Kitombise
JF-Expert Member
- Sep 24, 2013
- 8,652
- 25,849
SEHEMU YA NNE
SEHEMU YA NNE
KILICHONISAIDIA ni uenyeji wangu katika mitaa ile, niliongeza kasi na kisha nikapinda mkono wa kushoto ghafla na baada ya hatua mbili nikayumba kulia na hapo nikakutana na kichochoro kingine na kwa mbali ulikuwa ni uwanja wa mpira. Uwanja ambao zilizuka vurugu siku kadhaa nyuma na kunikutanisha na Ezekiel na sasa nipo katika balaa.
Kulikuwa na wachezaji uwanjani wakiwa katika mazoezi, nikaona hiyo ni nafasi ya kipee ya kupata wasaidizi. Nikaanza kupiga mayowe kwa jitihada zote huku nikipepea mikono juu.
Kumbuka nilikuwa kifua wazi!! Wanasoka wale wakabaki kunishangaa mimi huku wengine wakisogea nyuma na pembeni kwa tahadhari ya lolote baya ambalo nilikuwa nakabiliwa nalo.
Walinipokea huku wakisubiri kuona ni kitu gani kinanifanya nirukwe akili vile.
“Majambaziii majambaziiii…..” nililalamika huku pumzi zikikata na hofu ikitanda zaidi.
Kusikia neno majambazi, tahadhari kubwa zaidi ikachukuliwa kila mmoja akawa katika mkao wa kujiokoa mwenyewe. Macho yakatazama pande kuu nne za dunia lakini hakuna kilichotokea. Umakini ukaongezeka hadi wa kutazama pande zote kumi na sita, thelathini na mbili na hadi sitini na nne. Hapakuwa na kitu chochote cha hatari kilichojongea pale uwanjani.
“Huyu chizi huyu labda…” mchezaji mmoja akatoa hoja hiyo. Wenzake wakamkanya na hapo wakamtambulisha kuwa mimi ni mwandishi wa habari katika gazeti fulani. Licha ya yeye kuduwaa, mimi niliduwaa maradufu. Kumbe najulikana sana.
Yule aliyetoa shutuma za kuwa mimi nina wazimu akagwaya!! Akaungana na wenzake kuendelea kungoja hayo majambazi.
Bado hayakutokea!!
Wakaanza kupungua mtu mmoja baada ya mwingine, nikahisi vichwani mwao wamekubaliana na wazo la yule mwenzao kuwa huenda nimepandwa na wazimu.
Hatimaye nikabaki peke yangu, kifua wazi!! Kifurushiu mkononi. Kila mmoja akaendelea na shughuli zake, hakuna ambaye alikuwa tayari kuniamini.
Nikiwa kifua wazi nikalazimika kuendelea kukimbia maana niliamini kuwa wale watu wabaya walikuwa wakinifuatilia.
Nilitembea kwa tahadhari huku nikiamini kuwa watu kadhaa waliokuwa wananifahamu walikuwa wakinishangaa. Nilipenya nyumba kadhaa hatimaye nikafika nyumbani kwa Enock, rafiki yangu ambaye kabla ya kuhamia kwake ni mimi nilimkaribisha jijini na akaishi nami chumba kimoja kabla sijaamua kuishi na mama Eva.
Nilimkuta mnkewe yeye alikuwa ametoka kidogo. Mke wake ambaye ni shemeji yangu alishtuka kuniona katika ile hali, nikiwa katika pensi na mkononi kifurushi kikiwa na makaratasi ambayo ni mimi pekee niliamini yalikuwa yana umuhimu.
Shemeji alinikaribisha ndani huku macho yake yakikwepa mara kwa mara kunitazama.
“Shem…hebu mwambie Enock akatishe zoezi la kuoga aje kunisikiliza” shemeji akaruka upesi na kuelekea bafuni, hakurejea tena badala yake Enock akiwa amevaa taulo alitokea sebuleni.
