Baba Mungu Mwenyezi tunakushukuru sana kwa wema wako unaotutendea siku hadi siku,asante kwa kutuamsha salama na kutupa uzima na afya njema,tunaomba utusamehe makosa yetu tuliyokukosea kwa mawazo ,maneno,matendo tunaomba utusaidie tuwe na upendo na uvumilivu katika maisha yetu kila siku tunawaombea wagojwa,wafiwa,wenye shida mbalimbali,wazazi,watoto,vijana wasafiri wape kukutegemea wewe tu,wasipungukiwe..bariki kazi za mikono yetu ,utafutaji utubariki tuingiapo na tutokapo,Asante Bwana Yesu maana utatenda sawa na mapenzi yako Amen
1 Nyakati 23
30 Nao wasimame kila asubuhi kumshukuru na kumsifu BWANA na jioni pia

Tunapaswa kumshukuru BWANA MUNGU wetu kila wakati.

Haijalishi tunapiti changamoto gani.

Tumshukuru kuashwa salama sio kwa uwezo wetu.

Tumshukuru kwa riziki na neema anazotupatia peke yetu hatuwezi.

Tumshukuru ametupa marafiki wema,ndugu hata mahali hapa MAKAPUKU tunapokutana na kufurahi ni Upendo wake.

Hata tukipungukiwa tushukuru maana ni kwa muda tu ,atatuinua tena.
ASANTE MUNGU KWA YOTE UNAYOTUTENDEA.
Muwe na siku njema mbarikiwe