Makapuku Forum

Makapuku Forum

Habari zenu wana Makapuku!

Nimecheka sana na stori zenu za namba na miamala, mko poa sana! Ni furaha kuona familia inakutana na kupata muda wa kucheka pamoja. Shunie , hata sisi tumekumiss magazeti yako, tunajua tu u busy!

Lakini pia, nikikumbuka madhumuni ya uzi huu, ni muhimu sana kuwa na sehemu kama hii ya kupeana moyo na kushare changamoto zetu. Maisha yana mambo mengi, na kuwa na jamii inayokuelewa na kukupa support ni baraka kubwa.

Kama kuna jambo lolote, tusisite kushare. Pamoja tunaweza kusaidiana na kupeana mbinu. Mimi nipo hapa pia kuunga mkono.

Karibuni sana wote!
Atoto Seran leo dada moudgulf Tresor Mandala Obe win-one makaveli10
Hahahhaa furahi tu Poker we hakikisha tu no zetu umezisave ukijisikia unatupia tu. [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema hana mpango wa kukutana na Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Leo XIV, kufuatia tofauti zao za wazi kuhusu suala la Iran na umiliki wa silaha za Nyuklia.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Trump amesisitiza msimamo wake kuwa Iran haipaswi kuruhusiwa kumiliki silaha za Nyuklia, akidai taifa hilo limehusika katika matukio mbalimbali ya vurugu yaliyosababisha vifo vya raia wasio na hatia.

Alipoulizwa kama yuko tayari kukutana na Papa ili kupunguza mvutano huo, Trump alijibu kwa kifupi kuwa haoni umuhimu wa kufanya hivyo kwa sasa.

Hata hivyo, Trump ameeleza kuwa hana uadui binafsi na Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki, akibainisha kuwa tofauti yao ni ya kimtazamo kuhusu masuala ya kimataifa, huku akigusia pia kuwa ndugu wa Papa anaunga mkono vuguvugu lake la kisiasa la MAGA (Make America Great Again)
.
millardayo-20260417-0001.jpg
 
Mtoto mdogo ameibua hisia na kuvutia maelfu ya Watu baada ya kuonyesha ujasiri wa kipekee kwa kumkimbilia Papa Leo XIV mara baada ya ibada ya Misa nchini Cameroon.

Katika tukio hilo, mtoto huyo ameonekana kuvuka eneo la usalama bila woga na kumfikia Papa, hatua iliyowashangaza walinzi pamoja na waumini waliokuwepo.

Badala ya taharuki, Papa alionekana kumkaribisha kwa utulivu na upendo, akionesha ishara ya ukarimu na kujali, jambo lililowagusa wengi waliokuwa wakishuhudia tukio hilo.

Wengi mitandaoni wamesifu ujasiri wa mtoto huyo, wakieleza kuwa kitendo chake kinaonyesha imani ya dhati na moyo wa kumwamini kiongozi huyo wa dini, huku wengine wakivutiwa na namna Papa alivyolipokea tukio hilo kwa upole na busara.

Tukio hilo sasa limegeuka kuwa gumzo, likitafsiriwa kama picha ya uhusiano wa karibu kati ya viongozi wa dini na waumini wao, hasa watoto.
millardayo-20260417-0002.jpg
 
Rais wa Cuba, Miguel Díaz-Canel, amesema Taifa lake liko tayari kupambana endapo Marekani itachukua hatua za Kijeshi, licha ya kusisitiza kuwa hawatamani vita.

Akizungumza katika mkutano mkubwa wa kuadhimisha miaka 65 ya Mapinduzi ya Kisoshalisti, Díaz-Canel amesema hali ya sasa ni ngumu na inahitaji taifa kuwa tayari kukabiliana na vitisho vikubwa, ikiwemo mashambulizi ya kijeshi.

“Hatutaki hali hiyo, lakini ni wajibu wetu kujiandaa ili kuizuia, na ikiwa haitakwepeka, basi tuishinde,” alisema.

Kauli hiyo inakuja wakati mvutano kati ya Cuba na Marekani ukiendelea kuwa juu, huku mgogoro wa nishati ukizidi kuathiri maisha ya kila siku kufuatia vikwazo vya Marekani.