“Kaka nini tena hiki….kimetokea nini…mama Eva ama?? Yaani mmefikia huku.” Alizungumza upesiupesi asinipe nafasi ya kusema lolote, nikaamua kumkatisha, “Noki eeeh!! Hebu nisikilize bwana…..” nilifoka kisha nikamsimulia kwa ufupi kuwa haja yangu ya kwanza ilikuwa nguo. Hilo hapakuwa na utata, miili yetu iliendana hivyo ningeweza kuvaa nguo zake.
Akanitimizia hilo mara moja nikavalia palepale sebuleni. Na baada ya pale nikamwomba anipatie kiasi fulani cha pesa, uzuri ulikuwa mwisho wa mwezi na alitambua ni fadhila kiasi gani nimewahi kumtendea. Nikamtajia kiasi akaniahidi kunipa kiasi chote kama nilivyoomba.
“Mengineyo nitakupigia simu uje mahali tukae tuzungumze, hapa si mahali sahihi hata kidogo. Kuna watu wabaya wasije wakazua lolote la kuzulika.
Enock hakunielewa kabisa lakini hakuwa na la kufanya, nilikuwa nimefedheheka na akili yangu ilikuwa haijakaa mkao wa kusimulia juu ya Ezekiel kisha mazingaombwe ya kumuona akiwa Ubungo hai na kisha akiwa maiti anayeharibika kitandani baada ya nusu saa, mkasa wa mke wangu kuchukuliwa kisha kuachwa ujumbe, mkasa wa Selemani yule mtoto kukwapuliwa na watu wabaya kisha kuanza kunifukuza mimi. Ningeweza vipi kusimulia tukio lote kwa ufasaha wakati shemeji yangu alikuwa ameniona nikiwa kama tahira tayari aliponikaribisha ndani.
Hakika sikuweza!!
“Enock….shemeji yako yupo matatani hadi sasa sijui alipo, tukionana hiyo jioni ama muda wowote ule uje unishauri. Sijui kama yupo mwingine wa kunishauri zaidi yako” nilimnong’oneza Enock kisha nikajivika vyema kofia aliyonipatia, kifurushi changu nikakiweka katika mpangilio mzuri, badala ya ule mfuko mweusi sasa niliyapanga makaratasi yale katika bahasha kubwa ya kaki.
Dereva wa pikipiki akapigiwa simu, akafika hadi mlangoni. Nikapanda pikipiki na kuagana na Enock mwenye mashaka.
“Nipeleke Ubungo maji.” Nilimpa maelekezo.
“Shilingi ngapi?” nilimuhoji.
“Jamaa amesema atalipia kila kitu cha msingi nikupeleke popote utakapoenda.” Alinijibu.
Kisha akavaa ngao ya kichwani na kutokomea.
Wakati huo ilikuwa tayari saa saba mchana!!!
Upepo uliovuma wakati pikipiki ikizidi kushika kasi, kidogo ulinipa ahueni ya kufikiri. Nilijiona mtu kati ya watu. Lakini mtu asiyekuwa mkamilifu!!
Mke wangu alikuwa matatani. Na hawa jamaa hawakusema naenda kumchukua wapi. Baadaye kidogo nikatabasamu baada ya kugundua kuwa kile ninachokiandika kila siku sasa kilikuwa kinanitokea. Maisha ya kwenye simulizi!!
Tulipofika Ubungo maji nilishuka na kumshukuru yule bwana.
Baada ya kuondoka nikachukua daladala iliyonipeleka maeneo ya kimara. Nilifanya vile ili kukwepa kupatikana kirahisi iwapo tu mambo yatakuwa makubwa zaidi ya pale.
Nilichukua chumba maeneo ambayo yalikuwa yamejificha sana. Nikajiandikisha jina la uongo na hatimaye nikawa chumbani huru.
