Makapuku Forum

Makapuku Forum

Manii ya nguruwe yanatoka kwa awamu tatu kuu ndani ya hizo dakika:

- Awamu ya Kwanza (Pre-sperm): Majimaji ya wazi yasiyo na mbegu yanayosafisha njia.

- Awamu ya Pili (Sperm-rich): Sehemu yenye mkusanyiko mkubwa wa mbegu za kiume (hii ndio sehemu muhimu zaidi ya utungisho).

- Awamu ya Tatu (Post-sperm/Gel): Majimaji mazito kama jeli au kamasi. Kazi ya jeli hii ni kuziba mlango wa uzazi wa jike (cervix) ili kuzuia mbegu zisimwagike nje baada ya dume kushuka.View attachment 3639459View attachment 3639460
Manii ndyo nn jamani 😎
 
Manii ya nguruwe yanatoka kwa awamu tatu kuu ndani ya hizo dakika:

- Awamu ya Kwanza (Pre-sperm): Majimaji ya wazi yasiyo na mbegu yanayosafisha njia.

- Awamu ya Pili (Sperm-rich): Sehemu yenye mkusanyiko mkubwa wa mbegu za kiume (hii ndio sehemu muhimu zaidi ya utungisho).

- Awamu ya Tatu (Post-sperm/Gel): Majimaji mazito kama jeli au kamasi. Kazi ya jeli hii ni kuziba mlango wa uzazi wa jike (cervix) ili kuzuia mbegu zisimwagike nje baada ya dume kushuka.View attachment 3639459View attachment 3639460
Yaani upotee kisha uje na manii jamani🙆‍♂️🙆‍♂️
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linamshikilia Rahma Musa Tito (16), mkazi wa Kijiji cha Msoga, Wilaya ya Chalinze, kwa tuhuma za kumuua mama yake mzazi, Hadija Hemedi Shaha (51), ambaye alikuwa mkulima na mwenye ulemavu wa miguu yote miwili.

Kwa mujibu wa Polisi, tukio hilo lilitokea usiku wa Julai 28, 2026, majira ya saa 5:00, baada ya marehemu kumzuia binti yake kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa ya rafiki yake iliyokuwa ikifanyika karibu na Hospitali ya Msoga, iInadaiwa kuwa Mtuhumiwa alianza kumshambulia mama yake kabla ya kumchoma kichwani kwa kutumia kitu chenye ncha kali.

Aidha, asubuhi ya Julai 29, 2026, Fundi ujenzi aliyekuwa akidai malipo na kufuata mfuko wa saruji alifika Nyumbani kwa marehemu, baada ya kugonga mlango, alifunguliwa na Rahma Musa Tito, ndipo alipobaini mwili wa Hadija Hemedi Shaha ukiwa umelala sakafuni na ukiwa na majeraha kichwani yaliyokuwa yakivuja damu.

Jeshi la Polisi limesema Mtuhumiwa anaendelea kushikiliwa kwa mahojiano na hatua nyingine za kisheria zinaendelea huku uchunguzi wa tukio hilo ukiendelea ili kubaini mazingira yote yaliyosababisha mauaji hayo.
Screenshot_20260730_164753_InstaPro%20.jpg
 
Tanzania inatarajiwa kuingia katika orodha ya nchi 10 zinazoongoza kwa uzalishaji wa uranium duniani ifikapo mwaka 2029, kupitia mradi wa Mantra Tanzania Limited unaotarajiwa kuzalisha tani 3,000 za madini hayo kwa mwaka na kutoa ajira zaidi ya 4,000.

Meneja wa Uendelevu wa Mantra Tanzania Limited, Majani Wambura, amesema hayo katika kikao cha Mining Breakfast Briefing (MBB) kilichoandaliwa kwa ushirikiano wa Wizara ya Madini na Chemba ya Migodi Tanzania (TCM).

Amesema utafiti uliofanyika umebaini hifadhi ya takribani tani 58,500 za uranium, huku mradi ukitarajiwa kuwa na maisha ya zaidi ya miaka 20 na tafiti zaidi zikiendelea kubaini uwepo wa rasilimali nyingine.

Wambura amesema utekelezaji wa mradi huo utaongeza shughuli za kiuchumi, ajira na mapato ya Serikali, sambamba na kuiweka Tanzania katika nafasi ya ushindani kwenye soko la kimataifa la madini ya uranium kutokana na matumizi makubwa ya madini hayo katika uzalishaji wa nishati ya umeme pamoja na sekta ya afya.

Akizungumza katika kikao hicho, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde amesema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wa sekta ya madini kupitia majukwaa ya majadiliano ili kujenga sekta yenye ushindani, inayovutia uwekezaji na kuchangia zaidi ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Amesema Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji na kutatua changamoto zinazojitokeza ili kuongeza uzalishaji, ajira na mapato.

