Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20250424_073506_Chrome.jpg
Screenshot_20250424_073522_Chrome.jpg
 
Je ni nani anaweza kuwa Papa..!?

Papa ni Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani. Miongoni mwa waumini wa Kanisa Katoliki, Papa anachukuliwa kama mrithi wa Mtume Petro hapa duniani.

Baada ya Yesu Kristo Kufufuka na Kupaa alimwacha Mtume Petro kuwa Kiongozi wa mitume na wafuasi wengine wa Yesu.

Petro anachukuliwa kama Kiongozi wa mwanzo wa Kanisa. Kwa hiyo, kwa Wa Katoliki, Papa anachukua mamlaka ya Petro.

Kwa mujibu wa Sheria za Kanisa Katoliki, Mkatoliki yeyote ambaye amekwisha batizwa, anaweza kuchaguliwa kuwa Papa na Kiongozi wa Kanisa Katoliki.

Kwa sasa Kanisa Katoliki linawaumini wanaokadiriwa kufikia bilioni 1.4. Muumini yeyote miongoni mwa hao bilioni 1.4 anaweza kuwa Papa.

Uchaguzi wa Papa huwa unafanywa na makaridinali ambao wana umri chini ya miaka 80. Kwa sasa kuna jumla ya Makaridinali 252. Makaridinali watakaopiga kura ya kumchagua Papa ni135.

Mpaka sasa, licha ya kwamba, Sheria ya Kanisa inataja kwamba muumini yeyote anaweza kuwa Papa, karibu mara zote Mapapa ambao wametangulia wamekuwa na hadhi ya Ukaridinali.

Miaka ya nyuma mchakato wa kumpata Papa mpya umekuwa ukianza siku 10 hadi siku 15 baada ya kiti cha Papa kubaki wazi...!
Screenshot_20250424_081226_InstaPro2%20.jpg
 
Papa amefariki kutokana na Stroke.

Taarifa iliyotolewa na Vatican inaeleza kwamba kabla ya kufariki Papa Francis alipata Kiharusi(Stroke) hali iliyosababisha moyo kushindwa kufa kazi.

Taarifa hiyo inaeleza kwamba madaktari walifanya jitihada kurudisha moyo kufanya kazi lakini ilishindikana.

"Papa amefariki kutokana na Stroke", inaeleza sehemu ya taarifa rasmi ya sababu ya kifo cha Papa.

Pia hati ya kifo imetaja magonjwa mengine yalikuwa yanamsumbua Papa ni pamoja na homa ya mapafu, kushindwa kupumua, shinikizo la juu la damu na ugonjwa wa Kisukari.

Kwa taratibu za kimatibabu ugonjwa ambao mgonjwa huwa anakuwa nao muda mfupi au masaa machache kabla ya kifo chake ndio huwa unatajwa kwenye cheti cha kifo kama sababu ya kifo.

Baada ya Papa Kufariki, Kardinali Msimamizi wa Nyumba ya Papa huwa anaitwa jina lake mara tatu kwa kutaja jina lake la ubatizo na kumuuliza, Fulani umelala.

Baada ya hapo ndio kifo cha Papa hutangazwa. Papa Francis amefariki akiwa na umri wa miaka 88...!
Screenshot_20250424_081501_InstaPro2%20.jpg
 
Kaburi langu lisiwe na mbwembwe, liandikwe jina langu tu: Fransicus

Wosia wa mwisho wa aliyekuwa kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis umeeleza jinsi utaratibu wa mazishi yake utavyokuwa. Katika Wosia huo, Papa ameeleza kwamba, lazima azikwe katika Kanisa Kuu la Bikira Maria.

Kanisa Kuu la Bikira Maria liko Roma, Italia haliko Vatican ambako Mapapa wengi wamekuwa wakizikwa kwenye Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro.

"Katika maisha yangu nimekuwa nikimtumainia Mama Bikira Maria daima, kwa sababu hii nizikwe kwenye Kanisa hilo nikisuburi kufufuliwa siku ya Ufufuo", imesema taarifa hiyo.

