Makapuku Forum

NUKUU NO 1#

Nadhani tunaangushwa na viongozi wetu na wasomi wetu

Wamefikia mahari wanafikiri mwananchi hajui chochote,
Yeye ni wa kuelimishwa tu

Viongozi ndio wanaohitaji kuelimishwa kutokana na mawazo ya wananchi

Kweli tuna mapungufu, yaani nchi hii imefika mahali mtu anaona aibu kujivunia nchi hii.

Haya yalisemwa dar es salaam, Mei 12,2008 na waziri mkuu wa zamani Jaji Joseph Sinde Warioba.
Aliyatamka maneno hayo kwenye mahojiano na waandishi wa habari, akijibu baadhi ya shutuma kwa watawala kwamba maoni aliyokuwa ameyatoa awali kuhusu mwafaka wa CUF na CCM yalikuwa niya kukurupuka
 

Huyu babu alifanyiwa uhuni na Makondakta
..................
 
NUKUU NO 2#

Katika Dunia yetu hii, namna tunavyofurahia vitu na namna tunavyovichukia Kuna uhusiano wa moja kwa moja na ubora wa utashi, uadilifu na hulka zetu binadamu.


Haya yalisemwa na mwanafalsafa wa kale wa Ugiriki Aristotle
Mwanafalsafa huyo alizaliwa mwaka 384 BCE huko stagira, Macedonia ya kale.

Inaaminika kuwa Aristotle alikuwa mfuasi mkubwa wa mafundisho ya Plato kabla ya kujiondoa na kujenga fikra na mitazamo yake mwenyewe
 

Words never die
...........
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…