Wakati huo huo, Donald Trump amesema huenda akaivamia Cuba baada ya kumaliza mzozo unaohusisha Iran, akiitaja nchi hiyo kuwa imekuwa ikikumbwa na matatizo kwa muda mrefu.
millardayo-20260417-0003.jpg
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetoa taarifa kikieleza kuwa April 15, 2026, Mwenyekiti wake, Tundu Lissu, amewasilisha mapendekezo muhimu kwa Rais wa zamani wa Jamhuri ya Malawi, Lazarus Chakwera, akiwa mahabusu katika Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam, wakati Lissu alipopata fursa ya kukutana na Kiongozi huyo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA, Brenda Rupia, Lissu amewasilisha hoja kadhaa zinazolenga mustakabali wa demokrasia na utawala wa sheria Nchini Tanzania, miongoni mwa hoja hizo ni pamoja na kueleza kuwa kesi ya uhaini inayomkabili inatokana na msimamo wake wa “No Reforms, No Election,” akisisitiza kufutwa kwa kesi zote zinazomkabili yeye na chama, pamoja na utayari wake kushiriki mazungumzo akiwa huru.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa Lissu pia amependekeza kufanyika kwa uchunguzi huru wa kimataifa kuhusu matukio ya Oktoba 2025 kupitia Taasisi za Kikanda kama SADC, pamoja na kuwepo kwa mazingira wezeshi yatakayowezesha mazungumzo ya kweli na utekelezaji wake.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa uwajibikaji wa taasisi mbalimbali za umma ikiwemo Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), akirejea pia mapendekezo ya ripoti za Jaji Nyalali (1992) na Jaji Chande (2023), kuhusu mageuzi ya kisiasa na kiutawala.

Katika hatua nyingine, Lissu ameeleza umuhimu wa kufanyika kwa mageuzi ya mfumo wa uchaguzi, ikiwa ni pamoja na kuundwa kwa chombo huru cha kusimamia uchaguzi, kwa kuzingatia ripoti za waangalizi wa uchaguzi kuanzia mwaka 1995 hadi 2025, pamoja na mapendekezo ya Tume za Jaji Warioba na Nyalali.

Wakati huo huo, CHADEMA imesema Lissu amepatiwa nakala ya uamuzi wa Mahakama ya Rufani uliotolewa Aprili 15, 2026 unaoruhusu chama kuendelea na shughuli zake, ambapo baada ya kuupitia uamuzi huo, ametoa wito kwa Wanachama na Watanzania kwa ujumla kujiandaa kwa hatua zinazofuata za kisiasa, hususan maandalizi ya mikutano ya hadhara.
.
millardayo-20260417-0004.jpg
millardayo-20260417-0005.jpg
millardayo-20260417-0006.jpg
 
Simanzi imetawala katika Mtaa wa Mnazi, Kata ya Ng’ambo mkoani Kilimanjaro, baada ya mwanamke mmoja anayefanya biashara ya chakula, Restituta Moshiro (40), kukutwa ameuawa na mwili wake kutupwa kwenye shamba la mahindi, ukiwa na majeraha yanayoashiria aliburuzwa na kukabwa kabla ya kukutwa na mauti.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo, Aprili 17, 2026, wakati mwanamke huyo, aliyekuwa akifanya biashara ya kuuza chakula kando ya barabara kuu ya Moshi–Arusha, eneo la Shaa Tours, akirejea nyumbani kwake.

Mwili wa Restituta, anayefahamika zaidi kama Mama Baraka, umekutwa ukiwa na damu puani, baada ya nguo yake ya ndani kukutwa imevuliwa na kutupwa pembeni ya mwili.

Pamoja na nguo hizo, vifaa alivyokuwa amebeba kwa ajili ya mwanaye wa miezi saba, ikiwemo maziwa, unga wa lishe na mwamvuli kwa ajili ya mvua, vilikutwa vimetapakaa hatua chache kutoka ulipo mwili wake.

Akizungumza katika eneo la tukio, Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Moshi (OCD), Azizi Kalokola, amesema Jeshi la Polisi tayari limeanza upelelezi wa kina kubaini mazingira yaliyosababisha kifo hicho cha kutatanisha.
mwananchi_official-20260417-0001.jpg
 
Wakazi wa mji wa Netivot kusini mwa Israel wametakiwa kubaki majumbani mwao baada ya nyuki kuvamia maeneo ya biashara na makazi, tukio lililosababisha taharuki na usumbufu.

Tukio hilo lililotokea Aprili 15, 2026, lilianza ghafla wakati kundi kubwa la nyuki lilipoonekana katika eneo la kituo cha manunuzi chenye shughuli nyingi mjini humo.