Papa Francis amekuwa akiishi maisha ya ufukara hali ambayo ameisisitiza kuhusu maziko yake katika Wosia wake. Wosia wake unaeleza kwamba, mazishi yake yasiwe ya kifahari na wala kaburi lake lisiwe na mapambo yoyote isipokuwa liandikwe jina lake tu. Fransicus.

Kuhusu gharama za maziko, Wosia wa Papa umeeleza kwamba, gharama zote zimetolewa na mfadhili ambaye hakutajwa jina na zimekabidhiwa kwa Kardinali Rolandas Makrickas.

Mwisho wa Wosia wake Papa amesema, "Mola awape thawabu ifaayo wale wote walionipenda na wanaoendelea kuniombea. Mateso ambayo yamenizonga katika kipindi cha mwisho cha maisha yangu, nayatoa kwa Bwana, kwa ajili ya amani duniani na udugu kati ya watu."
Screenshot_20250424_082052_InstaPro2%20.jpg
 
Tazama Vatican wametoa picha zinazoonyesha mwili wa Papa Francis ukiwa kwenye jeneza.

Papa atazikwa Siku ya Jumamosi tarehe 26 kwenye Kanisa Kuu la Bikira Maria huko Roma Italia.

Kesho mwili wa Papa Francis utawekwa kwenye Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro Vatican kwa ajili waumini kutoa heshima za mwisho..!
Screenshot_20250424_082254_InstaPro2%20.jpg
Screenshot_20250424_082314_InstaPro2%20.jpg
 
Je Vatican ni wapi na Roma ni wapi....!?

Tuchukulie hivi, Dar es Salaam si iko Tanzania. Sasa hiyo ndio Roma iko katika nchi ya Italy. Halafu tuseme hivi, Ubungo si iko Dar es Salaam, hiyo ndio kama Vatican sasa.

Vatican iko ndani ya Jiji la Roma katika nchi ya Italia lakini Vatican sio sehemu ya Italia. Vatican ni nchi kamili inayojitegemea yenyewe tena yenye mamlaka kamili na serikali yake yenyewe.

Vatican ina Rais wake. Rais wake ni Papa. Vatican ina serikali yake na baraza la mawaziri ambao ni makardinali. Vatican ina mabalozi wake katika nchi nyingine kama zilivyo nchi nyingine huru. Pia Vatican ina jeshi lake.

Vatican ndio nchi ndogo zaidi duniani. Kwa kulinganisha, ukubwa wa eneo la nchi ya Vatican unazidi kidogo eneo la Kariakoo kwa hekta 9.

Vatican ina ukubwa wa Hekta 49. Vatican ina wakaazi wanaokadiriwa kufikia 882. Ndani ya Vatican eneo analoishi Papa na kufanya shughuli zake za kila siku linaitwa Holy See.

Baada ya Papa kufariki, Vatican inakuwa chini ya Kardinali Kiongozi anayeitwa Kardinali camerlengo ambaye kwa sasa ni Kardinali Kevin Farrell raia wa Marekani.

Katika kipindi anachofariki Papa, Kardinali huyu anamajukumu ya kutangaza kifo cha Papa, kuharibu Pete na Muhuri aliyokuwa anatumia Papa, kusimamia mazishi ya Papa pamoja na kuandaa mchakato wa kupatikana Papa mwingine.

Huko Vatican hakuna hospitali, kwa hiyo kimsingi hakuna raia wa kuzaliwa wa Vatican. Watu wanapata uraia wa Vatican kulingana na hadhi yao na majukumu yao katika Kanisa na ndani ya Vatican yenyewe.

Papa ana makanisa makuu manne ambayo yanaitwa Basilicas. Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro huko Vatican ndio maarufu zaidi lakini Kanisa Kuu la Roma kwa jina lingine ndio Kanisa lenye hadhi kubwa zaidi.

