Mwenyekiti Mstaafu wa CHADEMA, Freeman Mbowe amewaomba wananchi wa Hai kumsamehe aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo, Lengai Ole Sabaya, akieleza kuwa hakuna binadamu asiye na dhambi.
Mbowe amesema hayo wakati wa ibada ya mazishi ya mama wa Mbunge wa Hai, Saashisha Mafue.
"Toka nimetoka gerezani mtagundua tembea yangu imebadilika ni ya kikuu, mtagundua ongea yangu sasa ni ya heshima, mtaona kwamba Mungu ameenda kunibadilisha, nimekuwa mtu bora, yaani amekutana na mimi amenifanya kuwa chuma chake."- Lengai Ole Sabaya, aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai
Rais wa Kenya, William Ruto amesema nchi za Afrika Mashariki zinajadili mpango wa kujenga kiwanda cha pamoja cha kusafisha mafuta katika bandari ya Tanga, kikifanana na kile cha Aliko Dangote cha nchini Nigeria.
Ruto amebainisha kuwa kiwanda hicho kitahudumia nchi kadhaa kwa kutumia mafuta ghafi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Kenya, Sudan Kusini na Uganda.
Kwa upande wake Dangote amesema yuko tayari kujenga kiwanda kama chake chenye uwezo wa kuchakata mapipa 650,000 kwa siku, ikiwa serikali za nchi hizo zitatoa ushirikiano.
Askari wa kikosi maalum cha Jeshi la Marekani aliyeshiriki kwenye operesheni ya kukamatwa kwa aliyekuwa Rais wa Venezuela, Nicolas Maduro, amekamatwa kwa tuhuma za kuweka dau la kamari la kuondolewa kwa Maduro, kabla taarifa hiyo haijawa wazi.
Gannon Ken Van Dyke alijipatia zaidi ya TZS bilioni 1 katika kamari hiyo.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Hamis Mwinjuma amekanusha taarifa kuwa Mashindano ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON 2027) yamehamishwa kutoka Afrika Mashariki kwenda Afrika Kusini.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.