Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linamshikilia Rahma Musa Tito (16), mkazi wa Kijiji cha Msoga, Wilaya ya Chalinze, kwa tuhuma za kumuua mama yake mzazi, Hadija Hemedi Shaha (51), ambaye alikuwa mkulima na mwenye ulemavu wa miguu yote miwili.
Kwa mujibu wa Polisi, tukio hilo lilitokea usiku wa Julai 28, 2026, majira ya saa 5:00, baada ya marehemu kumzuia binti yake kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa ya rafiki yake iliyokuwa ikifanyika karibu na Hospitali ya Msoga, iInadaiwa kuwa Mtuhumiwa alianza kumshambulia mama yake kabla ya kumchoma kichwani kwa kutumia kitu chenye ncha kali.
Aidha, asubuhi ya Julai 29, 2026, Fundi ujenzi aliyekuwa akidai malipo na kufuata mfuko wa saruji alifika Nyumbani kwa marehemu, baada ya kugonga mlango, alifunguliwa na Rahma Musa Tito, ndipo alipobaini mwili wa Hadija Hemedi Shaha ukiwa umelala sakafuni na ukiwa na majeraha kichwani yaliyokuwa yakivuja damu.
Jeshi la Polisi limesema Mtuhumiwa anaendelea kushikiliwa kwa mahojiano na hatua nyingine za kisheria zinaendelea huku uchunguzi wa tukio hilo ukiendelea ili kubaini mazingira yote yaliyosababisha mauaji hayo.
View attachment 3640018