini na kukiri hivyo tu. Basi automatically kile kilichofanyika msalabani kinakwenda kufanya kazi kwetu kwa 100%.
3. Kitu chochote kile (kilicho hai au kisicho hai) kinaweza kutumiwa na mapepo (shetani) na kitu chochote kile (kilicho hai au kisicho hai) kinaweza kutumiwa na Mungu. Kama Ibilisi alimtumia nyoka kwenda kumlaghai Hawa kwenye bustani ya Eden, Mungu pia kupitia Musa naye akamtumia nyoka kuleta ukombozi na uponyaji kwa wana wa Israel. Tusikariri.
4. Viumbe vyote kiasili viliumbwa na Mungu, na tangu vinaumbwa mbele ya Mungu vilikuwa vizuri kwa 100%. Kuanzia Paka, mbwa, Mijusi nk.
5. Ndoto ni ndoto tu, tafsiri ya ndoto ni kitu tofauti kabisa. Ikiwa kila tunachokiota tutakitafsiri hivyo hivyo kilivyo, basi tutaishia kuchukiana, kuuana, kuchanganyikiwa nk.
Mwisho kabisa, kiumbe cha hatari zaidi na kinachotumiwa na shetani mara kwa mara kuangamiza watu ni BINADAMU, hususani wale unaowaamini na kuwa karibu nao kuanzia mkeo/mumeo, mtoto wako, rafiki yako nk. Kama unaogopa sana kusambaratishwa na shetani basi ishi mwenyewe tena huko porini kabisa!