Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,231
- 464,524
Rais wa Marekani Donald Trump ameitaka Iran kusitisha ufadhili wake kwa kundi la Hezbollah akisisitiza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kufanikisha makubaliano ya kudumu ya kusitisha mapigano kati ya pande husika.
Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ofisi ya Oval baada ya kusimamia duru ya pili ya mazungumzo ya ngazi ya Mabalozi kati ya Israel na Lebanon, Trump ameulizwa kama Iran inapaswa kuacha kuifadhili Hezbollah ili kufikia makubaliano hayo ambapo amesisitiza kuwa hilo ni sharti lisiloepukika.
Mazungumzo ya hivi karibuni kati ya Marekani na Iran yameendelea kujikita zaidi katika suala la Nyuklia, huku Tehran ikionekana kupinga masharti yanayolenga kuizuia kuendelea kuunga mkono makundi Washirika katika eneo la Mashariki ya Kati jambo linaloendelea kuwa kikwazo kikubwa katika juhudi za kidiplomasia.
Trump ameeleza kuwa kusitishwa kwa ufadhili wa Hezbollah na Iran ni jambo la lazima ili kufikia makubaliano ya amani na kuongeza kuwa anaamini uwezekano wa Israel na Lebanon kufikia makubaliano ya amani upo iwapo hatua madhubuti zitachukuliwa mapema mwaka huu.
Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ofisi ya Oval baada ya kusimamia duru ya pili ya mazungumzo ya ngazi ya Mabalozi kati ya Israel na Lebanon, Trump ameulizwa kama Iran inapaswa kuacha kuifadhili Hezbollah ili kufikia makubaliano hayo ambapo amesisitiza kuwa hilo ni sharti lisiloepukika.
Mazungumzo ya hivi karibuni kati ya Marekani na Iran yameendelea kujikita zaidi katika suala la Nyuklia, huku Tehran ikionekana kupinga masharti yanayolenga kuizuia kuendelea kuunga mkono makundi Washirika katika eneo la Mashariki ya Kati jambo linaloendelea kuwa kikwazo kikubwa katika juhudi za kidiplomasia.
Trump ameeleza kuwa kusitishwa kwa ufadhili wa Hezbollah na Iran ni jambo la lazima ili kufikia makubaliano ya amani na kuongeza kuwa anaamini uwezekano wa Israel na Lebanon kufikia makubaliano ya amani upo iwapo hatua madhubuti zitachukuliwa mapema mwaka huu.