Mapapa wengi wamekuwa wakizikwa katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro lakini ambalo liko ndani ya Vatican, lakini Papa Francis yeye atazikwa katika Kanisa Kuu la Bikira Maria ambalo liko nje ya Vatican lakini bado liko Roma lakini ni mali ya Vatican. Papa pia ndie Askofu wa Jimbo la Roma..!
Screenshot_20250424_082431_InstaPro2%20.jpg
Screenshot_20250424_082453_InstaPro2%20.jpg
 
Ujue utaratibu wa Kuchagua Papa.

Baada ya Kifo cha Papa shughuli zote za Kanisa Katoliki huwa chini ya Baraza la Makardinali.

Hawa wanasimamia shughuli za kila siku za Kanisa na kutoa maamuzi juu ya mambo ya dharura tu. Baraza la Makardinali ndio linajukumu pekee la kuchagua Papa mwingine.

Baraza hili ndio hutangaza rasmi tarehe ya kuzikwa Papa na tarehe ya kufanya uchunguzi wa Papa mwingine.

Tayari Baraza la Makardinali limekwisha tangaza kwamba, Papa Francis atazikwa siku ya Jumamosi, huko Roma. Bado tarehe ya kufanya uchaguzi wa Papa mwingine bado haijatangazwa

Kwa kawaida, utaratibu unataka ibada na maomboleze ya Kifo cha Papa yafanyike kwa muda wa siku 9 mfululizo.

Katika siku hizo 9, kama hakuna kipingamizi kingine mazishi yanapaswa kufanyika kuanzia siku ya 4 na si zaidi ya siku ya 6.

Baada ya Papa kuzikwa, Kanisa litaendelea kuomboleza hadi siku 9 zitimie. Kisha uchaguzi wa Papa utafuata.

Siku ya kwanza, Makardinali wote ambao wana sifa ya kupiga kura watafanya ibada. Mchana wa siku hiyo wataandama kwenda kwenye chumba maalumu kilichoandaliwa.

Siku hiyo watakulipa kiapo cha uaminifu. Katika kipindi chote hicho, Makardinali hawaruhusuwi kuwasiliana kwa njia yoyote ile wala kusoma magazeti mpaka atakapopatikana Papa Mpya.

Siku zinazofuata uchaguzi utafanyika. Kura zipigwa kwa kura ya siri. Kardinali atakayepata theluthi mbili ya kura zote ndie atatangazwa kuwa Papa.

Iwapo baada ya siku 3 mfululizo za kupiga kura kutakuwa hakuna Papa aliyepatikana, Makardinali watapewa siku 1 ya kupumzika na kutafakari.

Kisha watarudi tena kuendelea kupiga kura hadi Papa achaguliwe. Iwapo kura zitapigwa mara 7 na hakuna aliyechaguliwa, Makardinali watapumzika tena siku 1.

Iwapo kura zimetosha, Kardinali aliyechaguliwa ataitwa mbele ya Baraza la Makardinali na kuulizwa, "Je, unakubali kuchaguliwa kwako kuwa Papa?" Iwapo atakubali ataulizwa tena " Je Unataka kuitwa jina gani?" Baada ya Papa Mteule kutoa jina, mashahidi wawili wanaohusika na sherehe za kipapa wataandaa kiapo na Jina la Papa.

Kuanzia muda huu, Kardinali aliyeshinda anakuwa na Mamlaka kama Papa. Kisha Makardinali hula kiapo cha uaminifu. Baada ya hapo dunia itatangaziwa kupatikana kwa Papa Mpya.
Screenshot_20250424_081501_InstaPro2%20.jpg
 
Ni Moshi mweusi au Ni Moshi mweupe...!?

Siku sio nyingi, Kanisa Katoliki litakuwa linapata Kiongozi Mpya. Kwa kawaida, uchaguzi wa Papa Mpya unapaswa kufanyika baada ya siku 15 toka kiti cha Papa kiwe wazi na si zaidi ya siku 20.