Nilihisi uchovu lakini sikutaka kulala, nikafungua bahasha yangu. Kitu cha kwanza kukitoa ilikuwa ni picha ndogo ya mtoto wa kiafrika alikuwa anatabasamu. Haikuandikwa chochote kwa mbele lakini nyuma yake iliandikwa ‘MICHIGAN’.
Jina likanichanganya sana, hii Michigan ya bara la Amerika ama Michigani ni jina la yule mtoto katika picha. Na inahusu nini sasa picha hiyo!!
Nikabakli na swali kuu la kwanza, nikaiweka kando ile picha nikakutana na makaratasi mengine, moja lilikuwa na maandishi yaliyoandikwa na mtu ambaye anajifunza kuandika ama ni maksudi aliamua kuhadaa kwa namna ile. “THE DON 20 MKAKATI WA KUDUMU” Halikuandikwa neno jingine zaidi.
Makaratasi yalikuwa mengi sana na pia picha mbalimbali, nyingine nikamuona Ezekiel, alikuwa amekumbatiana na mwanaume wa kizungu, kwa namna walivyokuwa Ezekiel alionekana kama hapendi kushikwa vile lakini ilimlazimu tu. Katika picha ya mzungu paliwekwa alama ya ‘x’….hapakuwa na maelezo kwa nyuma.
Katika kila karatasi nilijaribu kubashiri majibu yangu lakini hata moja halikuonekana kuendana na ukweli wowote bambao ungeweza kunivusha hatua moja mbele.
Ina maana Ezekiel alikuwa analazimishwa kuwa alivyokuwa?
Nani alikuwa anamlazimisha?
Michigan? Ni kitu gani hiki?
Picha ya yule mtoto na yule mzungu aliyewekewa alama ‘x’ zinahusika vipi?
Haya yalikuwa baadhi ya maswali yaliyolundikana katika kichwa changu!!
Kabla sijamaliza makaratasi mengine, nilihisi njaa kali, hapa ni baada ya kusimama. Nilipoangalia saa ilikuwa saa kumi na mbili na nusu jioni. Nikakumbuka sikuwa nimekula kwa siku nzima.
Ahadi ya kukutana na Enock nayo ikawa imekufa, kwa sababu simu yangu ya mkononi niliiacha ndani wakati naenda kuoga na sikurudi tena kuichukua.
Nikajikongoja hadi nje na kufanikiwa kupata chakula. Nikala kwa kadri ya mahitaji yangu na kisha nikalipia na kurejea chumbani ambapo nilioga na kujaribu kujinyoosha kidogo. Usingizi ulipoanza kuninyemelea nikajiahidi kuwa nitalala kidogo na kisha kuamka, nipitie tena makaratasi yaliyosalia ili siku inayofuata niende polisi kisha nifike kazini pia kutafuta watu waelewa ambao wangeshirikiana nami katika mkasa huu wa ajabu ambao hadi wakati huo ulikuwa umenitia matatani.
Haikuwa kama nilivyojiahidi, nilikuja kushtuka majira ya saa saa kumi na mbili asubuhi. Kitu cha kwanza kusikia zilikuwa ni kelele zilikzokuwa zinapigwa na mwanamke, nilizisikiliza kwa makini nitambue kama kuna hatari yoyote eneo lile lakini nikang’amua kelele zile hazikuwa na wasiwasi wowote na wala hazikuelezea uchungu wowote na badala yake zilikuwa zinaelezea raha fulani na huyo aliyezipiga hakujua kama alikuwa anapiga kelele na kusumbua wengine ambao walikuwa wamelala tena peke yao.
Nikaghafirika na kuwashangaa wawili hao waliokuwa wakifanya mapenzi kwa raha zao na kutupigia kelel wengine.
Nikachukua rimoti na kuwasha luninga bila dhumuni lolote ilimradi tu kukwepa kuzisikia kelele za mwanamke yule ambaye kwa lugha moja ningeweza kusema hajastaarabika.
