Makapuku Forum

NUKUU NO 1# Sote tunajua kwamba Africa si Ufaransa, Uingereza,Marekani au Urusi. Tunajua shabaha ya nchi za magharibi. Jana walitugawa katika ngazi makabila yetu, koo na vijiji kwa kweli wamekuwa wakirenga kutugawa kwa mbinu ya kuibua makundi ya kiuadui miongoni mwetu. Haya yalisemwa na aliyekuwa waziri mkuu wa Congo -Leopoldville(sasa jamuhuli ya kidemokrasia ya Congo DRC),Patrice Emery Lumumba, katika hotuba yake ya Agosti 25,1960, Patrice Lumumba alizaliwa Julai 2,1925 na kuuawawa January 17,1961
 
 
NUKUU NO 2#; Inawezekana kabisa, nani kweli kwamba jogoo ndiye anayewika, lakini vile vile ni tembe (kuku jike) ndiye anayetaga mayai. Haya yalisemwa na Margaret Hilda Thatcher, aliyezaliwa Oct 13,1925 na kufariki Dunia April 8,2013. Thatcher anatajwa kama kuwa mmoja wa viongozi mashuhuri uingereza akishika wadhifa wa waziri mkuu kuanzia mwaka 1979 hadi mwaka 1990 na kuweka record ya mwanamke pekee kushika wadhifa huo katika nchi hiyo yenye muunganiko wa mataifa manne. Alikuwa kiongozi wa Chama cha conservative mwaka 1975 hadi 1990. Ndiye waziri mkuu aliyekaa kwa muda mrefu zaidi uingereza
 
Namkubali sana Lumumba.
I wish R.i.p could stand for " Return If Possible "
 
 
Wanamuita Iron Lady. Alikuwa ni kiongozi wa shoka sana. Alikuwa na urafiki wa karibu na Rais wa Marekani wa wakati huo, Ronald Regan.

Waziri mkuu mpya wa Uingereza ni mwanamke.
Hivyo ni mwanamke wa pili kushika wadhifa huo baada ya Magreth Thatcher
 
Maneno mazito kabisa
 
Mwanamke wa shoka
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…