Makato kwenye mshahara wangu

Makato kwenye mshahara wangu

blind fighter

Member
Joined
May 17, 2021
Posts
85
Reaction score
128
Habari wakuu.

Mnamo wa mwaka jana mwezi wa nne nilipata kazi kwenye kampuni moja hivi, tulikubaliana kiasi cha mshahara take home itakuwa 500K. nilivoanza, nilikuwa napokea cash kwa accountant bila makato yoyote.

Yaani ilikuwa hiyo 500k hadi mwezi December. Nilikuwa situmii bank, na hawakunipa mkataba wowote. Wala mwongozo wowote wa makato. Nimeendelea hivo hadi mwaka jana mwezi wa 12. Sasa kutokana na usumbufu wa yule accountant kunizungusha kwenye kutoa hela kwa wakati, nikaona nitumie bank account kupokea hela, na alisema nitaanza kuwekewa hela kwenye account kuanzia January hii..

Mshahara ulivoingia, nimekuta wamekata takribani 85,400, bila maelezo yoyote, hamna deni lolote ninalodaiwa na kampuni. Na hamna mkataba wowote niliopewa unaoonesha makato. Hii imekaaje wakuu.

Kwa sasa nimesafiri sijarudi ofisini na wala sijapiga simu kuulizia.
Sasa. Naombeni ufafanuzi kwa wanaojua nisipanik bure
 
Habari wakuu.
Mnamo wa mwaka jana mwezi wa nne nilipata kazi kwenye kampuni moja hivi, tulikubaliana kiasi cha mshahara take home itakuwa 500K. nilivoanza, nilikuwa napokea cash kwa accountant bila makato yoyote. Yaani ilikuwa hiyo 500k hadi mwezi December. Nilikuwa situmii bank, na hawakunipa mkataba wowote. Wala mwongozo wowote wa makato. Nimeendelea hivo hadi mwaka jana mwezi wa 12. Sasa kutokana na usumbufu wa yule accountant kunizungusha kwenye kutoa hela kwa wakati, nikaona nitumie bank account kupokea hela, na alisema nitaanza kuwekewa hela kwenye account kuanzia January hii..

Mshahara ulivoingia, nimekuta wamekata takribani 85,400, bila maelezo yoyote, hamna deni lolote ninalodaiwa na kampuni. Na hamna mkataba wowote niliopewa unaoonesha makato. Hii imekaaje wakuu.
kwa sasa nimesafiri sijarudi ofisini na wala sijapiga simu kuulizia.
Sasa. Naombeni ufafanuzi kwa wanaojua nisipanik bure
Au ulijiunga na bima? Wamekata juu kwa juu
 
Rudi kazn acha kibri! Ukisharudi tenga muda kaongee na accountant wako.... pengine unakatwa Nssf, bima ama whatever....

Kazi ngumu wazee, usisuse
 
Tafuta wakili mzuri wafungulie kesi wamekata hela nyingi sana hao jamaa au ulizinguana nao
Sijazinguana nao, na bado nipo nafanya nao kazi. Mkataba wowote sijapewa, hamna makato yoote yaliyokuwa yakikatwa. Najiuliza, au ndo wameanza kukata PAYE na NSSF? na hii inawezekanaje labla sijapewa mkataba wakuu? Yawezekana wapo sahihi mimi ndo sijui, lakini inawezekana bila kuambizana?
Rudi kazn acha kibri! Ukisharudi tenga muda kaongee na accountant wako.... pengine unakatwa Nssf, bima ama whatever....

Kazi ngumu wazee, usisuse
Nakuelewa mkuu wangu. Kazi sijasusa, na nipo huku kwa makubaliano yangu na ofisi.
Sijawahi lipia NSSF, sina BIMA. in short ni kwamba, toka mwaka jana mwezi wa 4 hadi wa 12, sijawahi katwa chochote.. nashangaa mbona ghafla
 
Itakuwa ni faini ya kulalama sana huyo jamaa alimaindi kusikia hakulipi kwa wakati.
 
Mkuu badala ya kuongea na muajiri wako unakuja kuwauliza wana JF?

Ongea na kampuni yako ili upate uhakika wa hayo makato,
Humu utapata kila aina ya majibu but yatakua ni majibu ya kubahatisha tu,
Mwenye jibu sahihi la swali lako ni muajiri wako.
 
Habari wakuu.

Mnamo wa mwaka jana mwezi wa nne nilipata kazi kwenye kampuni moja hivi, tulikubaliana kiasi cha mshahara take home itakuwa 500K. nilivoanza, nilikuwa napokea cash kwa accountant bila makato yoyote.

Yaani ilikuwa hiyo 500k hadi mwezi December. Nilikuwa situmii bank, na hawakunipa mkataba wowote. Wala mwongozo wowote wa makato. Nimeendelea hivo hadi mwaka jana mwezi wa 12. Sasa kutokana na usumbufu wa yule accountant kunizungusha kwenye kutoa hela kwa wakati, nikaona nitumie bank account kupokea hela, na alisema nitaanza kuwekewa hela kwenye account kuanzia January hii..

Mshahara ulivoingia, nimekuta wamekata takribani 85,400, bila maelezo yoyote, hamna deni lolote ninalodaiwa na kampuni. Na hamna mkataba wowote niliopewa unaoonesha makato. Hii imekaaje wakuu.

Kwa sasa nimesafiri sijarudi ofisini na wala sijapiga simu kuulizia.
Sasa. Naombeni ufafanuzi kwa wanaojua nisipanik bure
Sehemu sahihi ya kupata maelezo ni kwa huyo accountant. Huku hutapata majibu sahihi
 
Back
Top Bottom