Mashuhuda wamesema waliona makundi makubwa ya nyuki yakifunika magari, miti na maduka, hali iliyowalazimu wanunuzi na wafanyabiashara kufunga milango na kujifungia ndani kwa usalama.

Mamlaka za eneo hilo zilichukua hatua za haraka kwa kutoa tahadhari kwa wakazi kuepuka maeneo yaliyoathirika huku wakisisitiza umuhimu wa kubaki ndani wakati timu za dharura na wataalamu wa nyuki wakiendelea na juhudi za kudhibiti na kuondoa kundi hilo.

Tukio la Netivot sasa limevutia pia watafiti wa kisayansi wanaotaka kufahamu kilichosababisha mkusanyiko huo mkubwa wa nyuki na iwapo matukio kama hayo yanaweza kuongezeka siku zijazo.

mwananchi_official-20260417-0002.jpg
 
Droo ya hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB iliyopangwa leo, Ijumaa, Aprili 17, 2026 imeibua mechi kadhaa za kusisimua za timu ambazo zilionyeshana upinzani mkali katika mechi za Ligi Kuu msimu huu.

Katika droo hiyo, Simba imepangwa kukutana na TRA United, Singida Black Stars dhidi ya Coastal Union, JKT Tanzania dhidi ya Yanga na Mashujaa FC dhidi ya Azam FC.

Simba dhidi ya TRA United ni mechi inayokumbushia pambano la mzunguko wa pili wa Ligi Kuu baina ya timu hizo lililochezwa wiki iliyopita ambalo lilimalizika kwa sare tasa.

Mashujaa dhidi ya Azam nazo zilikutana Aprili 19, 2026 katika mechi ya Ligi Kuu ambayo ilimalizika kwa sare tasa.

Hata hivyo Coastal Union na JKT Tanzania zina fursa ya kulipa kisasi cha mechi za Ligi Kuu zilizopoteza dhidi ya Singida Black Stars na Yanga au kuendeleza unyonge.

mwananchi_official-20260417-0003.jpg
 
Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Iringa Vijijini kimetangaza rasmi kuanza kwa mchakato wa ndani wa kuwapata wanachama watakaowania nafasi ya ubunge katika Jimbo la Isimani, baada ya kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, William Lukuvi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Aprili 16, 2026 na Katibu wa CCM Wilaya ya Iringa Vijijini, Sure Mwasanguti, wanachama wote wenye sifa wametakiwa kujitokeza kuchukua na kurejesha fomu za kuomba uteuzi kuanzia Aprili 17 hadi Aprili 18, 2026.

Amesema fomu zitatolewa kuanzia saa 1:00 asubuhi hadi saa 10:00 jioni katika ofisi za chama wilayani humo, likiwa ni sehemu ya maandalizi ya kujaza nafasi hiyo kupitia taratibu za chama.

Kifo cha Lukuvi kimehitimisha safari ndefu ya uongozi wa zaidi ya miongo mitatu katika Jimbo la Isimani, alikochaguliwa kwa mara ya kwanza mwaka 1995 na kuendelea kuchaguliwa hadi 2025.
mwananchi_official-20260417-0004.jpg
 
Meli nne za mizigo zimevuka mstari wa zuio lililowekwa na Marekani baada ya kuondoka katika bandari mbalimbali za Iran kuoitia mlango wa Hormuz, huku taarifa zikionyesha kuwa safari hizo zimefanyika licha ya vikwazo vinavyoendelea.

Kwa mujibu wa data za ufuatiliaji wa trafiki ya majini, meli zote zilizobainika ni za kubeba makontena, ambapo tatu zinapeperusha bendera ya Iran na moja, Tava 4, ikiwa imesajiliwa nchini Comoro.

Zuio hilo la Marekani lilianza kutekelezwa Jumatatu, lakini meli hizo ziliripotiwa kuvuka katika nyakati tofauti siku hiyo.

Miongoni mwa meli hizo ni Azargoun, iliyoondoka katika Bandari ya Shahid Rajee na kuvuka mstari huo ikielezwa kuwa inaelekea Kandla, kaskazini magharibi mwa India.

Nyingine ni Ashkan3, iliyoondoka katika Bandari ya Chabahar mashariki mwa Iran na imeelekea Karachi nchini Pakistan.

mwananchi_official-20260417-0005.jpg
 
Back
Top Bottom