Nilisimama na kujinyoosha viungo kisha nikauendea mlango wa bafuni, nikaingia kwa ajili ya kujistiri na haja ndogo. Niliacha mlango wazi, sikuwa na shaka kwa sababu nilikuwa mwenyewe.
Nikiwa maliwatoni, nilisikia vitu ambavyo akili yangu ilinituma kuwa ni muhimu nivisikilize, upesi nikarejea chumbani na kukuta mtangazaji akizungumza juu ya habari fulani ya kuvutia.
“……mwandishi huyo ambaye alitimua mbio baada ya tukio anasadikiwa kufanya mauaji hayo kwa makusudi. Mwanamke aliyemshuhudia kwa jicho lake akitokea chumbani mwa marehemu anadai mwandishi alitimua mbio baada ya tukio hilo. Uthibitisho zaidi wa suruali yake ambayo ilisheheni simu ya mkononi ambayo imethibitika ni mali yake, pochi iliyokuwa na pesa taslimu laki tatu, katika suruali palikutwa pia na sumu kali ya kuulia wanyama. Jitihada za kumpata yeye na mkewe waliyekuwa wanaishi naye ziligonga mwamba. Hata hivyo mtoto wao mdo aliyejitambulisha kwa jina la Eva amehifadhiwa na jeshi la polisi Tanzania. Huku upelelezi wa kuhakikisha Samson Josephat na mkewe wanaingizwa nguvuni kwa kosa hilo la mauaji.” Alipomaliza kusoma habari hiyo, ilionyeshwa picha kwa ukaribu kabisa, ilikuwa ni suruali yangu, na pochi ilikuwa yangu lakini sumu na zile pesa hazikuwa mali yangu!!!
Na mbaya zaidi waandishi na maaskari wakaaminishwa kuwa nguo zile zimekutwa katika chumba cha Ezekiel.
“Mungu wangu..kwani yule dada hakuniona kuwa nilikuwa nimevaa suruali yangu na shati zuri kabisa!!” nilijiuliza kwa sauti kama kwamba kuna yeyote wa kushirikiana nami katika mjadala huu.
Wakati nawaza juu ya mchezo huu wa ajabu na mchafu kuwahi kunikumba nikaikumbuka kauli ya mwisho ya mtangazaji…”Mtoto wao mdogo aitwaye Eva…..”
Mapigo ya moyo yakapiga maradufu!!
Eva alinizoea mimi na mama yake tu!! Hakuna mtu mwingine ambaye angeweza kuishi na Eva.
Mtoto wangu jamani!! Nilijikuta katika manung’uniko na majuto wakati sijui najutia jambo gani!!
Mambo yalikuwa yameharibika.
Wakati nahangaisha kichwa changu kufikiria ni jambo gani sahihi natakiwa kufanya, habari ile ikaendelea, wananchi kadhaa walikuwa wakihojiwa juu ya tukio lile, macho yangu yakamwona yule mchezaji aliyeniita mwehu. Alizungumza kwa hisia kubwa sana akinishutumu kuwa alihisi tu kuna jambo baya nimefanya lakini wenzake wakampinga!!
Nilitaka kumpiga ngumi lakini nikakumbuka kuwa kile ni kioo, yeye hayupo pale.
Kwa siku ile sikuiona sura yangu ikirushwa kwenye luninga lakini ningejuaje labda vituo vingine walirusha picha yangu!! Hii ni hatari sana.
Mke wangu yupo wapi?? Hii ni hila ya watu wabaya kwa sababu nimewakimbia basi wamemuunganisha na mke wangu katika tukio mili kuunda ukweli, maana kwa kumwacha yule angenitetea mpaka tone lake la mwisho la damu.
Lakini hakuwepo tena!!
Safari ya kwenda kituo cha polisi kutoa taarifa ikaishia pale na sasa nikawaza mengine, lakini hata yenyewe hayakujiweka katika mkondo mahususi!!!
Nikapagawa!!!
