Makapuku Forum

Huyu nae alikuwa kichwa hatari
 
4.Fyodor Dostoevsky;


(11 Novemba 1821 (30 Oktoba ya Kalenda ya Juliasi) – 9 Februari 1881 (28 Januari ya kalenda ya kale) alikuwa mwandishi wa riwaya nchini Urusi. Mara nyingi ametajwa kama mwandishi Mrusi muhimu zaidi. Kati ya riwaya zake zianzojulikana kimataifa ni "Kosa na adhabu" pamoja na "Ndugu Karamasov".

Dostoyevski alizaliwa katika familia ya makabaila maskini babake alikuwa mganga. 1838-1843 alisoma uhandisi kwenye chuo kikuu cha kijeshi mjini Sankt Peterburg. 1839 alipata habari ya kwamba baba aliuawa na wakulima waasi alipokaa kwenye shamba lake. 1844 Fyodor alianza kutunga riwaya yake ya kwanza "Watu Maskini" iliyopokelewa vizuri na kuweka msingi wa kwanza kwa umaarufu wake.

1847 Dostoyevski alishiriki katika kundi la wanamapinduzi akakamatwa na kupewa adhabu ya kifo akasamehewa na Tsar Nikolai I na badala yake akapewa adhabu ya kufanya kazi nzito kwa muda wa miaka minne huko Siberia. Baadaye alipaswa kujiunga na jeshi hadi 1859.

Aliendelea kuandika na riwaya ya kwanza iliyopokelewa pia kimataifa ilikuwa "Kosa na Adhabu"iliyohusu kijana aliyekuwa mwuaji lakini baadaye anaanza kutambua dunia upya. Uwezo wa Dostoyevski wa kuonyesha roho na saikolojia ya watu ulionekana bora katika riwaya hii.

Kibinafsi Dostoyeski alipambana na hamu ya kucheza kamari iliyomsababisha kuwa na madeni makubwa.

Riwaya yake ya mwishi ilikuwa "Ndugu Karamasov" ambayo alishindwa kuimaliza.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…