Screenshot_20260730_165022_InstaPro%20.jpg
 
Baadhi ya viatu vinavyoangushwa na abiria wa mwendokasi kwa nyakati tofauti wakati wa kugombea kuingia kwenye mabasi hayo hasa nyakati za jioni kama vilivyokutwa kwenye Stendi ya Gerezani.

Abiria hapo wamekuwa wakigombania mabasi hayo ambayo yanafanya safari zake za Mbagala-Gerezani na Gerezani-Mbezi.
Screenshot_20260730_165423_InstaPro%20.jpg
 
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia amesema wameweka kanuni ya kuipoka timu pointi tano ikiwa itagundulika haijatumia vyumba vya kubadilishia nguo bila sababu za msingi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Julai 30, 2026 katika Ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia amesema wameandaa vifaa mbalimbali vitakavyotumika katika vyumba vya kubadilishia nguo.

"Kumekuwa na malalamiko mengi ya timu kuhusu vyuma vya kubadilishia nguo, sasa vifaa hivyo tulivyonunua tutavitumia kwa ajili ya kufanyia uchunguzi wa madai mbalimbali ambayo yamekuwa yakisemwa," amesema Karia.

Aidha, Karia amesema ikiwa timu yoyote itatumia vyumba tofauti na vya uwanjani huku uchunguzi ukionekana hakukuwa na shida yoyote, basi timu hiyo itapokwa pointi tano hata kama uwanjani itakuwa imeshinda.
Screenshot_20260730_170245_InstaPro%20.jpg
 
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia amesema kipengele kilichokuwa kikisambaa mitandaoni kuhusu udhibiti wa wachambuzi wa soka hakitakuwa sehemu ya kanuni za shirikisho baada ya kuondolewa kutokana na kutokuwa ndani ya mamlaka yake.

Karia amesema kipengele hicho kilitokana na mapendekezo yaliyotolewa na wadau mbalimbali wa klabu wakati wa mchakato wa kuandaa kanuni, lakini baadaye kikafutwa baada ya kubainika kuwa masuala yanayohusu wachambuzi wa soka yanasimamiwa na sheria za nchi pamoja na vyombo vyenye mamlaka ya kufanya hivyo.

"Ni jambo ambalo zipo mamlaka nyingine zinazosimamia, lile lilikuja kama pendekezo ila sisi tumeona tuliondoe," amesema.

Amesema TFF haina jukumu la kusimamia au kudhibiti wachambuzi wa soka, hivyo haikuwa sahihi kuendelea na kipengele hicho ndani ya kanuni zake.

Karia ametoa ufafanuzi huo wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Julai 30, 2026 katika makao makuu ya TFF yaliyopo Karume, Dar es Salaam.
Screenshot_20260730_170623_InstaPro%20.jpg
 
Mwili wa Mchungaji Silvanus Msuya (44) tayari umewasili kijijini kwao Shighatini, Wilaya ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya taratibu za maziko ambazo zinafanyika katika kanisa la KKKT Usharika wa Shighatini.

Baada ya mwili kuwasili kanisani hapo leo Julai 30, 2026 shughuli mbalimbali za kuaga mwili zinaendelea huku baadhi ya viongozi wa kanisa la KKKT wakiendelea kuwasili katika viwanja vya kanisa hilo ambapo shughuli zote za kiibada zinaendelea.

Baada ya shughuli ya kuaga mwili itakapomaliza salamu mbalimbali za rambirambi zitatolewa na kisha ibada kuanza saa 4 asubuhi.

Mchungaji Silvanus Msuya alifariki dunia Julai 26, 2026 katika hospitali ya Rabininsia jijini Dar es Salaam alipokuwa amelazwa akisumbuliwa na nimonia.

Screenshot_20260730_170734_InstaPro%20.jpg
 
Mbunge wa Tarime Vijijini, Mwita Waitara pamoja na Karoli Jacob na Mara TV wameibuka washindi baada ya Mahakama ya Rufani kufuta hukumu iliyokuwa imewaamuru kwa pamoja kumlipa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Eliakim Maswi, fidia ya Sh6 bilioni katika kesi ya madai ya kashfa.

Uamuzi huo umetolewa leo Jumatano, Julai 29, 2026 na jopo la majaji watatu, Dk Mary Levira, Patricia Fikirini na Issa Maige, ambao wamehitimisha kuwa Maswi hakuthibitisha kwa kiwango kinachotakiwa kisheria kuwa maneno aliyodai yalimkashifu yalichapishwa kupitia chombo cha habari kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari.

Rufaa hiyo ya Madai Na. 1557 ya mwaka 2025 ilikatwa na Waitara, Karoli Jacob na Mara TV wakipinga hukumu ya Mahakama Kuu Kanda ya Musoma iliyotolewa Juni 16, 2025 katika Kesi ya Madai Namba 23 ya mwaka 2023.

Screenshot_20260730_171023_InstaPro%20.jpg
 
Back
Top Bottom