SEHEMU YA NNE
KILICHONISAIDIA ni uenyeji wangu katika mitaa ile, niliongeza kasi na kisha nikapinda mkono wa kushoto ghafla na baada ya hatua mbili nikayumba kulia na hapo nikakutana na kichochoro kingine na kwa mbali ulikuwa ni uwanja wa mpira. Uwanja ambao zilizuka vurugu siku kadhaa nyuma na kunikutanisha na Ezekiel na sasa nipo katika balaa.
Kulikuwa na wachezaji uwanjani wakiwa katika mazoezi, nikaona hiyo ni nafasi ya kipee ya kupata wasaidizi. Nikaanza kupiga mayowe kwa jitihada zote huku nikipepea mikono juu.
Kumbuka nilikuwa kifua wazi!! Wanasoka wale wakabaki kunishangaa mimi huku wengine wakisogea nyuma na pembeni kwa tahadhari ya lolote baya ambalo nilikuwa nakabiliwa nalo.
Walinipokea huku wakisubiri kuona ni kitu gani kinanifanya nirukwe akili vile.
“Majambaziii majambaziiii…..” nililalamika huku pumzi zikikata na hofu ikitanda zaidi.
Kusikia neno majambazi, tahadhari kubwa zaidi ikachukuliwa kila mmoja akawa katika mkao wa kujiokoa mwenyewe. Macho yakatazama pande kuu nne za dunia lakini hakuna kilichotokea. Umakini ukaongezeka hadi wa kutazama pande zote kumi na sita, thelathini na mbili na hadi sitini na nne. Hapakuwa na kitu chochote cha hatari kilichojongea pale uwanjani.
“Huyu chizi huyu labda…” mchezaji mmoja akatoa hoja hiyo. Wenzake wakamkanya na hapo wakamtambulisha kuwa mimi ni mwandishi wa habari katika gazeti fulani. Licha ya yeye kuduwaa, mimi niliduwaa maradufu. Kumbe najulikana sana.
Yule aliyetoa shutuma za kuwa mimi nina wazimu akagwaya!! Akaungana na wenzake kuendelea kungoja hayo majambazi.
Bado hayakutokea!!
Wakaanza kupungua mtu mmoja baada ya mwingine, nikahisi vichwani mwao wamekubaliana na wazo la yule mwenzao kuwa huenda nimepandwa na wazimu.
Hatimaye nikabaki peke yangu, kifua wazi!! Kifurushiu mkononi. Kila mmoja akaendelea na shughuli zake, hakuna ambaye alikuwa tayari kuniamini.
Nikiwa kifua wazi nikalazimika kuendelea kukimbia maana niliamini kuwa wale watu wabaya walikuwa wakinifuatilia.
Nilitembea kwa tahadhari huku nikiamini kuwa watu kadhaa waliokuwa wananifahamu walikuwa wakinishangaa. Nilipenya nyumba kadhaa hatimaye nikafika nyumbani kwa Enock, rafiki yangu ambaye kabla ya kuhamia kwake ni mimi nilimkaribisha jijini na akaishi nami chumba kimoja kabla sijaamua kuishi na mama Eva.
Nilimkuta mnkewe yeye alikuwa ametoka kidogo. Mke wake ambaye ni shemeji yangu alishtuka kuniona katika ile hali, nikiwa katika pensi na mkononi kifurushi kikiwa na makaratasi ambayo ni mimi pekee niliamini yalikuwa yana umuhimu.
Shemeji alinikaribisha ndani huku macho yake yakikwepa mara kwa mara kunitazama.
“Shem…hebu mwambie Enock akatishe zoezi la kuoga aje kunisikiliza” shemeji akaruka upesi na kuelekea bafuni, hakurejea tena badala yake Enock akiwa amevaa taulo alitokea sebuleni.
“Kaka nini tena hiki….kimetokea nini…mama Eva ama?? Yaani mmefikia huku.” Alizungumza upesiupesi asinipe nafasi ya kusema lolote, nikaamua kumkatisha, “Noki eeeh!! Hebu nisikilize bwana…..” nilifoka kisha nikamsimulia kwa ufupi kuwa haja yangu ya kwanza ilikuwa nguo. Hilo hapakuwa na utata, miili yetu iliendana hivyo ningeweza kuvaa nguo zake.
Akanitimizia hilo mara moja nikavalia palepale sebuleni. Na baada ya pale nikamwomba anipatie kiasi fulani cha pesa, uzuri ulikuwa mwisho wa mwezi na alitambua ni fadhila kiasi gani nimewahi kumtendea. Nikamtajia kiasi akaniahidi kunipa kiasi chote kama nilivyoomba.
“Mengineyo nitakupigia simu uje mahali tukae tuzungumze, hapa si mahali sahihi hata kidogo. Kuna watu wabaya wasije wakazua lolote la kuzulika.
Enock hakunielewa kabisa lakini hakuwa na la kufanya, nilikuwa nimefedheheka na akili yangu ilikuwa haijakaa mkao wa kusimulia juu ya Ezekiel kisha mazingaombwe ya kumuona akiwa Ubungo hai na kisha akiwa maiti anayeharibika kitandani baada ya nusu saa, mkasa wa mke wangu kuchukuliwa kisha kuachwa ujumbe, mkasa wa Selemani yule mtoto kukwapuliwa na watu wabaya kisha kuanza kunifukuza mimi. Ningeweza vipi kusimulia tukio lote kwa ufasaha wakati shemeji yangu alikuwa ameniona nikiwa kama tahira tayari aliponikaribisha ndani.
Hakika sikuweza!!
“Enock….shemeji yako yupo matatani hadi sasa sijui alipo, tukionana hiyo jioni ama muda wowote ule uje unishauri. Sijui kama yupo mwingine wa kunishauri zaidi yako” nilimnong’oneza Enock kisha nikajivika vyema kofia aliyonipatia, kifurushi changu nikakiweka katika mpangilio mzuri, badala ya ule mfuko mweusi sasa niliyapanga makaratasi yale katika bahasha kubwa ya kaki.
Dereva wa pikipiki akapigiwa simu, akafika hadi mlangoni. Nikapanda pikipiki na kuagana na Enock mwenye mashaka.
“Nipeleke Ubungo maji.” Nilimpa maelekezo.
“Shilingi ngapi?” nilimuhoji.
“Jamaa amesema atalipia kila kitu cha msingi nikupeleke popote utakapoenda.” Alinijibu.
Kisha akavaa ngao ya kichwani na kutokomea.
Wakati huo ilikuwa tayari saa saba mchana!!!
Upepo uliovuma wakati pikipiki ikizidi kushika kasi, kidogo ulinipa ahueni ya kufikiri. Nilijiona mtu kati ya watu. Lakini mtu asiyekuwa mkamilifu!!
Mke wangu alikuwa matatani. Na hawa jamaa hawakusema naenda kumchukua wapi. Baadaye kidogo nikatabasamu baada ya kugundua kuwa kile ninachokiandika kila siku sasa kilikuwa kinanitokea. Maisha ya kwenye simulizi!!
Tulipofika Ubungo maji nilishuka na kumshukuru yule bwana.
Baada ya kuondoka nikachukua daladala iliyonipeleka maeneo ya kimara. Nilifanya vile ili kukwepa kupatikana kirahisi iwapo tu mambo yatakuwa makubwa zaidi ya pale.
Nilichukua chumba maeneo ambayo yalikuwa yamejificha sana. Nikajiandikisha jina la uongo na hatimaye nikawa chumbani huru.
Nilihisi uchovu lakini sikutaka kulala, nikafungua bahasha yangu. Kitu cha kwanza kukitoa ilikuwa ni picha ndogo ya mtoto wa kiafrika alikuwa anatabasamu. Haikuandikwa chochote kwa mbele lakini nyuma yake iliandikwa ‘MICHIGAN’.