Makardinali wenye umri chini ya miaka 80 ndio hupiga kura ya kumchagua Papa. Mara nyingi Papa anachaguliwa miongoni mwa Makardinali, lakini mwanaume Mkatoliki yeyote ambaye amebatizwa anaweza kuchaguliwa kuwa Papa.

Siku ya Kwanza ya Uchaguzi, Makardinali wote wenye sifa ya kumchagua Papa wanakaa ndani ya Kanisa.

Mtu yeyote ambaye sio Kardinali mwenye sifa anaondoka kwenye Kanisa hilo. Kardinali mwenye umri mdogo zaidi kuliko wenzake anafunga milango.

Karatasi za Kura zinagawiwa miongoni mwa Makardinali. Kila Kardinali anaandika jina la mtu anayetaka kumchagua. Baada ya Makardinali wote kupiga kura, kura zinahesabiwa.

Kuna Makardinali watatu wanakuwa wamechaguliwa kupitia kura zilizopigwa. Wawili wanaandika jina, watatu anasoma jina kwa sauti.

Iwapo kuna litakalopata theluthi mbili ya kura zote. Papa atakuwa amepatikana. Iwapo hakuna jina lililopata idadi ya kura zinazohitajika kura zitarudiwa. Siku ya Kwanza, Makardinali huwa wanapiga kura mara 1 tu siku nyingine wanapiga kura mara 3.

Iwapo kura zitakuwa hazikutosha kumpata Papa, kura pamoja na makaratasi yote yaliyotumika siku hiyo huwa yanachomwa moto.

Ili kutoa moshi ambao huwa unaashiria Papa hajapatikana, kura huwa zinachanganywa na kemikali nyingine zinazoitwa potassium perchlorate, anthracene sulphur.

Kemikali hizo hufanya Moshi Mweusi ambao ni ishara kwamba Papa hajapatikana. Kwa siku kura huchomwa mara moja tu.

Iwapo kura zitakuwa zimetosha na Papa amechaguliwa. Kura zote za siku hiyo huchomwa na kuchanganywa na kemikali potassium chlorate, lactose na rosin. Kemikali hizo zinapochomwa moshi mweupe hutokea na kuashiria Papa amepatikana.

Baada ya taratibu zingine kukamilka, Kardinali Mwandamizi huongozana na Papa aliyechaguliwa kwenye Dirisha la Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro na kuwatangazia waumini. Tunaye Papa. Kisha Papa hutoa baraka zake za Kwanza kwa Mji wa Roma na Dunia...!
Screenshot_20250424_083154_InstaPro2%20.jpg
 
Magazeti yako yote ni ya tarehe 24 Aprili, 2024

Ni bahati mbaya Mjukuu ama umeamua kuturudisha nyuma kidogo Wazee wako

Good morning
Kheeeee. Jamanjii mnisamehee tu bila kuniambia nisingejua hata babu muyasome tu hivyohivyoo
 
Kheeeee. Jamanjii mnisamehee tu bila kuniambia nisingejua hata babu muyasome tu hivyohivyoo
Pole Mjukuu, bahati nzuri nina maktaba hapa nyumbani iliyosheheni magazeti ya tangu Mwaka 47 kwahiyo ikawa rahisi ku-relate habari 🤗

Heri ya Pasaka Mjukuu, hata kama nimechelewa kukuwish pitia hapa nyumbani nikukamatie jogoo mmoja ukale 🤗
 
Pole Mjukuu, bahati nzuri nina maktaba hapa nyumbani iliyosheheni magazeti ya tangu Mwaka 47 kwahiyo ikawa rahisi ku-relate habari

Heri ya Pasaka Mjukuu, hata kama nimechelewa kukuwish pitia hapa nyumbani nikukamatie jogoo mmoja ukale
Asante Babu na kwako pia haya leo soma ya leo leo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom