1994 - Wakala wa CIA, Aldrich Ames na Mkewe wanashtakiwa na Serikali ya Marekani kwa kosa la kukubali kuuza siri za Nchi hiyo na kufanya kazi shirika la Ujasusi la Urusi KGB.
Aldrich Ames baada ya miaka 31 ya utumishi wake ndani ya CIA alijikuta akiwa " Double Agent " wa KGB jambo ambalo ni kosa la jinai.
Kwasasa anatumikia kifungo cha Maisha katika gereza lenye ulinzi mkali la Allenwood.
2002 - Kiongozi wa waasi nchini Angola, Jonas Savimbi anauwawa.
Aliuwawa baada ya mapambano makali kati yake na majeshi ya Serikali ambapo Savimbi alipigwa risasi 15 kichwani na kifuani hali iliyopelekea kupoteza maisha papo hapo.