Makapuku Forum

Safiiiiii
Kwanza naomba kujua utakuwa unaleta muda gani?? (Hii itasaidia ili tuwe tunapishana muda kuwapa ladha tofauti Makapuku na pia tuweze kujazia nyama)
Kuhusu ushauri utafuata polepole kadri itakavyokuwa unatiririka
Hongera sana kwa ubunifu
Ujumbe huu
uliuona?
Ningependelea hasa jioni ndipo naweza kuwa na utulivu wa kuposti na nisingependa kuingilia ratiba ya shululu na mzee wa 10. Hivyo naomba uweke mpangilio nani aanza, afuate nani na amalizie nani

Njema kabisa habari ya kwako?
 
Ujumbe huu
uliuona?
Sikuuona
ile we na shululu ndo muwe mnachekiana kama mi na Mussolin5 ye akiona sisomeki anaanza kutiririka nikifika natulia nikiona amemamiza ndo naweka magazeti au siku mi nikiwahi ye ananiwait akiniona nimeaga ye anatirirka...
Siku hazilingani hivyo hatujapangiana muda maalumu ila tunafanya hivyo na mambo hayajawahi kuharibika,
Sasa nanyie fanyeni hivyo pia..
 
NUKUU NO #1. Usimamizi unamaanisha kufanya vitu kwa namna sahihi ;Uongozi ni unamaanisha kufanya vitu sahihi. Maneno haya yalisemwa na mtaalamu wa masuala ya menejimenti Ferdinand Peter Drucker, mmarekani mwenye asili ya Australia ambaye maandishi yake yamechangia kwa kiasi kikubwa dhana ya usimamizi wa biashara za kisava. Alizaliwa Nov 19,1909 na kufariki Dunia Nov, 11,2005
 
 
 
NUKUU NO #2. Kama matendo yako yanahamasisha wengine kuwa na ndoto zaidi,kujifunza zaidi, kufanya zaidi na kujitambua zaidi, wewe ni kiongozi. Maneno haya yalisemwa na Rais wa sita wa Marekani, John Quincy Adam. Aliyeongoza taifa hilo Kati ya mwaka 1825 mpaka 1829. Alizaliwa Julai 11,1767 na kufariki Dunia Feb 02,1848.
 
Duuu aliishi muda mrefu kweli
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…