Jina likanichanganya sana, hii Michigan ya bara la Amerika ama Michigani ni jina la yule mtoto katika picha. Na inahusu nini sasa picha hiyo!!
Nikabakli na swali kuu la kwanza, nikaiweka kando ile picha nikakutana na makaratasi mengine, moja lilikuwa na maandishi yaliyoandikwa na mtu ambaye anajifunza kuandika ama ni maksudi aliamua kuhadaa kwa namna ile. “THE DON 20 MKAKATI WA KUDUMU” Halikuandikwa neno jingine zaidi.
Makaratasi yalikuwa mengi sana na pia picha mbalimbali, nyingine nikamuona Ezekiel, alikuwa amekumbatiana na mwanaume wa kizungu, kwa namna walivyokuwa Ezekiel alionekana kama hapendi kushikwa vile lakini ilimlazimu tu. Katika picha ya mzungu paliwekwa alama ya ‘x’….hapakuwa na maelezo kwa nyuma.
Katika kila karatasi nilijaribu kubashiri majibu yangu lakini hata moja halikuonekana kuendana na ukweli wowote bambao ungeweza kunivusha hatua moja mbele.
Ina maana Ezekiel alikuwa analazimishwa kuwa alivyokuwa?
Nani alikuwa anamlazimisha?
Michigan? Ni kitu gani hiki?
Picha ya yule mtoto na yule mzungu aliyewekewa alama ‘x’ zinahusika vipi?
Haya yalikuwa baadhi ya maswali yaliyolundikana katika kichwa changu!!
Kabla sijamaliza makaratasi mengine, nilihisi njaa kali, hapa ni baada ya kusimama. Nilipoangalia saa ilikuwa saa kumi na mbili na nusu jioni. Nikakumbuka sikuwa nimekula kwa siku nzima.
Ahadi ya kukutana na Enock nayo ikawa imekufa, kwa sababu simu yangu ya mkononi niliiacha ndani wakati naenda kuoga na sikurudi tena kuichukua.
Nikajikongoja hadi nje na kufanikiwa kupata chakula. Nikala kwa kadri ya mahitaji yangu na kisha nikalipia na kurejea chumbani ambapo nilioga na kujaribu kujinyoosha kidogo. Usingizi ulipoanza kuninyemelea nikajiahidi kuwa nitalala kidogo na kisha kuamka, nipitie tena makaratasi yaliyosalia ili siku inayofuata niende polisi kisha nifike kazini pia kutafuta watu waelewa ambao wangeshirikiana nami katika mkasa huu wa ajabu ambao hadi wakati huo ulikuwa umenitia matatani.
Haikuwa kama nilivyojiahidi, nilikuja kushtuka majira ya saa saa kumi na mbili asubuhi. Kitu cha kwanza kusikia zilikuwa ni kelele zilikzokuwa zinapigwa na mwanamke, nilizisikiliza kwa makini nitambue kama kuna hatari yoyote eneo lile lakini nikang’amua kelele zile hazikuwa na wasiwasi wowote na wala hazikuelezea uchungu wowote na badala yake zilikuwa zinaelezea raha fulani na huyo aliyezipiga hakujua kama alikuwa anapiga kelele na kusumbua wengine ambao walikuwa wamelala tena peke yao.
Nikaghafirika na kuwashangaa wawili hao waliokuwa wakifanya mapenzi kwa raha zao na kutupigia kelel wengine.
Nikachukua rimoti na kuwasha luninga bila dhumuni lolote ilimradi tu kukwepa kuzisikia kelele za mwanamke yule ambaye kwa lugha moja ningeweza kusema hajastaarabika.
Nilisimama na kujinyoosha viungo kisha nikauendea mlango wa bafuni, nikaingia kwa ajili ya kujistiri na haja ndogo. Niliacha mlango wazi, sikuwa na shaka kwa sababu nilikuwa mwenyewe.
Nikiwa maliwatoni, nilisikia vitu ambavyo akili yangu ilinituma kuwa ni muhimu nivisikilize, upesi nikarejea chumbani na kukuta mtangazaji akizungumza juu ya habari fulani ya kuvutia.
“……mwandishi huyo ambaye alitimua mbio baada ya tukio anasadikiwa kufanya mauaji hayo kwa makusudi. Mwanamke aliyemshuhudia kwa jicho lake akitokea chumbani mwa marehemu anadai mwandishi alitimua mbio baada ya tukio hilo. Uthibitisho zaidi wa suruali yake ambayo ilisheheni simu ya mkononi ambayo imethibitika ni mali yake, pochi iliyokuwa na pesa taslimu laki tatu, katika suruali palikutwa pia na sumu kali ya kuulia wanyama. Jitihada za kumpata yeye na mkewe waliyekuwa wanaishi naye ziligonga mwamba. Hata hivyo mtoto wao mdo aliyejitambulisha kwa jina la Eva amehifadhiwa na jeshi la polisi Tanzania. Huku upelelezi wa kuhakikisha Samson Josephat na mkewe wanaingizwa nguvuni kwa kosa hilo la mauaji.” Alipomaliza kusoma habari hiyo, ilionyeshwa picha kwa ukaribu kabisa, ilikuwa ni suruali yangu, na pochi ilikuwa yangu lakini sumu na zile pesa hazikuwa mali yangu!!!
Na mbaya zaidi waandishi na maaskari wakaaminishwa kuwa nguo zile zimekutwa katika chumba cha Ezekiel.
“Mungu wangu..kwani yule dada hakuniona kuwa nilikuwa nimevaa suruali yangu na shati zuri kabisa!!” nilijiuliza kwa sauti kama kwamba kuna yeyote wa kushirikiana nami katika mjadala huu.
Wakati nawaza juu ya mchezo huu wa ajabu na mchafu kuwahi kunikumba nikaikumbuka kauli ya mwisho ya mtangazaji…”Mtoto wao mdogo aitwaye Eva…..”
Mapigo ya moyo yakapiga maradufu!!
Eva alinizoea mimi na mama yake tu!! Hakuna mtu mwingine ambaye angeweza kuishi na Eva.
Mtoto wangu jamani!! Nilijikuta katika manung’uniko na majuto wakati sijui najutia jambo gani!!
Mambo yalikuwa yameharibika.
Wakati nahangaisha kichwa changu kufikiria ni jambo gani sahihi natakiwa kufanya, habari ile ikaendelea, wananchi kadhaa walikuwa wakihojiwa juu ya tukio lile, macho yangu yakamwona yule mchezaji aliyeniita mwehu. Alizungumza kwa hisia kubwa sana akinishutumu kuwa alihisi tu kuna jambo baya nimefanya lakini wenzake wakampinga!!
Nilitaka kumpiga ngumi lakini nikakumbuka kuwa kile ni kioo, yeye hayupo pale.
Kwa siku ile sikuiona sura yangu ikirushwa kwenye luninga lakini ningejuaje labda vituo vingine walirusha picha yangu!! Hii ni hatari sana.
Mke wangu yupo wapi?? Hii ni hila ya watu wabaya kwa sababu nimewakimbia basi wamemuunganisha na mke wangu katika tukio mili kuunda ukweli, maana kwa kumwacha yule angenitetea mpaka tone lake la mwisho la damu.
Lakini hakuwepo tena!!
Safari ya kwenda kituo cha polisi kutoa taarifa ikaishia pale na sasa nikawaza mengine, lakini hata yenyewe hayakujiweka katika mkondo mahususi!!!
Nikapagawa!!!
kikofia nmeshafanya yangu tayari sasa kwa muendelezo wa episode ya 6 etc. Tukutane kesho wasaa kama huu huu.